KINGAZI BLOG: 08/10/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, August 10, 2016

Gazeti la Mseto lapewa siku 7 kumuomba radhi na kumlipa Bilioni 1 Naibu Waziri wa ujenzi

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi, Edwin Ngonyani amelitaka gazeti la Mseto kumuomba radhi na kumlipa fidia ya shilingi bilioni moja kutokana na kuandika habari ya kumchafua.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake Waziri Ngonyani amesema kuwa Gazeti hilo la tarehe 4 Agosti 2016 liliandika habari yenye kichwa cha Habari “Waziri amchafua JPM” ikimuhusisha na upokeaji wa fedha kutoka moja ya Kampuni ya Madini wakati akiwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (Stamico).

“Nimewaandikia notisi ya siku saba ikiwataka waombe radhi na kunilipa fidia, na wasipofanya hivyo hatua stahiki kuwapeleka mahakamani akiwemo Mwandishi Josephat Isango, Mwanahalishi Publisher na Mchapaji wa gazeti hilo”. Alisema Mhandisi Ngonyani.

Mhandisi Ngonyani amesema kuwa habari hiyo siyo ya kweli na mwandishi ametumia nyaraka za kughushi ikiwemo barua iliyoandikwa tarehe 24 Julai  na kutiwa saini yake akiwa Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO wakati ukweli ni kwamba tarehe hiyo yeye alikuwa ni Mkurugenzi kamili na siyo Kaimu kama barua hiyo inavyosomeka.

Ameongeza kuwa habari hiyo imewachafua watu wengi ikiwemo familia yake, wapiga kura wake wa jimbo la Namtumbo ambao walijitoa katika kumsaidia wakati wa kampeni na hali kadhalika zimemchafua Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumhusisha na fedha kutoka kwa wawekezaji wa nje kwa kuwaahidi kuwa mitaji yao nchini itakuwa salama.

“Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli alishasema kama kuna mfanyabiashara yeyote aliyechangia kuingia kwake ikulu ajitokeze na hakuna aliyefanya hivyo, Iweje leo mtu tu anaibuka na kuandika habari za kugushi? ”. Aliongeza.

Aidha Naibu Waziri huyo ametumia fursa hiyo kuwataka waandishi wa habari nchini kuwa waangalifu pindi wanapoandika habari za kutunga kwa kutotumia majina halisi kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na kanuni za uandishi wa hadithi (Habari za kutunga).

“Waandishi wa habari mnatakiwa kufuata maadili ya kazi yenu kwa kuandika habari zenye ukweli ili kuliepusha taifa kuingia katika machafuko na  migogoro isiyo ya lazima” Alisema Naibu waziri huyo.


Historia ya jezi namba 6, Manchester United katika EPL

Mnamo msimu wa mwaka 1992-1993 ligi kuu ya nchini England ilianza kutambulika kama ‘ENGLISH PREMIER LEAGUE (EPL) ‘ Ni ligi inayohusisha Club 20, Manchester ikiwa ni moja ya timu ya mpira inayoshiriki katika ligi hiyo.Ni klabu kubwa nchini England na barani Ulaya kwa ujumla, ndiyo club inayoongoza kwa kutwaa kombe hilo ikiwa imechukua mara 13 tangu ligi hiyo iaanze kutambulika kama EPL. Ni klabu ambayo Wanasoka Bora wengi duniani walishawahi kuchezea.

Na namba ya jezi mgongoni imekuwa moja ya alama kwa wachezaji. Leo tutajikita katika kuangalia historia ya jezi namba 6 na tutapata kuona wanasoka mashuhuli ambao walishaivaa jezi hiyo ndani ya Manchester United.

1995-1998 GARY PALLISTER

Mwaka 1989 alisajiliwa kutoka katika klabu ya Middlesbrough na ndio ulikuwa usajili ghali zaidi kwa mchezaji nafasi ya beki, ni beki wa kati aliyeweza kuisaidia timu yake ya Middlesbrough kupanda daraja kutoka ligi daraja la pili hadi ligi daraja la kwanza msimu wa mwaka 1988-1989 kabla ya Manchester United na kukabidhiwa jezi namba 6 mnamo mwaka 1993.

Mlinzi huyo wa kati mwenye asili ya Uingereza atakumbukwa pia kwa kuweza kuipeleka Manchester United fainal katika kombe la FA baada ya kuweza kuisawizishia bao katika dakika za nyongeza za mchezo  wa kwanza wa nusu fainal dhidi ya Crystal Palace na kufanya mchezo huo kumalizika kwa kufungana 2-2 na  hivyo  mchezo  kurudiwa na aliweza kuipatia tena goli Manchester United katika ushindi wa 2-0 katika mchezo wa marudiano na kufanikiwa kuipeleka katika fainal ya kombe la FA mwaka 1995.

1998-2001 JAAP STAM

Alisajiliwa kutoka klabu ya nchini kwao Uholanzi klabu ya PSV Eindhoven kwenda kuziba pengo la Gary Pallister ambaye alirejea katika klabu yake ya zamani ya Middlesbrough kwa kiasi cha pauni million 2.5 ikiwa kiasi kikubwa zaidi ya alichosainiwa nacho mara ya kwanza na klabu ya Manchester United. Stam alikabidhiwa jezi namba 6 iliyovaliwa awali na mlinzi wa kati Gary Pallister.

Jaap Stam alisifika kuwa beki mwenye kasi, nguvu na mwenye uwezo wa kuuchezea mpira, aliweza kudumu Manchester United kwa muda wa misimu mitatu na kuweza kushinda mataji matatu ya ligi kuu, taji moja la kombe la FA, kombe la mabara la vilabu pamoja na kombe la mabingwa barani Ulaya.

2001-2002 LAURANT BLANC

Alikuwa ni moja ya walinzi ambao walikuwa wakimvutia sana Sir Alex Ferguson. Sir Alex Ferguson alishajaribu mara kadhaa kutaka kumsajili mfaransa huyu tangu mwaka 1996 lakini juhudi zake ziligonga mwamba, kupelekea kuondoka kwa Jaap Stam na kuelekea katika klabu ya Lazio, Sir Alex Ferguson alijaribu tena bahati yake kumsajili mlinzi huyo na kuweza kuipata saini yake kutoka klabu ya Internazionale ya nchini Italia mwaka 2001 akiwa na umri wa miaka 35.

Laurant Blanc alirithi Jezi namba 6 kutoka kwa Jaap Stam na katika miezi mitano ya kwanza alionekana kutovaa viatu vya Mholanzi huyo kwani alionekana akiboronga katika nafasi yake ya ulinzi wa kati na kupelekea klabu ya Manchester United kupoteza mechi tano mfululizo dhidi ya Bolton Wandereres, Liverpool, Arsenal, Newcastle United na Chelsea (B.L.A.N.C) huku ukizuka utani wa kuwa timu zote hizo zilizoifunga Manchester United zinaunda Jina la B.L.A.N.C

2002-2003 RIO FERDINAND

Alisajiliwa na klub ya Manchester United kutoka klabu ya Leeds United kwa ada ya pauni million 30 ikivunja rekodi ya kuwa beki aliyesajiliwa kwa kiasi kikubwa cha pesa kuliko wote na huku akikabidhiwa jezi namba 6. Ila Jezi hiyo ikionekana kama ilimpa gundu baada kufungiwa kutojihusisha na mpira kwa muda wa miezi 8 ikiwa ni mwaka mmoja na miezi miwili mara baada tu ya kukabidhiwa jezi namba 6 na kujiunga na klabu ya Manchester United. Rio Ferdinand aliukosa mchezo wa  fainali  wa kombe la FA, na vilevile alishindwa kuiwakilisha timu yake ya taifa ya England katika michuano ya kimataifa ya barani Ulaya.

2003-2011 WES BROWN

Ndiye mchezaji pekee mpaka sasa aliyeweza kukaa na Jezi no 6 mgongoni katika Klabu ya Manchester United katika EPL kwani ameweza kudumu nayo kwa muda wa miaka 8. Aliweza kukabidhiwa jezi namba 6 miaka 7 baadae baada ya kupandishwa katika kikosi cha kwanza akitokea katika akademia ya Manchester United ambayo alijiunga nayo akiwa na umri wa miaka 12 mwaka 1992 na hadi kufikia  kupandishwa katika timu ya wakubwa ya Manchester United mwaka 1996.

Wes Brown alikuwa ni mmoja ya wachezaji walioweza kushinda mataji matatu (treble) mwaka 1999 chini ya uongozi wa Sir Alex Ferguson. Wes Brown alikuwa ni mmoja ya wachezaji waliopendwa sana na Sir Alex Ferguson aliwahi kunukuliwa akisema kuwa Wes Brown ni mmoja ya walinzi wenye asili ya Uingereza wenye vipaji vikubwa.

Kuwasili kwa Nemanja Vidic Mwaka 2006 na kuwa na kombinesheni nzuri na Rio Ferdinand katika ulinzi wa kati kukamfanya Sir Alex Ferguson kumuhamisha nafasi Wes Brown kutoka katika nafasi ya ulinzi wa kati na kwenda kucheza nafasi ya ulinzi wa pembeni huku akiwa na namba yake hiyohiyo 6 mgongoni na atakumbukwa katika kusababisha goli kwa kumpa assist Christiano Ronaldo katika mchezo wa fainal ya ligi ya Mabingwa Ulaya na kuisaidia Manchester United kushinda taji hilo mwaka 2008.

2011-2015 JONNY EVANS

Kabla ya kuanza kwa msimu wa mwaka 2011-2012 John Evans alipewa jezi namba 6 baada ya Wes Brown kuhamia klabu ya Sunderland Aug 2011 John Evans alivaa jezi yake mpya hiyo ya nambari  6 kwa mara ya kwanza katika mchezo wa kwanza wa ligi baina ya Manchester United dhidi ya West Browmich Albion ambapo aliingia dakika ya 52 kuziba pengo la  mlinzi wa kati Nemanja Vidic baada ya kuumia na Mchezo huo ulimalizika Kwa Manchester United kushinda 2-1.

Baada ya miezi saba na siku 4 baada ya John Evans kupewa jezi namba 6 aliweza kufunga bao lake la kwanza katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Wolverhampton Wanderers. Katika msimu huohuo 2011-2012 aliokabidhiwa jezi namba 6 alishindwa kuitumikia jezi namba 6 hiyo katika michezo mitatu ya mwisho wa msimu baada ya kupata majeraha ya mguu iliyompelekea kufanyiwa operation na kushindwa kufanya mazoezi ya kabla ya kuanza kwa msimu mpya (pre season) wa mwaka 2012-2013 huku kukiwa na makadirio kuwa angeweza kurejea katika mchezo wa pili dhidi ya Fulham. John Evans akiwa na jezi namba 6 aliweza kufunga bao lake la pili akiwa na jezi namba 6 katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Newcastle October 7 2012 na nyota yake ya kufunga iliendelea baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Robin Van Persie na kuweza kufunga bao lake la kwanza katika UEFA Champions League katika uwanja wa Old Trafford dhidi ya Braga.

Akiwa na jezi namba 6 mgongoni aligombana na mshambuliaji wa Newcastle Papis Cisse na kupelekea kufungiwa kwa mechi sita March 7 2015. John Evans aliiacha jezi namba 6 ya klabu ya Manchester United mnamo tarehe 29 Uugust 2015 baada ya kujiunga na West Browmich Albion.

2016-2017 PAUL POGBA

Awali jezi namba 6 katika klabu ya Manchester United ilionekana kuvaliwa na Walinzi hasa walinzi wa kati. Sasa jezi hiyo itavaliwa na kiungo ghali kwa sasa Paul Pogba baada ya kusajiliwa kwa kiasi cha £89 million kutoka Juventus.

Kiungo huyo amerejea tena na ‘Mashetani Wekundu’ baada ya kuondoka klabuni hapo mwaka 2012 kuelekea Juventus. Paul Pogba alisajiliwa kwa mara ya kwanza na Manchester United kutoka Le Havre ya nchini Ufaransa akiwa na miaka 16 na kuweza kupenya moja kwa moja katika kikosi cha vijana cha Manchester United na kuweza kufunga mabao 7 katika michezo 21 katika msimu wake wa kwanza 2009-2010.

Msimu uliofuata 2010-2011 aliweza kuendelea katika akademia ya manchester united hadi November 2010 alipoitwa katika kikosi cha akiba, aliingia katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Bolton Wanderers katika ushindi wa 3-1 Feb 2011  Paul Pobga alikuwa miongoni mwa wachezaji waliopandishwa kwenda katika kikosi cha timu ya wakubwa cha  Manchester United na Sir Alex Ferguson na alikabidhiwa jezi namba 42 na aliweza kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Arsenal katika mchezo wa ufunguzi na alioonyesha kiwango bora.

August 25 alifunga bao dhidi ya Swansea katika ushindi 6-0 3 July 2012 alijiunga na Juventus baada ya Sir Alex Ferguson kuthibitisha hilo na kuongezea kuwa Paul Pogba alionyesha utovu wa nidhamu kwa klabu hiyo ya jijini Manchester.

Baada ya miaka minne sasa amerejea Manchester United na kupewa jezi namba 6 yenye heshima klabuni hapo kwa sasa klabu hiyo ipo chini ya kocha Mreno Jose Mourinho na akitarajiwa Paul Pogba kufanya makubwa klabuni hapo baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano.


Wanawake 2 wakiri kufanya mapenzi na wanaume 355,000

Wanawake wawili (pacha) walio na miaka sabini na nne wameeleza kuhusu maisha yao na kazi yao ya Ukahaba.

Louise na Martine Fokkens wameeleza kuwa wamefanya kazi ya ukahaba kwa miaka 50 na kufanya mapenzi na zaidi ya wanaume 355,000!

“Hatukuwa na pesa, marafiki wa mume wangu ndio waliosema kuwa ingekuwa njia bora ya kupata pesa, ikabidi nijaribu. Wazazi wetu hawakuipenda hiyo kazi, ijapokuwa walikubali baadaye,” ameeleza Louise.

Dadake, Martine amesema kuwa alianza kuwa mfanyakazi wa kawaida tu katika danguro kabla ya kujiunga na dadake kama Kahaba.

“Sikuamini niliposikia kuwa dadangu alikuwa ameamua kuwa kahaba lakini baada ya muda, nilikubali tu,” amesema.


Wawili hao wanasemekana kuzindua muungano wa makahaba katika nchi yao.

Rais Uhuru Kenyatta awaita wageni wake 'Wezi'

 Rais Uhuru Kenyatta amejulikana kwa maoni yake hasa yanayowahusu wafisadi serikalini.

Katika mkutano ulioandaliwa katika ikulu ya Rais, Rais Kenyatta alisema kuwa kulikuwa na wezi kati yao.

Aitha, Rais Kenyatta alimpa changamoto Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya Bandari nchini Catherine Mturi, na kumsihi kulishughulikia swala la ufisadi katika bandani Pwani.

 “Ufisadi upo hata katika bandari yetu Pwani, lishughulikie swala hilo. Tushirikiane ili tujue mwizi ni yupi kati yetu,” Amesema.

Aitha, Rais Kenyatta alikiri kuwa kuna wengi serikalini walio na njia za kuwaibia wananchi.




Rais Magufuli Aanza Ziara Yake Mkoani Mwanza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella mara baada ya kuwasili katika Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Sengerema mkoani Mwanza mara baada ya kuwasili akitokea Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wanakwaya wa UWT Kisima cha maji Chumvi mara baada ya kuhutubia wakazi wa Sengerema mkoani Mwanza.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwalimu Mstaafu wa Shule ya Sekondari Sengerema Wilson Fumbuka Mbanga ambaye walifundisha naye shule hiyo tokea mwaka 1982-1985 mara baada ya kumaliza mkutano wa hadhara Sengerema Mkoani Mwanza.



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiaagana na wakazi wa Sengerema mkoani Mwanza mara baada ya kumaliza kuwahutubia.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Busisi wakati akielekea Mwanza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ndani ya kivuko cha MV. Misungwi wakati akielekea mkoani Mwanza. 

PICHA NA IKULU.

Mwigulu Nchemba Awaonya Polisi Wanaowabambikiza Kesi Raia

Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba amewaambia askari wa jeshi la Polisi mkoani Katavi kufanya kazi kwa taratibu na sheria bila kumuonea mtu yeyote hasa wanyonge.

Waziri Mwigulu ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kutembelea makazi ya watanzania wapya pamoja na kuzungumza na askari wa jeshi la polisi, Magereza pamoja na Uhamiaji.

Mhe. Mwigulu amesema kuwa Askari hao waondokane na tabia ya matukio ya kuwabambikizia kesi raia kwa maslahi binafsi na kuwaonea na kusema kuwa serikali kali ya awamu ya tano haitamfumbia macho askari atakayebainika kufanya hivyo.

Aidha Waziri Mwigulu amechukua fursa hiyo kuwapa hamasa Askari hao kwa kusema kuwa serikali itawaboreshea maslahi yao kadri bajeti itakavyoruhusu ili waweze kufanya kazi kwa weledi zaidi.

Kufanya Mapenzi na Binamu ni Halali Kenya..Mahakama Yapitisha

Mahakama ya juu nchini Kenya imehalalisha ngono baina ya mabinamu kwa sababu inakubalika katika baadhi ya jamii nchini humo.

Mahakama hiyo imemuachilia huru mtu mmoja aliyekuwa amefungwa kwa kosa la kushiriki ngono na binamu yake mwaka wa 2014 kwa sababu sio makosa nchini Kenya.

Jaji wa mahakama ya juu James Makau, alisema katika uamuzi kuwa kujamiana kwa maharimu sio haramu nchini Kenya.

''Ibara maalum inachoshughulikia ngono ya maharimu hajata binamu kuwa mmoja wa wale ambao kujamiana nao ni haramu maksudi, kwa sababu baadhi ya jamii nchini Kenya zinaruhusu sio tu ngono bali hata ndo baina yao''

Jaji wa mahakama ya juu James Makau, alisema katika uamuzi kuwa kujamiana kwa maharimu sio haramu nchini Kenya.

''jamii ya wahindi, waislamu na baadhi ya makabila humuhumu Kenya hukubali ndoa baina ya mabinamu'' alisema jaji Makau.

Bwana huyo ambaye anatambulika kama WOO alikamatwa mwaka wa 2014 kwa kushiriki ngono na mpenzi wake wa kike ambaye pia ni binamu yake na akahukumiwa kifungo cha miaka 10 gerezani.

''Kwa ufupi hakuna ushahidi wowote uliotolewa kuthibitisha kuwa ngono baina ya wawili hao ni kinyume cha sheria na kwa sababu hiyo ninaamuru mtu huyo aachiwe huru mara moja'' hukumu ya jaji Makau.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AUGUST 10 2016




 

Gallery

Popular Posts

About Us