KINGAZI BLOG: 05/04/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, May 04, 2016

JIONEE PICHA YA KABURI ATAKALOZIKWA PAPA WEMBA HIVI KARIBUNI

 
Zimepita siku zaidi ya kumi tangu mwanamuziki wa kitambo PAPA WEMBA kufariki dunia akiwa stejini nchini mjini Abidjan ivory coast.
 Alikokuwa amealikwa kutumbuza katika  tamasha na hatimaye umauti ukamkuta akiwa anatumbuiza.Baada ya kuwasili mjini kinshasa wiki iliyopita mwili wake ulihifadhiwa na kusubiri hatua za mazishi zifanywe.
Hebu jionee picha ya kaburi ambapo anatarajiwa kuzikwa nguli huyu wa muziki.HILI NDILO Kaburi atakalozikwa Papa Wemba


Zijue Tabia 7 za Wanawake wanao-Cheat(Kuchepuka)






Kama mke wako, demu wako au side chick wako ana tabia zifuatazo, amesha-cheat kwako au ipo siku ataku-cheat.

1) Ana boreka haraka – 

black-couple-kissing-e1329280934214
Wanawake wanaoboreka haraka nirahisi kutafuta mwanaume mwingine wa kum-entertain, muda sio mrefu huyo mwanaume atachoka kum-entatain rafiki asiye na faida na ndio hapo atakapo anza kudai faida zake na wanaishia kuwa friends with benefits.
2) Marafiki wengi wa kiume 
– Mwanamke mwenye marafiki wengi wa kiume ni rahisi ku-cheat kwasababu anapata muda mwingi wa kuongea na wanaume wengine, watamsifia anavyopendeza, kama wewe unamwambia amependeza mara moja kwa wiki basi wenzako watamwambia anapendeza kila wanapoonana. Wataabza kumtoa out na mwisho wake ataona hao wanaume wamanjali kuliko wewe na kulala nao.
3) Anapenda attention
black-couple-angry1-300x199
 Wanawake wanaopenda attention ni rahisi kudanganyika. Wanaume wengi hasa ambao hawataki kuwa committed kwenye mahusiano yoyote wanatoa sana attention kwa wanawake. Mwanamke anayependa sana attention hawezi ridhishwa na attention ya mwanaume mmoja.
4) Anapenda vitu “material things” 

  Wanawake wengi wanaopenda material things wanashindwa kupata kila kitu kutoka kwa waume zao au maboyfriend zao na kuishia kutafuta mwanaume mwingine ambaye ana uwezo wa kumnunulia vitu anavyotaka ili awatese wenzake kwenye instagram.
5) Ana marafiki ambao ni michepuko

  – Umeshasikia usemi kuwa ndege wanaofanana huruka pamoja, hata kama demu wako hana tabia ya ku-cheat, akiwa anakaa sana na marafiki ambao wana-cheat na yeye atashawishika kujaribu. Kama mke wako au demu wako ana kupigia story za marafiki zake wanao-cheat mwambie aachane nao haraka sana.
6) Anapenda kufanya ngono kuliko wewe 

 – kila mkimaliza kufanya tendo la ndoa mwenzako anakwambia anataka tena, na wewe humtimizii basi lazima tatafuta serengeti boy ambaye anamsikiliza na kumpa anachotaka.
stay-or-go-divorce
7) Anaujuzi kitandani kuliko wewe – 

Wewe kama umeshawahi kuingia kwenye dancing floor na kucheza na mtu ambaye anajua kucheza kuliko wewe, unasubiria tu wimbo ukiisha ukakae chini kabla hujaaibishwa, au kama wewe ndio unayejua kucheza vizuri utatafuta mtu mwingine anayejua kucheza kama wewe. Kwenye tendo la ndoa ni hivyo hivyo kama mwenzako ana ujuzi kuliko wewe, inabidi ufanye mazoezi ufikie kwenye ujuzi wake la sivo muda sio mrefu atasubiri wimbo ukiisha akakae chini au atafute mtu mwingine anayejua kucheza kama yeye.
Demu wako au mchepuko wako una tabia moja wapo kati ya nilizozitaja hapo juu? Usisite kuacha comments hapo chin

Serikali imeongea inachoweza kufanya sasa hivi kuhusu ishu ya Bunge kuonyeshwa LIVE.

Hii kauli nimeinasa kwenye siku ya uhuru wa vyombo vya habari ambapo Waziri wa habari, sanaa utamaduni na michezo Nape Nnauye alialikwa na kusimama mbele ya Wadau na Wanahabari na kuyaeleza yafuatayo.

Umri sahihi wa mwanamke kubeba mimba na kuwa na mtoto



MAISHA yalivyo sasa si sawa na yalivyokuwa miongo kadhaa iliyopita. Wakati huo wanawake waliingia kwenye ndoa katika umri mdogo (mara nyingi usiozidi miaka 25) na kuchukua jukumu la kuzaa na kulea kama ndilo la kwanza. Wasichana na wanawake walipenda jukumu la kuwa mama kwenye familia na walitimiza jukumu hilo kwa utayari. 
Katika miaka ya hivi karibuni, wanawake wengi wamejikita katika masomo, na kujiendeleza kwa muda mrefu. Huko, wanaelekeza nguvu zao nyingi katika kupata shahada zaidi ya mbili na kazi nzuri huku umri ukizidi kwenda.

Kuchelewa kwa wanawake kuolewa na kuwa na watoto pia kumechangiwa na makundi mengi yanayodai haki sawa kwa wote (feminist organisations), ambazo zinasisistiza kuwa mwanamke ana haki sawa na mwanaume na anaweza kufanya vile atakavyo kutimiza ndoto zake.
Wakati makundi haya yamewasaidia wanawake kujitambua na kusonga mbele, pia yamechangia katika kuongezeka kwa idadi ya wanawake wanaochelewa kuzaa na wanaotaka kulea watoto wenyewe bila msaada wa mwanaume.
Japo wanawake wengi, hasa katika nchi za magharibi, wameweza kuwa na watoto baadae katika maisha, wengine hadi miaka 40 na kuendelea, wataalamu bado wanashauri kuwa umri unaofaa kwa mwanamke kuzaa na kuwa na watoto wenye afya pamoja na kuwa na muda wa kutosha wa kulea watoto hao, ni kwanzia miaka 20 hadi 35. Zaidi ya hapo mtoto au mama anaweza kupata matatizo mbalimbali. 
Matatizo yanayoweza kutokea kutokana na kuchelewa kuzaa au kuzaliwa
Wanawake wenye kubeba mimba wakiwa na umri zaidi ya miaka 35 wana hatari kubwa ya kupoteza mtoto au mimba kutoka (miscarriage).
Mfumo wa uzazi unakuwa umeanza kuchoka hivyo kubeba mimba kwa kuchelewa, hasa kuanzia miaka 36 na kuendelea kunaweza kuuchosha zaidi na kusababisha matatizo siku za mbele hasa katika ukuaji wa mimba.
Matatizo na hatari katika ubebaji mimba yanaweza kuzidi katika kipindi hiki (miaka 36 na kuendelea) kuliko kwa mama mwenye umri wa miaka 20 hadi 35.
Kuchelewa kuzaa pia kunaweza kusababisha kuzaliwa mtoto mwenye magonjwa na matatizo kiafya. Afya ya mama pia inaweza ikawa hatarini (hasa kwa magonjwa kama presha ya kupanda).
Kunaweza kuwa na matatizo wakati wa kujifungua kama vile kuwa na uchungu kwa muda mrefu kabla ya kuzaa, kuhitaji upasuaji au kuwa na uzazi mfu.
Ni vyema wanawake wakafanya maamuzi sahihi mapema na kuwahi kuwa na familia (kuzaa) ili kuepusha hatari kwao na kwa watoto wakati wa mimba na baada ya watoto kuzaliwa.

Video ya SNURA_CHURA YAFUNGIWA KWA KOSA HILI

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo May 04 2016 imetoa kauli ya kuufungia wimbo wa Snura ‘chura’ kuchezwa kwenye MEDIA kuanzia leo mpaka Snura atakapoifanyia marekebisho video ya wimbo huo na kuitoa nyimbo hiyo kwenye mitandao ya kijamii yote.
Serikali imeeleza sababu ya kuufungia imetokana na maudhui ya utengenezaji wa video hiyo, pia serikali imesitisha maonyesho yote ya hadhara ya Snura mpaka atakapokamilisha taratibu za usajili wa kazi zake za sanaa katika baraza la sanaa la taif

Rais wa Burundi afariki Dunia leo

Rais wa zamani wa Burundi Kanali Jean-Baptiste
Bagaza amefariki akitibiwa nchini Ubelgiji.
Kanali Bagaza amekuwa akitibiwa kwa muda
katika hospitali ya Sainte Elisabeth mjini Brussels.
"Imethibitishwa, rais wa zamani Jean Baptiste
Bagaza amefariki dunia akiwa nchini Ubelgiji,2
ameandika mshauri wa rais wa Burundi Willy
Nyamitwe kwenye Twitter.
"Alikuwa seneta maisha.”
Kanali Bagaza aliingia madarakani Novemba 1976
kupitia mapinduzi ya kijeshi.
Aliondolewa madarakani kupitia mapinduzi
mengine yaliyoongozwa na binamu wake Meja
Pierre Buyoya Septemba 1987.

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo Mei 4 2016 kwenye,Habari za Udaku, Kitaifa,kimataifa na michezo.

20160504_074806
20160504_074113
20160504_074251
20160504_074259
20160504_074407
20160504_074414(0)
20160504_074700
20160504_074707
20160504_074428
20160504_074437
20160504_074446
20160504_074453
20160504_074502
20160504_074518
20160504_074547
20160504_074600
20160504_074621
20160504_074633
20160504_074721
20160504_074734
20160504_074746

20160504_074754

20160504_074821
20160504_074829
20160504_074932
20160504_074942
20160504_075030

 

Gallery

Popular Posts

About Us