KINGAZI BLOG: 08/27/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Saturday, August 27, 2016

MAAAAAJABU YA MWAKA!!!MUME AMFUMANIWA NA MKEWE AKIFANYA NGONO NA MBWA WAKE


Mwanamke mmoja amepigwa na butwaa baada ya kumpata mumewe akishiriki ngono na mbwa wao nyumbani Spring Valley, Nairobi
–Inasemekana mwanamke huyo alikuwa amezuru mashambani kupeleka watoto ambapo alirudi nyumbani Nairobi bila kutarajiwa
Mwanamke mmoja alielezea kisa cha kushtua baada ya kumpata mumewe akishiriki ngono na mbwa nyumbani, Spring Valley, Nairobi.
Mwanamke huyo aliondoka nyumbani Jumamosi Agosti 20, kuelekea mashambani Gatanga kupeleka watoto wao.
Walikuwa wamekubaliana na mumewe kuwa angekaa wikendi na wazazi mashambani, hasa baada ya kuacha amemtayarishia chakula mwanamume huyo.
Hata hivyo, alirudi nyumbani ghafla baada ya kukumbuka alikuwa ameacha dawa za mmoja wa watoto wao.
Lakini baada ya kufika nyumbani alipigwa na butwaa baada ya kuingia ndani ya chumba chao cha kulala na kumpata mumewe akishiriki ngono na mbwa wao!
Baada ya kupatikana, mwanamume huyo alivaa nguo haraka na kuondoka nyumbani mara moja, bila kusema chochote!

UKWELI KUHUSU MSANII BELLE9 KUJIUNGA NA WCB(SOMA HAPA)

Kumekuwa na tetesi nyingi kwenye mitandao ya kijamii zikimuhusisha msaani wa bongo fleva Belle 9 kusajiliwa kwenye lebo kubwa ya muziki wa bongo fleva Tanzania,WCB ianyomilikiwa na Diamond Platnumz.
Tetesi hizo ziliibuka baada ya kuonekana kwa kipande cha video zikumuonyesha Belle 9 akiimba pamoja na Diamond wimbo wa ‘kidogo’ kwa live band katika studio za lebo hiyo.Alipoulizwa kwa upande juu ya kujiunga na lebo hiyo ,Belle 9 alikuwa na haya ya kusema.
“Me ni msanii ambaye niko huru kukutana na wasanii wenzangu,na kama kuna mtu amefanya kitu kizuri ni vyema kumsapoti.Mimi binafsi nilikwenda tu kuitembelea ile studio,pia nilikwenda kuangalia bendi,maana mshikaji anajiandaa kufanya live band,Alichokifanya mshikaji ni kitu kizuri kwa maendeleo ya muziki wetu na mimi nilivutiwa nacho,lakini waandishi wanapoandika habari wanaangalia upande wao tu” alifunguka Belle anayetamba na kibao chake cha BMS (bunger,movie&selfie).

source: Tizneez

HEBU ONA PICHA ZOTE UKWELI KUHUSU MAPAMBANO YA POLISI NA MAJAMBAZI JANA HUKO VIKINDU


Eneo la Mtaa wa Vikindu Mashariki mkoani Pwani kwenye nyumba ya mtu mmoja aliyetajwa kwa jina la Mzee Manitu paligeuka uwanja wa mapambano baada ya polisi kuizingira nyumba hiyo na kupiga risasi nyingi hewani wakati wakimtaka jambazi anayetuhumiwa kufanya mauaji ya katika tukio la kuuawa askari polisi wanne waliokuwa wakibadilishana lindo kwenye Benki ya CRDB Tawi la Mbande wialayani Temeke jijini Dar. Katika tukio hilo Afisa wa Polisi mwenye cheo cha ASP Thomas Njuki wa Kikosi Maalum cha Kupambana na Ujambazi ameuawa.

Baada ya jambazi huyo kumuua askari, jeshi la polisi liliongeza nguvu eneo hilo na kupiga mabomu na risasi nyingi hewani zilisababisha taharuki katika eneo hilo na kusababisha kila mmoja aseme lake.

Mapaparazi wetu baada ya kufika eneo hilo walitaka kuzungumzia na maofisa wa polisi waliokuwa eneo hilo akiwemo, RPC wa Pwani, Bonaventura Mushongi, Gilles na Kamishna Mwandamizi wa Jeshi hilo, Liberatus Sabas lakini wote walisema hawawezi kuongea chochote mpaka wapate ruhusa kutoka ngazi za juu kwa kuwa tukio hilo si la Kimkoa bali ni la Kitaifa.

Licha ya viongozi hao kukataa kuzungumza, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Vikindu Mashariki, Mohammed Ismaili ambaye alikuwa bega kwa bega na askari hao alisema kwenye nyumba hiyo walikuwa wakiishi wanaume 7 ambapo walikutwa wanaume 3 na wanawake 3 ambapo mwanaume mmoja aliyetajwa kumuua Afisa huyo wa Polisi alitoroka pamoja na silaha yake.

Hakuna Jambazi yeyote aliyeuawa katika tukio hilo zaidi ya afisa huyo wa polisi.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Vikindu Mashariki, Mohammed Ismaili
Angalia picha
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS/ ISSA MNALLY /GPL.

Waziri Nape Atengua Uteuzi wa Mjumbe wa Kamati ya Maudhui ya TCRA



Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Agosti 27


Serikali yaagiza Mabasi Mapya 165 ya Mwendokasi

Serikali imeanza mchakato wa kuagiza mabasi mapya 165 ya mwendokasi yatakayotoa huduma za usafiri kwa wakazi Dar es Salaam kwenye maeneo yasiyo na huduma hiyo.

Tayari imeshatangaza zabuni ya kununua mabasi hayo na mwezi Desemba, mwaka huu itasaini mkataba na mzabuni.

Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi (Dart), Ronald Rwakatare amewaeleza wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa waliotembelea mradi huo kuwa wanatarajia mabasi hayo yataanza kazi Aprili mwakani.

“Mabasi haya yatahudumia maeneo ya Morocco, Tegeta, Masaki, Makumbusho na mengine yasiyofikiwa, wakati tukiendelea na ujenzi wa awamu ya pili ya mradi huo,” amesema.

Askari Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi vikindu

Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi kwenye nyumba iliyo eneo la Vikindu wilayani Mkuranga.

Taarifa ambazo zimepatikana kutoka kwa watu waliokuwa karibu na operesheni hiyo na ambazo hazijathibitishwa na mamlaka rasmi, zinasema kamishna wa Kitengo cha Kuzuia Ujambazi, ASP Thomas Njuki aliuawa kwa kupigwa risasi kichwani. 

Taarifa hizo zilisema kuwa jambazi mmoja aliuawa ingawa idadi ya waliokamatwa haikufahamika mara moja kutokana na mashuhuda kutoa takwimu tofauti. 

Kamanda wa Polisi wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema ataongea na waandishi wa habari leo saa 4:00 asubuhi kuzungumzia tukio hilo. 

Tukio hilo limetokea siku chache baada ya askari wanne wa Jeshi la Polisi kuuawa wakati wakibadilishana lindo kwenye tawi la benki ya CRDB lililoko Mbande jijini Dar es Salaam. 

Watu hao, waliofika wakiwa wamepanda pikipiki, walipora silaha na kutoweka nazo. Katika tukio la jana, askari wa Jeshi la Polisi walikuwa na nia ya kuwakamata watu waliowashuku kuwa ni majambazi. 

Kwa mujibu wa watu wanaoishi karibu na nyumba hiyo, mpambano kati ya polisi na majambazi hao ulianza saa 7:30 usiku baada ya polisi kuvamia nyumba walimopanga majambazi hayo. 

Tukio lilivyotokea 
Chanzo kimoja cha habari kimeeleza kuwa baada ya polisi kufuatilia nyendo za wakazi wa nyumba hiyo walianza upelelezi na kubaini kuwa huenda wanahusika na matukio kadhaa ya uhalifu, likiwamo la uvamizi wa kituo cha polisi cha Stakishari na lile la tawi la CRDB Mbande mkoani Pwani. 

Mpashaji huyo alisema kuwa jana saa saba usiku, polisi walifika kwenye nyumba hiyo iliyo Mtaa wa Vikindu Mashariki ambayo ina maduka upande wa mbele, ikipakana na nyumbani nyingine mbili pembeni na nyuma zikiwa umbali usiozidi hatua nne. 

Habari hizo zinasema askari hao kwanza walimtuma mwenyekiti wa serikali ya mtaa kwenda kuwasihi wafungue mlango na walipokataa ndipo walipoenda kugonga, wakiwaamrisha watu hao wafungue mlango. 

“Baada ya kuona hawatii amri ya kufungua mlango, polisi waliamua kuvunja vitasa kwa kutumia bastola, ndipo risasi zikaanza kurushwa,” alisema mpashaji habari huyo. 

 “Kwa kuwa mkuu alikuwa mbele, wahalifu walimpiga risasi kichwani na alikufa palepale.” 

Mtu huyo alisema kuwa baada ya Kamishna Njuki kufariki, askari wengine walirudi nyuma kujihami zaidi. 

Baada ya hapo polisi waliendelea kupiga risasi kuelekea maeneo mbalimbali ya nyumba hiyo na wahalifu hao kujibu mashambulizi. 

“Kila chumba ambacho polisi walikuwa wakijaribu kurusha risasi, zilijibiwa. Inaelekea kila chumba kilikuwa na mtu mwenye silaha,” alisema shuhuda mwingine wa tukio hilo. 

Habari kutoka kwa majirani zinasema hadi saa 2:45 asubuhi, milio ya risasi iliendelea kurindima katika eneo hilo. 

Baadaye polisi waliomba kuongezewa nguvu na Jeshi la Wananchi (JWTZ) ambao walifika na kuendeleza mapambano hayo. 

 Mtoto ataja alipojificha baba 
Wakati mapambano yakiendelea, sauti za watoto waliokuwa wakilia zilisikika na ndipo askari wa JWTZ waliamuru watu hao wawatoe nje. 

“Watoto walipotoka nje, polisi waliwauliza baba yupo wapi, mtoto mmoja akajibu yupo darini,” alisema

Baada ya polisi kusikia hivyo, walielekeza mashambulizi yao darini na kufanikiwa kumjeruhi mtu aliyejificha darini ambaye alishuka. 

Wakati polisi wakishinikiza atoke ndani ili kujisalimisha, mtu huyo alijipiga risasi mara baada ya kutoka na kufariki dunia.

Wakazi Vikindu wahaha!
Kutokana na tukio hilo, taharuki ilitanda kwa wakazi wa Vikindu na biashara zote zilifungwa eneo hilo huku wananchi wakiwa na chupa za maji kutokana na mabomu ya machozi yaliyokuwa yakipigwa kila mara. 

Wakazi wa eneo ambalo lipo karibu na maegesho ya magari ya Farid Seif, hawakuruhusiwa kutoka ndani na waliofanikiwa kutoka usiku hawakuingia hadi jana saa 7.00 mchana wakati hali ilipotulia. 

Kutokana na majibizano ya risasi, watu wanaofanya kazi jijini Dar es Salaam ambao wanaishi vijiji vya Melela, Vianzi, Pemba Mnazi na Mfuru hawakwenda kazini kutokana na barabara inayotoka Vikindu kufungwa hadi saa 7.00 mchana. 

Tukio hilo lilisababisha umati wa watu kukusanyika kushuhudia mapambano hayo, lakini hakuna raia aliyeruhusiwa kuvuka mita 150 kwenda eneo la tukio. 

Nyumba waliokuwa Wanaishi hao Majambazi



 

Gallery

Popular Posts

About Us