KINGAZI BLOG: October 2016

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Thursday, October 27, 2016

BREAKING NEWS: HAYA HAPA MATOKEO YA MTIHANI DARASA LA SABA(7) 2016


Serikali  imetangaza  matokeo  ya  mtihani  wa  darasa  la  7 kwa mwaka 2016  ambapo ufaulu  umeongezeka  kwa asilimia 2.52 na shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema  ya  mkoani Shinyanga

 Kutokana na ukweli kwamba si kila mtu mwenye acces na mtandao na itambidi kwenda internet cafe kuangalia,KINGAZITZ BLOG tumekurahisishia mambo.

Endapo utahitaji huduma ya kuangaliziwa jina la mwanao au ndugu yako fanya yafuatayo;

1.Tuma  jina la mwanao,mkoa,wilaya na shule aliyosoma

(mfano:juma paul-PWANI,KIBAHA,UHURU PRIMARY) 

kwenda namba 0716528779

2.Huduma hii uatozwa tshs 1000 tu.(kwa ajili ya kuisuport kingazitz blog)

3.Tuma pesa kwenda namba 0755542721-MPESA
                                             0716528779-TIGO PESA   
5.Utajibiwa ndani ya dk.moja tu,tuma pesa kwanza ndio ujibiwe


BREAKING NEWS:HAYA HAPA MATOKEO YA MTIHANI DARASA LA SABA(7)2016


Serikali  imetangaza  matokeo  ya  mtihani  wa  darasa  la  7 kwa mwaka 2016  ambapo ufaulu  umeongezeka  kwa asilimia 2.52 na shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema  ya  mkoani Shinyanga

 Kutokana na ukweli kwamba si kila mtu mwenye acces na mtandao na itambidi kwenda internet cafe kuangalia,KINGAZITZ BLOG tumekurahisishia mambo.

Endapo utahitaji huduma ya kuangaliziwa jina la mwanao au ndugu yako fanya yafuatayo;

1.Tuma  jina la mwanao,mkoa,wilaya na shule aliyosoma

(mfano:juma paul-PWANI,KIBAHA,UHURU PRIMARY) 

kwenda namba 0716528779

2.Huduma hii uatozwa tshs 1000 tu.(kwa ajili ya kuisuport kingazitz blog)

3.Tuma pesa kwenda namba 0755542721-MPESA
                                             0716528779-TIGO PESA   
5.Utajibiwa ndani ya dk.moja tu,tuma pesa kwanza ndio ujibiwe


Tuesday, October 18, 2016

PICHA 8: Wasichana 21 waliokuwa wametekwa na Boko Haram walivyokutana na familia zao.

 Aprili 2014 zaidi ya wasichana 270 walitekwa wakiwa shuleni katika mji wa Chibok na wapiganaji wa Boko Haram, mpaka leo ikiwa ni baada ya zaidi ya miaka miwili tangu kutekwa kwa wasichana hao, Alhamisi ya October 13, 2016  ziliripotiwa taarifa za kuachiwa kwa baadhi ya wasichana hao na kurejeshwa baada ya mazungumzo kati ya viongozi wa serikali ya Nigeria na viongozi wa Boko Haram.

Leo October 17 2016 Wasichana 21 wa Chibok hatimaye wamekutana na familia zao







Jambazi Awajeruhi Kwa Bomu Askari na Raia Wanne Kigoma

Polisi na raia wanne wamejeruhiwa kwa bomu la kutupwa kwa mkono walipokuwa wakimkamata mtuhumiwa wa ujambazi kwenye Kijiji cha Uvinza mkoani Kigoma. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 14. 

Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Yahya Kamuhanda (49) mkazi wa kijiji hicho. Mtui aliwataja majeruhi hao kuwa ni askari polisi F.3187 Koplo Isaya na raia Saidi Mohamed, Seleman Kashali, Joseph Daudi na Hassan Nasibu, wote wakazi wa Kijiji cha Uvinza. 

Alisema askari walipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba Kamuhanda anajiandaa kufanya uhalifu hivyo waliweka mtego eneo la Uvinza Madukani alikokwenda kununua mahitaji. 

Alidai kuwa alipotambua anafuatiliwa alitupa bomu ndipo polisi walimpiga risasi mguuni na wananchi walimvamia na kumshambulia kabla ya askari kutumia nguvu kumwokoa asiuawe kwa kipigo. 

Mtui alisema mtuhumiwa alipohojiwa alisema alificha bunduki kijijini kwao Lukole wilayani Ngara mkoani Kagera, ambako askari walikamata SMG yenye namba 78GA5062 ikiwa imefukiwa ardhini.

 Pia, walikamata magazini saba, moja ilikuwa na risasi 40, nne (risasi 30 kila moja) na mbili (risasi 20 kila moja) na risasi 75 zilikuwa kwenye mfuko wa sandarusi. Pingu moja na funguo zake, maski tisa na laini 20 za mtandao wa Halotel ambazo hazijasajiliwa. 

Mtui alisema mtuhumiwa huyo alifariki dunia juzi akipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma (Maweni). Alisema majeruhi wote watano walipata matibabu hospitalini hapo na waliruhusiwa kurudi nyumbani. 


Monday, October 17, 2016

Watumishi TBS na TRA Waliohusika n a Upotevu wa Makontena 100 Bandarini Watakiwa Kujisalimisha Haraka kabla Hawatumbuliwa


Serikali imewataka baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) walioshirikiana na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitisha  makontena zaidi ya 100 bila kukaguliwa na shirika hilo katika Bandari ya Dar es Salaam kujisalimisha haraka.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alitoa agizo hilo jana wakati akizindua baraza la wafanyakazi wa TBS.

“Nimeanza kukusanya orodha ya majina ya watu waliosaidia kupitisha makontena haya na nikija nayo hawatapona,”alisema.

Aliwataka wote wanaojijua kuhusika kujisalimisha mapema na kutubu ili wasamehewe kabla ya hatua hiyo.

Makontena hayo yalipitishwa katika Bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni bila ya kuthibitishwa na TBS.

Pia, aliitaka TRA kuacha kutoa makontena bila ya shirika hilo kuthibitisha au kukagua ubora wa bidhaa zinazoingizwa nchini kwa sababu ndilo lenye mamlaka hayo.

Alisema watakaotubu watapaswa kusema walishiriki vipi na lini, walishirikiana na nani na kutaja sehemu yalikopelekwa ili Serikali iweze kusaidia kukomesha hali hiyo.

Mwijage alisema anaamini waliofanya hivyo katika mamlaka hiyo walifanya kwa utashi wao bila ya ushiriki wa viongozi wao na kwamba sasa wakati umefika wa kukomesha tabia hiyo.

Alilitaka baraza hilo jipya la wafanyakazi kushirikiana na menejimenti kuhakikisha matatizo yanayojitokeza yanapatiwa ufumbuzi kwa masilahi ya nchi na kwamba Serikali itahakikisha inaongeza vitendea kazi na watumishi ili kufikia malengo ya shirika.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk Egid Mubofu alisema baraza hilo lina wajumbe 48 wanaotoka katika vitengo mbalimbali na litakaa kwa muda wa miaka mitano.

“Baraza hili linaundwa kutokana na mkataba wa menejimenti na Chama cha Wafanyakazi (Raawu),” alisema Dk Mubofu.

Alisema wafanyakazi wanatakiwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu katika majukumu yao ya kila siku.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TBS, Profesa Mekanya Maboko alilitaka baraza hilo kufanya kazi kwa kushirikiana na menejimenti na bodi kuhakikisha shughuli za udhibiti wa ubora zinafanyika kwa ufanisi.

“Bodi itaendelea kuisimamia menejimenti na kuishauri ifanye kazi kwa kuzingatia sera na sheria,” alisema.

CHOMBEZO: NILAMBE HUMOHUMO ==2

Image result for booty ebony
Nilambe Humo Humo - 2
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA

SEHEMU YA PILI

Unadhani nilifanikiwa kuinua domo langu na kumwambia japo ninakupenda tu? Thubutu! Kila nilipojitahidi kusema sasa nimwambie, ulimi ulikuwa mzito na pale ulipokuwa mwepesi maneno yalifanya mgomo! 
Mgomo ulipojisahau yalitoka maneno mengine tofauti kabisa na ninakupenda! 
Mpaka muda wa maongezi niliomuomba tuongee unakwisha na yeye kuniaga sikuwa nimemwambia lolote la
maana. Nilibaki nimeduwaa kwa muda wakati wakati akiyoyoma na kunipa nafasi ya kuyafaidi maungo yake kwa nyuma. 
Ghafla akageuka na kunitazama. 
Macho yetu yakagongana. 
Akatahayari, labda kwa vile alivyogundua kwamba alikuwa akitazamwa kifisifisi. Akageuza na kurudi kwa madaha akitumia hatua zilezile za miss Tanzania wa mwaka huu mpaka pale nilipokuwa nimesimama. Akaniangalia kwa muda kabla hajaniuliza kwa wasiwasi.
‘’Una nini Ibra?’’
“Sina kitu Shamsa!’’
‘’Kweli?’’ 
“Haki ya Mungu vile!’’
“Au nimekukatili?! Bado hujamaliza kiu yako ya maongezi na mimi?”
“Nilishamaliza kabisa. Amini nilitaka tu kujua kidogo kuhusu utendaji kazi wa Socket Bracker na vitambuzi vya Short, lakini jinsi ulivyonielekeza inatosha kabisa. Ahsante sana Da! Shamsa, Mungu akujaalie!”
“Amina” Akajibu akitabasamu, wasiwasi ukiondoka pole pole. Dimples zake zikabonyea na kukitonesha kidonda changu tena. Mshituko mdogo nilioutoa ambao nilijitahidi kuuficha asiuone, ukawa umeurudisha wasiwasi wake kwangu tena. 
‘’Sikiliza Ibra!’’ akaniambia kama aliyechoshwa na kitu fulani. 
“Mimi ni mwanadamu mwenye hisia timilifu kama wewe! Kama una lolote ambalo labda unahisi litahitaji msaada wangu we niambie tu. Acha kuteseka kipumbavu na njaa na wakati chakula unachodhani ni cha watu kipo karibu yako! Huwezi jua may be Mungu amepanga kukuokoa kwa chakula hicho.!” 
Akazidi kunionyesha kwamba yuko tayari kwa lolote binti wa watu. Masikini laiti angelijua jinsi alivyozidi kuniweka mbali kwa kauli ile, asingeendelea.
“Da’ Shamsa, msaada niliouhitaji umekwisha nisaidia, tena umenisaidia kiukamilifu. Nikiwa na tatizo jingine nitakwambia tu. Naomba nawe usichoke kupokea miito yangu!”
‘’Usijali!’’ akaniwahi kwa pupa.
Ukapita ukimya mfupi tukiwa bado tumesimama hivyo hivyo tukiangaliana kwa zamu tena kwa wizi, mwishowe Shamsa akaniita tena.
‘’Ibra?” Sasa alinitulizia macho usoni moja kwa moja.
‘’Naam!’’ Nikaangalia pembeni, nikisugua vidole vyangu kama jinga vile
‘’Au… Au… Au unanipenda na unashindwa kuniambia?”
“Mmmm, mmmm!” Nikatikisa kichwa kushoto na kulia kukataa.
Shamsa akanipuuza na kuendelea “Kama umenipenda niambie tu. Niambie dia, niambie nijue! Hizi ni zama za ukweli na uwazi niambie usiogope!’’ 
Ooops! nikashusha pumzi ya faraja ndani kwa ndani, kwa namna ya mtu aliyeshusha mzigo mzito. Shamsa aliamua kuweka ile Msondo ngoma wanaita mambo hadharani. Ndiyo! Alikuwa amegusa mzizi, amegusa pale nilipotaka aguse. 
Pengine ingelikuwa wewe ilikuwa ni kiasi cha kuongeza maneno machache tu ndio ni kweli ninakupenda, lakini kutokana na uzuri wako, uwezo wako kiakili na kifedha nimekuwa nikihofia kukwambia kwa kuwa nilijua utanikataa na hivyo nitaaibika lakini ninakupenda sana na ninataka uwe mpenzi wangu please please naomba upokee ombi langu na kunipokea mimi mwenyewe, 
Lakini kwangu thubutu! Haikuwa hivyo nikajichekeshachekesha kiwazanga pale huku nikiona aibu kupindukia pengine kwa Shamsa kuligundua lile lililomo moyoni mwangu, nikaropoka. 
“Hapana Da’ Shamsa! Wewe ni dada yangu, kwamwe siwezi kukutamkia maneno kama hayo, nikiwa na mengine nitakwambia si hili!’’ Nilizidi kujiweka mbali na kujikaanga kwa mafuta yangu mwenyewe. 
Shamsa akaniangalia vizuri asiamini lile nililoongea, kutaka uhakika akaniuliza tena. ‘’Unasemaje?” 
Nikarudia nilichokisema awali mithili ya muigizaji aliyeiva vyema baada ya kumeza scripts kikamilifu. Nikaona Shamsa akiishiwa nguvu kwa staili ileile ya kukata tamaa, alipogundua nimemgundua katika hilo, haraka akajirekebisha na kusema. 
“Ok! Nafurahi kwa mawazo yako yaliyokwenda shule Ibra, laiti kama wanaume wote wangelikuwa kama wewe…! Ndio maana ninakupenda Ibra, wewe sio muhuni, hupendi mambo ya kipumbavu! 
Angelikuwa mwanaume mwingine, tayari angeisha nitongoza zamani. Lakini wewe akah! Keep it up. Keep it real Ibra. Endelea na moyo wako huo huo siku moja nitakuja kukupa tuzo. Bye!’’
Akaondoka bila kunipa nafasi ya kujibu tena, nadhani maneno yale aliyasema kwa uchungu kiasi cha machozi kumlenga na nilihisi aliondoka upesi akihofia kulia mbele yangu!
Kulia? Nikajiuliza kwa mshangao, kwa ajili yangu! Maana yake nini? Sikupata jibu! Niliendelea kumwangalia mpaka alipotoweka kwenye upeo wa macho yangu. Ndio kwanza nikapambazukiwa na ukweli wa kile nilicho kifanya. 
“Shit!” Nikaguta ghafla nikijipiga makonde ya nguvu kichwani. “Nimefanya nini sasa? Ama kweli mimi ndio mjinga wa wajinga No! Mwenyekiti wa wajinga. Mtoto tayari alishakaa katika laini namba moja, mie nimemrudisha line namba ziro! Tena ziro pointi ziro tano! Kamwe siistahili kusamehewa!” Nikajiambia nikizidi kujipiga makonde kichwani. 
‘’We vipi Ibra?’’ sauti niliyoifahamu sana ikanishtua kutoka nyuma yangu. Nikageuka haraka huku nikitahayari mithili ya mtu aliyefumaniwa, ni kweli rafiki yangu Yusuph alikuwa amenifumania, nikijipiga makonde kichwani kama chizi.
“Vipi nini?” Nikasaili kipumbavu nikizidi kuona hatia na kuongeza 
“Mbona mie mambo yangu yako safi? 
‘’Unahakika ni safi?’’ Akimu akanitulizia macho asiyapepese walau kiduchu. 
Nikazidi kuona soo. 
“Sikiliza Ibra, mimi ni rafiki yako wa damu, rafiki wa dhati rafiki wa kufa na kuzikana. Unaponificha jambo ni kama unajificha mwenyewe!”
‘’Hakuna Akimu! Hakuna kabisa. Nothing!”
‘’Kweli?’’
‘’Kweli tupu!
‘’Sasa mbona unajipigapiga makonde kichwani huku ukikita miguu chini utafikiri umepoteza kitu fulani kama sio kufeli mitihani!”
Eh! Hii kali! Nikawaza. Kumbe nilikuwa nikikitakita na miguu chini? Sekunde kadhaa zikapita huku Akimu akiniangalia na mimi nikiangalia chini kwa tahayari wakati huo kichwa changu kikizunguka kutafuta jambo la kumuongopea Akimu, sikulipata.
“Ukingali unajaribu kunificha Ibra! Any way haya ni maisha yako. Wewe ni mwamuzi wa mwisho kwayo. Ukiona ninastahili kuambiwa utaniambia, Ukiona sistahili usiniambie na sitolalamika kwaheri!”.
Akimu akamaliza na kuondoka kwa haraka kama alivyoondoka Shamsa. Nahisi nae aliongea kwa uchungu kwa kuwa tangu nianze masomo yeye ndio amekuwa rafiki na mwandani wangu mkuu. 
Sasa nitawakorofisha watu wangapi jamani? Kwa kule tu kukataa kwangu kusema ukweli! Kwa Shamsa naweza kustahimili kuishi bila ya kuwa na mahusiano nae mazuri. Lakini Akimu?! Itanichukua muda gani kutengeneza urafiki mzuri na bora kama yeye? 
Liwalo na liwe! Nikaanza kumkimbilia huku nikimwita, alikuwa amefika mbali kidogo, aliposikia akasimama na kugeuka .
‘’Unasemaje?” Akaniuliza nilipo mfikia.
“I am so sorry kaka!’’
‘’Samahani ya nini Ibra?! Si umesema hakuna kitu?”
‘’Nilikuwa wrong Akimu, nina tatizo! Tena tatizo kubwa!’’
‘’Tatizo la mapenzi sio? Linamuhusu Shamsa bila shaka!’’
Nikasikia moyo unafanya pah! Amejuaje? Nikatikisa kichwa chini na juu kuafiki,
’’Nilijua tu lipo tatizo, nikashangaa na kuchukia ulipotaka kunificha. Ulipotoka bwenini nilikuwa na shida na wewe, nikawa nimekufuatilia ili nikujuze shida yangu. Nikakukuta na Shamsa, na kutokea hapo nimeshuhudia kila lililojiri baina yenu ingawa sikuweza kusikia maneno mliyokuwa mkizungumza!’’
Unaona? Siku nyingine mtu unaweza kufungwa hivi hivi. Kumbe amenichora A to Z halafu mie nakomaa tu hakuna kitu, hakuna kitu! 
“Haya niambie ni tatizo gani? 
Nikabakia nikiumauma meno kwa muda nisijue nianzie wapi. Maana haya matatizo mengine wewe unaona tatizo, hali mwenzako haoni kama ni tatizo. Nikaamua kumweleza ukweli.
‘’Tatizo ni Shamsa Akimu, Nampenda sana, tena sana !’’
“Amekukataa? kwa kadiri nilivyoona na ninavyohisi kama sio kufahamu Shamsa nae anakupenda kupita kiasi, kwani bado haujamwambia kama unampenda?”
‘’Bado!’’
‘’Sasa tatizo liko wapi si ungemwita ukamwambia?! We mwambie tu Shamsa zungu yule hana tatizo!’’ 
“Tatizo lipo hapo kwenye kumwambia!”
“Unaogopa?”
‘’Naweza kusema hivyo, maana naweza kujipanga kwa sasa namwambia nikikutana nae tu nageuka zezeta kama sio bwege. Kujiamini kote kunatoweka na maneno yanakimbia kabisa!’’
Akimu akatabasamu.
‘’Wakati mwingine unapaswa kujiamini Ibra!’’
“Tatizo ni kwamba…” Nikamkumbusha kwa karaha, ’’Sio kwamba sijiamini, najiamini sana lakini ninapofika mbele yake tu ndipo hali hii inapo jitokeza! Unaweza kudhani Shamsa anadawa vile!’’
“Huko unakoenda mbali Shamsa hana dawa. Tatizo liko kwako tu tatizo ni kwamba hujiamini! Hilo tu. Lakini sio lazima umtongoze kwa kuongea nae, ziko njia nyingi za kufikisha ujumbe wako, 
Nikazibuka masikio. “Kama zipi?”
“Unaweza kumuandikia barua, ukamnunulia kadi za mapenzi, ukamtumia mauwaridi mazuri yenye ujumbe mzuri na hata kumwandikia sms za mapenzi na ujumbe ukafika, akaelewa na mkawa wapenzi. Shamsa hana ubavu wa kukukataa wewe Yule, sure am telling you!!
‘’Kumbe?!”
“Eeh!’’ Akakubali kwa msisitizo. Moyo wangu ukazizima kwa furaha nikajua naweza kutumia moja wapo kati ya njia hizo, mambo yakajipa na nikaweza kummiliki Shamsa Nuhu moja kwa moja. Image result for booty ebony
‘’Ila’’ Akimu akanizindua tena, “Itakubidi usubiri muhula huu wa mitihani uishe ili usichanganye mapenzi na masomo. Ukianza wewe kuvichanganya vyenyewe vitamalizia, na hupata zaidi ya hasara!’’
‘’Nitasubiri!” Nikamwambia
“Good!’’ Akashangilia baadae akaniambia lile alilokuwa akinitafutia, nami nikampa ushauri alioutaka. Mpaka tunaagana tabasamu lilikuwa bado limeupamba uso wake. itaendelea, usikose sehemu ya 3

Sunday, October 16, 2016

CHOMBEZO: ILAMBE HUMOHUMO sehemu ya -1

Image result for booty ebony
NILAMBE HUMO HUMO-1
Nilambe Humo Humo - 1

MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SIMU: 0755 697335

SEHEMU YA KWANZA

Kidokezo
…ulikuwa mduara wa Segere kwa lugha isiyo rasmi. Au ‘mnanda’ kama ilivyozoeleka. Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho walikuwa wakizunguka kwa pozi huku wakizungusha viuno vyao taratibu kwa ustadi mkubwa. 
Mirindimo ya ngoma sambamba na kiuno cha mwanamama mmoja kilichokuwa kikizunguka vitamu
vikayafanya macho yangu yamuandame! Yakamwandama kila alipokwenda. 
Halafu ngoma ikazimwa.
Yule mwanamama ambae wakati huo alikuwa ameshagundua kuwa nilikuwa nikimtazama akanitupia jicho na kuachia tabasamu. Ngoma ikapigwa upya na kurindima kwa robo saa hivi. Ilipozimwa tena na moto ulio kuwa ukitoa mwanga pekee hapo uwanjani nao ukazimwa! 
Kabla mshangao wangu haujaisha, nikajikuta ninashikwa mkono na kuvutwa kuelekea migombani kwenye kiza. Nikaweka mgomo kiasi, lakini nilipogundua kuwa kwamba jimama lililokuwa likizungusha kiuno vitamu ndilo lililokuwa likinivuta, nikatabasamu na kulifuata mithili ya mwanakondoo.
Kisha macho yangu yakazoea giza.
Huko Migombani nikashangaa kukuta seti mbilimbili za watu wakiwa wameng’ang’aniana huku wakitoa milio ya ajabu ajabu! Nilipowatazama vizuri, nikataharuki! Walikuwa wakifanya mapenzi!.
Nikatolewa ndani ya taharuki na jimama lililokuwa likinivuta, ambalo lilikuwa tayari likinishinikiza nasi tufanye mapenzi! Loh! My God ‘Gobbah…!’ 
Tembeeni muone. 

* * * 
Naweza kusema nilikuwa na bahati mbaya maishani, ndio mwenyewe nilijiona kuwa na sura ya wastani isiyo mbaya sana wala nzuri sana. 
Sura ambayo unaweza kumtongoza msichana huyu akakukatalia na yule akakukubalia! Lakini haikuwa kwangu. Kila niliyemtongoza alinikatalia, Kila niliyemtongoza! 
Hali hii haikuanza leo wala jana, ilianza kitambo toka ningali kinda lisilojua adha wala starehe ya tendo hilo la ndoa. Wakati huo akili za utoto zikinifanya niamini kwamba sikuwa mtaalamu wa kupangilia vyema mashairi yangu wakati nilipotaka kufikisha ujumbe wangu kwa mlengwa.
Nilipoingia primary wewe iite shule ya msingi na tatizo hilo kujirudia tena, sikutilia maanani sana. Nilikuja kuadhirika mwishoni mwa kidato cha pili na mwanzoni mwa kidato cha tatu. 
Nadhani kuathirika kwangu kisaikolojia kulitokana na ukweli kwamba kipindi hicho ndicho kilikuwa kipindi kipevu kwangu, kipindi cha masham sham na matamanio ya hamu. Kipindi cha mifadhaiko na majaribio, kipindi cha kupevuka.
Naam kilikuwa kipindi cha balehe. Kipindi cha kutoka utotoni na kuingia katika utu uzima. Ndugu yangu kipindi hiki kisikie hivyo hivyo, kama mwenzetu ulifanikiwa kukipita salama, hongera yako.
Lakini wale wenzangu na mimi tuliopelekwa na kupelekeshwa na kipindi hicho ambacho kila anayebahatika kupewa uhai na manani lazima akipitie, wanazielewa fika tamu na chungu za kipindi hiki hatari.

Wakati huo mheshimiwa sana kule ikulu alikuwa akinisumbua vilivyo nyakati za usiku muda mfupi kabla ya kulala, kila wakati akitaka kukagua gwaride la heshima. 
Hata hivyo bahati ilikuwa upande wangu mara nyingi usingizi uliponichukua ndoto nyevu ziliniokoa!
Ingawa shida za usiku hazikuwa za kupatiliza, adha nilizokuwa nikizipata mchana katika maeneo mbali mbali kila nilipokuwa nikikutana na mwanamke aliyeumbika vizuri, aliyevaa nguo za kubana sana, aliyevaa kimini na kitopu na hata wale waliovaa robo tatu uchi; hazikuwa na mfano.
Pengine ni hili lililoniingiza katika mkumbo waliopitia vijana wengi. Mkumbo wa kujichua! Potelea mbali kama unalegeza mishipa na kuathiri nguvu za kiume baadae! 
Ndiyo, niliamua kufanya mapenzi na mikono yangu kwa msaada wa sabuni, mafuta au chochote nilichokiona kinafaa au kunirahisishia kazi. Hii ikaendelea kuwa mkombozi pekee kwangu katika masuala ya kupoza makali ya ukware! 
Kumbe ningelifanyaje? hasa ukizingatia ukweli kwamba nilikuwa mwanafunzi nisiye na uwezo wowote kifedha, muoga wa kuwakabili viumbe hawa uzao wa Eva? Hakika hilo lilikuwa suluhisho kwangu.
Sikushauri uwe kama mimi, lakini mwenzako suluhisho hilo lilinifanya nihitimu elimu ya sekondari vizuri salama usalimini. 
Sikupata alama nzuri ambazo zingeniwezesha kuendelea na masomo ya juu ngazi ya A – level, kidato cha tano na sita. Na hili nilitarajia kabisa. Unadhani? Ningewezaje kupata alama nzuri hali nikiona mguu uliojaziajazia chini ya sketi basi hata kama nilikuwa ninasoma na wenzangu ni lazima nitafute mahali nijichue kwanza ndipo mambo yaende sawa?
Wazazi wangu wakaamua kunipeleka Veta kuchukua mafunzo ya ufundi umeme!

Kazi ambayo awali niliona inawastahili wanaume pekee, lakini nilipofika huko matokeo yakawa kinyume! Wanawake na labda niwaite wasichana walikuwa wamefurika isivyo kawaida katika darasa hilo. 
Pongezi kwa wanaharakati wanaopigania usawa wa kijinsia, harakati zao zinazaa matunda ati! Kwa mujibu wa waalimu wa hapo, kipindi cha nyuma ilikuwa aghalabu kukuta wanawake wengi wakijitokeza katika fani kama hizi zilizoonekana kama zina harufu ya uume uume!
Wengi ungewakuta ama katika mafunzo ya ufundi wa ususi, urembaji mapambo, mabatiki, ushonaji nguo, upishi na aina zote zenye mwelekeo huo lakini sasa hali ni tofauti, tena tofauti sana. 
Ni huko nilikokutana na rafiki yangu Akimu Yusuph, huyu alitokea kuwa rafiki wa kweli na mfariji mkuu wa maradhi yangu ambayo sina shaka kwamba sasa unayafahamu fika. 
Halafu ilifika siku moja, siku isiyo na jina!
Siku ambayo hatukuwa na masomo hapo chuoni. Nadhani itapendeza zaidi nikiita siku ya mapumziko. Mchana wa siku hiyo ulinikuta katika grosari moja jirani na chuo chetu pale chang’ombe nikipata kinywaji laini cha baridi. Mimi sio mtumiaji wa vikali na ninaomba Mungu anisaidie nisijaribu kuvigusa, usiulize sababu tafadhali.
Mchana huo ukiendelea kuyoyoma taratibu sambamba na kinywaji changu, mkononi nilikuwa na gazeti la Ijumaa wikienda nikiendelea kupata elimu ya kutakata ya namna ya kuyafikia mafanikio toka kwa Brother Erick Shigongo. 
“Hai Ibra?” Sauti nyembamba na laini ikaniharibia pozi.
Nikageuka taratibu kabla ya kujibu. Ni utaratibu nilio jiwekea toka enzi na enzi ili kuepuka kujibu salamu isiyonihusu na hivyo kumkwaza msalimiaji. Ndiyo! Kuna akina Ibra wangapi jijini?
Macho yangu yakakumbana na tabasamu zuri lililopachikwa kiufundi katika sura murua ya binti huyu mantashau. Hakuwa mgeni kwangu. Hili lilidhihirisha kwamba salamu ile ilikuwa yangu. Nami nikachanua tabasamu bomba kujibu tabasamu lake pamwe na salaam pia. 
“Hai Shamsa! Mambo?” 
“Kama mgambo kasoro kirungu!” 
“Hivi bado hamjamuelewa Karl P tu? Kwanini hukujibu kama mgambo kasoro bunduki na pingu?” 
Tukacheka.
Shamsa Nuhu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wenzangu tuliokuwa tukichukua mafunzo ya umeme pale VETA. Katika muziki Shamsa alikuwa akimpenda sana msanii Karl P, ingawa Karl P mwenyewe hayuko tena kwenye chati siku hizi .
Shamsa pia ni mmoja wa wasichana wachache walio kuwa wakiwapelekesha puta wanaume ndani na nje ya darasa letu. 
Alikuwa na akili za kutosha, hilo lazima nilikiri. Masomoni alikula sahani moja na wale unaoweza kuwaita majiniazi. Kifedha pia alikuwa njema kiasi kile ambacho usingeweza kumrubuni akubaliane na wewe kwa kwa kumringishia vijisenti! Kama hujui vijisenti, usiniulize mimi; muulize Chenge!
Kwa uzuri sijui wengine, lakini kwangu alikuwa na uzuri ulio shinda malaika! Alikuwa na sura nzuri, tabasamu zuri, ‘dimples’ nzuri, shingo ya miraba miraba, umbo zuri, mzigo wa uhakika nyuma yake, usafiri mzuri na hata mwendo wake ulikuwa mzuri. wachilia mbali sauti, roho na vitendo vyake. Alikuwa mzuri hasa, mzuri fika. 
Alikuwa mmoja kati ya wengi waliowahi kuumong’onyoa moyo wangu! Unadhani? Sio yeye tu, wako wengi waliowahi kupata hifadhi moyoni mwangu, lakini mimi nilipotaka kuingia katika mioyo yao wakagoma kunipa hifadhi!
Nilihofia kumueleza nilivyojisikia juu yake kutokana na ile hofu ya kawaida, hofu ya kukataliwa kwamba kama watu wanaoonekana; wenye akili zao darasani, fedha zao Benki na heshima zao katika jamii wamejaribu wameshindwa mimi mtoto wa msaka nyoka kama sio msaka tonge nitaweza kweli? 
Niliendelea kuumia kwa muda mrefu mpaka siku fulani nilipopata ujasiri wa aina yake na kumkabili. Hii ilikuwa ni baada ya kujishauri sana na kuamua kwamba mwanaume anakufa siku moja.

Aidha ilikuwa ni baada ya kujiuliza ni mara ngapi nimetongoza na kufaulu, nikagundua ni mara 0.05! Nikakubali kuishi siku moja kama simba kuliko kuishi siku mia moja kama inzi! Kwamba hata akinikatalia atakuwa tayari anajua ninampenda! Itatosha . 
Nikamvaa!
Unadhani nilifanikiwa kuinua domo langu na kumwambia japo ninakupenda tu? Thubutu! Kila nilipojitahidi kusema sasa nimwambie, ulimi ulikuwa mzito na pale ulipokuwa mwepesi maneno yalifanya mgomo! 
Mgomo ulipojisahau yalitoka maneno mengine tofauti kabisa na ninakupenda! 
Mpaka muda wa maongezi niliomuomba tuongee unakwisha na yeye kuniaga sikuwa nimemwambia lolote la maana. Nilibaki nimeduwaa kwa muda wakati wakati akiyoyoma na kunipa nafasi ya kuyafaidi maungo yake kwa nyuma. 
Ghafla akageuka na kunitazama. 
Macho yetu yakagongana. 

***NILAMBE HUMO HUMO INAANZIA HAPA……Na itaendelea
 

Gallery

Popular Posts

About Us