KINGAZI BLOG: 05/05/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Thursday, May 05, 2016

IJUE HISTORIA YA MAISHA NA SOKA YA MBWANA SAMATTA



 Mbwana Ally Samata amezaliwaTarehe 7 mwenzi wa 1 mwaka 1992 katika mkoa wa Dar es salam. Katika maisha yake ya soka alianza kucheza mpira katika klabu ya African Lyon kwa muda wa miaka miwili kutoka 2008 hadi 2010 alipohamia katika klabu ya Simba na kucheza mwaka mmja tu.

 Mwaka 2011 alihamia katika klabu ya Congo ambayo ni TP Mazembe aliweza kufunga magoli 60 pia katika timu ya taifa ya Taifa stars amefunga magoli 9. Samatta anajulikana sana katika mji wa Lubumbashi kwa kuwa alifunga magoli sita katika mashindano ya ligi ya mabingwa Africa na kuiwezesha Mazembe kutwaa kombe hilo.

Samata amekuwa mfungaji bora katika ligi ya mabingwa Africa pia Tarehe 7 mwenzi wa 1 mwaka 2016 Samata ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa Africa kwa wachezaji wa ndani pia ni mtanzania wa kwanza kutwaa taji hilo la ligi ya mabingwa Africa pamoja na Thomas Ulimwengu.

Baada ya kuwasili Tanzania Samata alipokelewa vizuri sana na watanzania akiwemo waziri wa habari na micheza Nape Nnauye pia Mh Zitto Kabwa na kufanyiwa Sherehe za kumpongeza katika sehemu mbalimbali Dar es salam. Kikwete alimpongeza na kumpa jezi ya TP M azembe pia mh. John Pombe Magufuli alimpongeza pia

MTOTO WA KITANZANIA ASHIRIKI KATIKA FILAMU YA KIMAREKANI

Juu, katika clip mojawapo Evan akifanya mazoezi ya kucheza mpira wa kikapu. Nyuma ni director wa filamu George Nelson na wasaidizi wake.

Juu, Evan akiwa anaongea na bibi yake (Pauletta) na mtoto anayeigiza kama kaka yake Kevin aitwaye Tony.

Juu Evan(aliyechuchumaa) akipitia script mbele ya wenzake.

Evan na mwenzake mwishoni walipata bahati ya kuonana na mama yake Kevin ambaye stori ya filamu inamuigiza.
Tasnia ya filamu Tanzania inazidi kukua kwa kasi, si tu nyumbani hata nje ya nchi watanzania wanazidi kungara.

Safari hii mtoto wa watanzania wenzetu aitwaye Evan Byarushengo amabahatika kupata nafasi ya kushiriki katika filamu ya kimarekani iitwayo THE REAL MVP: The Wanda Durant Story.

Filamu hii inajaribu kuonyesha jinsi mama wa mchezaji nyota wa mpira wa kikapu Kevin Durant alivyohangaika kuwakuza watoto wake mpaka kufikia kuwa mastaa.

Evan anaigiza kama Kevin Durant akiwa mtoto wa miaka 7. Waigizaji wakuu wa filamu hii ni pamoja na Cassandra Freeman anayeigiza kama mama Evan; Pauletta Washington (mke wake Denzel Washington) ambaye anaigiza kama bibi yake Evan na wengine wengi.

 

Gallery

Popular Posts

About Us