KINGAZI BLOG: 05/24/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, May 24, 2016

Polisi waendelea kumhoji Maalim Seif

Jeshi la Polisi Zanzibar litamhoji Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad Ijumaa ya wiki hii kuhusu masuala mbalimbali ambayo hata hivyo, hayakuwekwa wazi.
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdani Makame alisema jana:“Natambua kuwa wasaidizi wangu watazungumza naye Ijumaa. Wao ndiyo wanajua watamhoji nini.”
Alipoulizwa kuhusu mahojiano hayo, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, Salum Msangi naye hakuweka wazi badala yake alisema kuna masuala mengi ambayo ofisi yake inahitaji kuyafahamu kutoka kwa Maalim Seif.
Hii ni mara ya kwanza kwa Maalim Seif kuhojiwa na polisi tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu ambao kwa Zanzibar ulirejewa Machi 20, baada ya ule wa Oktoba 25 mwaka jana kufutwa.
Maalim Seif ambaye kabla ya uchaguzi huo alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, alipinga kurudiwa kwa uchaguzi huo msimamo ambao pia ulichukuliwa na chama chake.
Kiongozi huyo amekuwa akitoa matamko kadhaa ya kuwashawishi wananchi kupinga utawala wa Serikali iliyopo madarakani.
Akiwahutubia wafuasi wake huko Pemba hivi karibuni, Maalim Seif alisema Serikali ya CCM imeanza kutikisika kutokana na vikwazo vinavyoendelea kuwekwa na wahisani pamoja na hatua ya chama chake CUF kutowatambua viongozi wake pamoja na Serikali. 
“CCM wajue wamekalia kuti kavu, siku yoyote wataanguka... tufanye kazi mpaka haki yetu tuhakikishe imerudi na wenzetu hawana safari ya kudumu,” alisema.
Aliwataka wanachama wake kuonyesha kwa vitendo kutoitambua Serikali ikiwamo kukataa kulipishwa kodi za ovyovyo pamoja na kujitenga na viongozi wa Serikali katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Mfano tunaweza kuamua siku fulani kuanzia saa sita, tunasimamisha vyombo vyote vya usafiri na siku nyingine tunaamua kupiga honi Zanzibar nzima kuonyesha hatuitaki Serikali ya CCM,” alisema huku akishangiliwa na umati uliofurika katika ofisi za chama hicho.
Mapema jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa CUF, Shaweji Mketo alisema kuwa amesikia juu ya wito huo lakini hakuwa amepata taarifa rasmi kutoka kwa mkuu wake.
“Nimesikia kama mlivyosikia ninyi,” alisema na kuongeza: “Nimeelezwa pia hata leo Kamishna wa Polisi Zanzibar alikuwa na mahojiano naye.”
Kuhusu hilo Kamishna Makame alisema: “Sijaonana wala kuzungumza naye leo. Hiyo si kweli.”
Juzi, wakati akizindua ripoti ya Uvunjifu wa Haki za Binadamu uliofanyika visiwani humo kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema wanazo taarifa za Serikali kutaka kuwakamata viongozi waandamizi wa chama hicho na kuwashikilia.
Alisema wamebaini mpango wa kukamatwa kwao na kuwekwa kwenye Mahakama za bara ili kuwanyamazisha Wazanzibari

Waliokosa Ubunge Walipuliwa Bungeni......Mbunge Adai NHC Imepoteza Mwelekeo



Mbunge wa Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani (CCM), maarufu kwa jina la ‘Maji Marefu’ amewalipua wabunge waliokosa ubunge katika kipindi hiki na vilivyopita kwa kuhodhi nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mjini Dodoma na kupangisha watu wengine kinyume cha utaratibu wa shirika hilo.

Alisema hali hiyo imefanya wabunge wapya, ambao ni asilimia 70 ya wabunge wote kwa sasa, kukaa nyumba za kulala wageni wakati zipo nyumba hizo kwa wabunge kulingana na mkataba na NHC.

Mbunge alisema wapo watu wamepangishwa na wabunge hao wa zamani, ambao wamegeuza nyumba hizo kama kitega uchumi kinyume na taratibu. 

Ngonyani alisema hayo bungeni mjini hapa jana wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha 2016/17.

Alimuomba Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, kufuatilia suala hilo na shirika kwa ujumla, aondoe wapangaji hao waliowapangishia wengine kinyume cha utaratibu na kuwapatia nyumba wabunge wapya ambao hawana nyumba za kuishi.

Alisema wabunge hao waliokosa nafasi ya kurudi jimboni miaka tofauti, mkataba wao wa kupangishwa nyumba hizo umekwisha, kwani ukishakosa ubunge hauna dhamana tena mpaka utakaporudi.

“ Kuna wapangaji wengi ambao ni wabunge waliokosa nafasi hiyo ambao wamepangishwa na shirika na badala yake hadi leo wamezishikilia nyumba hizo hawataki kuziachia, ”alisema Ngonyani.

Alieleza kuwa baada ya kukosa nafasi za ubunge na kushindwa kurudi bungeni, wabunge hao walipaswa kurejesha nyumba hizo kwa shirika, ambalo ndilo lenye mamlaka ya kupangisha na si wao kupangisha wapangaji wengine kupitia mikataba yao.

Hata hivyo, taarifa kutoka NHC, Dar es Salaam jana kuhusu nyumba hizo zilifafanua kuwa hazikutengwa kwa ajili ya wabunge pekee, bali hata watu wa kawaida na kila mtu anaingia mkataba binafsi na shirika.

Pia zilieleza kuwa, nyumba hizo zilikodishwa awali kutokana na mahitaji ya wabunge uliokuwapo na wapo walionunua, hivyo wana dhamana nazo. 

Aidha ilieleza kuwa ikiwa kuna mpangaji aliyepangisha mtu mwingine bila kujali alikuwa mbunge au la, anakwenda kinyume cha utaratibu, watafuatilia suala hilo.

Katika hatua nyingine, Ngonyani alisema bungeni kuwa NHC imebadilisha dhana na kutoka kwenye kujenga nyumba za bei nafuu, kusaidia wananchi wenye uwezo mdogo sasa inafanya biashara, kwani inajiendesha kibiashara na si kwa lengo la kuundwa kwake.

Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulya (CUF) alisema nyumba za shirika hilo zimejengwa kwa ajili ya mabepari kwa sababu wananchi wa kawaida kutozimudu kutokana na bei zake za kati ya Sh milioni 40 hadi milioni 60.

Mbunge wa Mpanda Vijijini, Moshi Kakoso (CCM) alitaka shirika lijenge nyumba kulingana na uwezo wa watu wa eneo husika kutokana na kuwa wanajenga nyumba za gharama kubwa. 

Alisema ujenzi huo uzingatie katika miji inayokua kuiweka katika mandhari nzuri na wakazi wa maeneo husika kumudu kupanga na kununua.

Picha za Mbunge Zitto Kabwe Akimvisha Mwanamke Pete ya Uchumba Hizi Hapa

 Mwanasiasa Zitto Kabwe Ameamua kuacha ukapela, kwenye picha akionekana kumvisha pete ya ya uchumba mchumba wake anayetarajia kumuoa.


Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mshauri wa Rais Katika Masuala ya Uchumi

 Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mshauri wa Rais Katika Masuala ya Uchumi



Wafugaji jamii ya Wadatoga wilayani babati wajificha vichakani kupinga kuhamishwa .

vitatu wilayani Babati mkoani Manyara wakiwa na silaha za jadi mishale na mikuki wanalazimika kulala nje ya maboma yao wakipinga uamuzi wa serikali wa kutaka kubomoa maboma 11 kati ya 25 yaliyopo katika eneo la Maramboi linalopakana na mwekezaji raia wa Ufaransa kwa madai kwamba kumekuwepo na ongezeko la wafugaji ambao si wakazi wa kijiji hicho na wamekuwa wakiingiza mifugo yao katika eneo la mwekezaji huyo.

Kauli hiyo ya kupinga agizo la kutakiwa kuondoka ama kubomoa maboma yao wameitoa baada ya watendaji wa kijiji,kata na tarafa wakiwa na timu maalum iliyoandaliwa chini ya usimamizi wa polisi kufika katika eneo hilo la kijiji ili kuwashawishi kuondoka kabla ya kubomoa kwa nguvu na kwenda eneo walilopangiwa huku wakidai hawawezi kuondoka katika eneo hilo kwa kuwa agizo hilo linapingana na amri ya Mahakama ya Rufaa ya 2013 iliyowataka kuendelea kubaki hapo aidha pia wakipinga kuwepo kwa ongezeko la wageni.

Nae Katibu wa chama cha wafugaji nchini kata ya Nkaiti Bw Juma Kwanjay amesema chama hicho kinapingana na operesheni hiyo yenye muonekano wa  ushawishi ngazi ya kata kwa mujibu wa barua kwenda kwa mkuu wa wilaya hiyo badala ya kijiji,huku akidai kama lengo ni kubomoa maboma 11 na kuacha maboma 17 yaliyoamriwa na mahakama yatabaki maboma 14 kinyume na amri ya mahakama na kuchochea mgogoro huo uliokuwa umetulia.

Hata hivyo kiongozi wa oparesheni hiyo na Afisa Tarafa ya Mbugwe bw faustine Sedoyeka amesema operesheni hiyo ni utekelezaji wa agizo la mkuu wa wilaya la kuwasimamia kubomoa maboma yao na kuwapeleka eneo maalum lililotengwa lakini wamelazimika kusitisha operesheni hiyo kutokana na mazingira hayo kutokuwa rafiki kwao hasa kutokana na wafugaji hao kujificha vichakani kama mtego dhidi yao.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusufu amejibu upya swali lililomponza bosi wake wa zamani, Charles Kitwanga.


Uamuzi wa kurudia swali hilo ulitolewa juzi na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisema swali hilo lilijibiwa katika hali ya ulevi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na wabunge wakaomba mwongozo kuhusu majibu yaliyotolewa.

Kitwanga aliondolewa katika nafasi yake na Rais John Magufuli baada ya kujibu ya swali hilo akiwa amelewa.

Leo, Masauni amejibu swali hilo namba 211 la Mbunge wa Viti Maalumu Devota Minja (Chadema) na kuonyesha utofauti mkubwa kati ya majibu yake na yale yaliyotolewa mwishoni mwa wiki na aliyekuwa Waziri wake.

Swali hilo ambalo awali lilikuwa namba 205, liliulizwa na Devota Minja akitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kuboresha makazi ya polisi na askari magereza wanaoishi katika nyumba chakavu zisizokuwa na hadhi ukilinganisha na kazi zao kwa jamii.

Nyakati zote hizo, swali hilo limeulizwa na wabunge tofauti wa Chadema kutokana na Minja kutokuwapo, mara ya kwanza likiulizwa na Suzan Kiwanga (Mlimba) na leo Joseph Selasini wa Jimbo la Rombo.

Tofauti ya majibu ya Kitwanga, Masauni ametoa takwimu katika ujenzi wa nyumba 9,500 za Magereza nchi nzima, lakini kwa upande wa nyumba za Polisi majibu yalikuwa yaleyale.



Serikali imefanikiwa kukamata takribani kilo 139.69 za dawa za kulevya ikiwemo kilo 53.49 za Heroin, Cocaine kilo 86.2 kuanzia mwaka 2015 mpaka Aprili mwaka huu.


Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Elimu, Habari na Takwimu wa tume hiyo, Amani Msami, pia tume hiyo imekamata tani 97 za bangi na mirungi.

Alisema mbali na kukamata kilo hizo, takwimu zinaonesha kuwa watumiaji wa Heroin nchini wanakadiriwa kuwa kati ya 200,000 hadi 425,000 ambapo kati ya hao 30,000 hutumia dawa hizo kwa njia ya kujidunga sindano.

“Serikali imefanikiwa kukamata takribani kilo 53.49 Heroin, Cocaine kilo 86.2 kuanzia mwaka 2015 mpaka Aprili mwaka huu” alisema Msami na kuongeza kuwa:
“Watumiaji wa Heroin nchini wanakadiriwa kuwa kati ya 200,000 hadi 425,000 ambapo kati ya hao 30,000 hutumia dawa hiyo kwa njia ya kujidunga”.
Msami alifafanua kuwa mbali na kukamata dawa hizo, tume hiyo ilikamata tani 81.3 za bangi na Mirungi tani 15.7.

Aliongeza kuwa mbali na hayo idadi ya watuhumiwa waliyokamatwa wakijihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya zikiwemo Bangi,Mirungi, Heroin na Cocaine walikuwa 14,503.

Hata hivyo, alisema takwimu hizo zinaonyesha jitihada za serikali katika kukabiliana na biashara ya dawa za kulevya nchini na si ukubwa wa usafirishaji wa Heroin na Cocaine nchini.

“Moja ya jitihada za Serikali katika kukabiliana na tatizo la dawa za kulevya ni kutungwa kwa Sheria ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Na.5 ya mwaka 2015.” Alisema Msami.

Alifafanua kuwa sheria hiyo imeweka adhabu kali kwa makosa ya kujihusisha na matumizi na biashara ya dawa ya kulevya ikiwemo kifungo cha maisha kwa yeyote atakayesafirisha dawa za kulevya.

CHADEMA:JPM MFUATE LOWASSA AKUSHAURI TATIZO LA SUKARI


Monduli. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemtaka Rais John Magufuli kuweka siasa kando na kuomba ushauri kwa waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ili kutatua tatizo la kuadimika kwa sukari.
Kauli hiyo ilitolewa na naibu katibu mkuu wa Chadema, Salim Mwalimu juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Moto wilayani hapa Mkoa wa Arusha ambako Lowassa alizungumza na wananchi
kuwashukuru kwa kumpigia kura na akatangaza mpango wa kuzunguka nchi nzima kwa lengo hilo.
Tangu Rais atangaze kudhibiti uagizaji sukari kutoka nje na baadaye Bodi ya Sukari kutangaza bei elekezi, bidhaa hiyo muhimu imepanda bei kutoka Sh1,800 hadi kufikia Sh5,000 kwa kilo na kwa sasa imeadimika madukani, wakati Serikali ikisaka wafanyabiashara inaowatuhumu kuwa wameificha kwenye maghala kwa lengo la kuihujumu.
Akizungumza kabla ya kumruhusu Lowassa kuongea na wananchi hao, Mwalimu alisema inaonekana tatizo la sukari linaelekea kuishinda Serikali na hivyo inahitaji msaada wa ushauri.

“Tatizo la sukari kalianzisha yeye mwenyewe Magufuli na sasa anashindwa kulitatua,” alisema Mwalimu na kuongeza:

“Mtu pekee atakayemsaidia ni Lowassa. Huyu alijipanga na alijiandaa kuongoza nchi.”

Mwalimu alisema Lowassa amevumilia mengi kwa kuwa amenyanyaswa, ameonewa na kusimangwa lakini hakujibu.

“Amepitia kipimo cha mwisho cha utu, ni cha mwisho. Walimuonea mchana kweupe akavumilia. Walimsimanga mchana kweupe mpaka watoto wadogo walikuwa wakimuona Lowassa kama vile saizi yao, akavumilia,” alisema Mwalimu.

“Ninajua vijana waliumia, mzee. Lakini leo warudi nyuma wafikirie maisha yao. Ni nani angetoka nyumbani kwa kauli moja ya Lowassa, kumshika mtoto wake mkono kumpeleka shule kama Lowassa angeangalia ushetani na kumuacha Mungu,” alisema akirejea kauli ya Lowassa kuwa alikuwa akipigiwa simu na watu kumtaka atoe kauli baada ya matokeo ya Uchaguzi Mkuu mwaka jana kutangazwa, lakini akaawaambia watulie.

Lowassa, ambaye aligombea urais kwa tiketi ya Chadema baada ya kuenguliwa CCM, alishika nafasi ya pili kwenye mbio hizo akipata kura milioni 6.07 idadi ambayo ni rekodi kwa mgombea wa upinzani tangu siasa za ushindani zirejeshwe mwaka 1992. Magufuli aliibuka mshindi kwa kupata kura milioni 8.8.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Lowassa aliwataka wananchi kuendelea kutulia, akisema mwaka 2020 hauko mbali na Chadema inaendelea kujipanga upya ili kuhakikisha inashika dola na kuondoa kero zao.

Katika mkutano huo uliohudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa Chadema kutoka makao makuu, mkoa pamoja na makada waliojiunga wakitokea CCM wa wilaya ya Monduli, Lowassa alisema wafuasi wa ukawa wajiandae kwa mikutano hiyo.

Huku akishangiliwa na wananchi hao waliokuwa wakimkatisha kwa kelele za shangwe, Lowassa alisema kwa kushirikiana na viongozi wenzake wamejipanga kufanya ziara ya kuijenga Chadema nchi nzima.

“Nina hakika tumewashika pabaya CCM na tumewaumiza sana. Sasa kwa kushirikiana na viongozi wenzangu tutazunguka nchi nzima tunataka kuiweka Chadema kwenye chama cha siasa na si uanaharakati,” alisema.

Akizungumzia Uchaguzi Mkuu uliomalizika Oktoba 25 mwaka jana, Lowassa aliwashukuru wananchi kwa kumpa kura nyingi akisema hata walioiba kura zake wanajua na dunia inajua kuwa alishinda.

“Niliamua kukaa kimya kwani najua ningesema jambo moja nchi yetu ingeangamia. Na vijana kila kona ya nchi walikuwa wakinipigia simu wakidai wanasubiri neno kutoka kwangu,” alisema.

“Sikufurahishwa na kwenda Ikulu kwa mikono iliyojaa damu. Kuna siku nitakwenda Ikulu kwa mikono safi ya Watanzania, nina hakika na rafiki zetu wanajua kabisa kwamba hawakushinda.”

MWANANCHI

Alikiba Awaomba watanzania kumpigia Kura Diamond Platnumz

Alikiba alisema haya kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio na kusisitiza kuwa yeye kusaini mkataba na kampuni ya ‘Sony Music’ jambo kubwa sana katika maisha yake ya muziki.

“Kiukweli toka nimerudi rasmi kwenye game na kutoa wimbo wa Mwana mashabiki walipokea vizuri sana Africa Mashariki, na kadili nilivyokuja kutoa wimbo mwingine wa Chekecha walizidi kuongezeka mashabiki na kujiona nina mashabiki wengi, hivyo kuja kusaini mkataba na ‘Sony Music’ ndani ya muda mfupi hivi kwangu mimi najiona ni kama nimepiga msamba maana siyo hatua za kawaida” alisema Alikiba.

Mbali na hilo Alikiba alimuombea msanii Diamond Platnum kwa watanzania ili wampigie kura kwenye tuzo anazoshiriki sasa na kusema kuwa yeye ndiye msanii pekee anayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano hayo hivyo watanzania wampigie kura ili aweze kushinda.

Magazeti ya Leo Jumanne ya May 24 kwenye habari za kitaifa kimataifa udaku na michezo.




 

Gallery

Popular Posts

About Us