KINGAZI BLOG: 05/25/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, May 25, 2016

Kamati, wabunge wambana Waziri Maghembe.



Dodoma. Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeitaka Serikali kuteua bodi za Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Wanyamapori, ambazo zimemaliza muda.

Mbali na kuteua bodi hizo, wameiomba Serikali kutoa fedha zinazotengwa kwa ajili ya wizara kwa wakati, kuiwezesha kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Bodi ya Tanapa ilimaliza muda wake mwaka 2014. Tangu wakati huo, Serikali haikuteua bodi nyingine kusimamia utendaji wa mamlaka hiyo.

Akiwasilisha hotuba kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati, Atashasta Nditiye, Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi alisema Wizara ya Maliasili na Utalii ina mchango muhimu kwa uchumi wa Taifa, endapo itasimamiwa kikamilifu.

Alisema baadhi ya mashirika na taasisi za umma yamekaa muda mrefu bila kuwa na bodi, hali inayoathiri utekelezaji wa majukumu ya mashirika hayo.

Kapufi alisema kamati inaitaka Serikali kuteua bodi za taasisi hizo, ziweze kufanya kazi kama ilivyopangwa.

Akizungumzia fedha za maendeleo kwa wizara hiyo, mpaka kufikia Machi, mwaka huu, alisema zilizopokewa ni Sh1 bilioni za nje, kati ya Sh7.7 bilioni zilizotengwa kwa ajili hiyo. Alisema fedha zilizotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo zilijumuisha Sh5.7 bilioni, fedha za nje na Sh2 bilioni za ndani. Hata hivyo, Serikali haikutoa kiasi chochote kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

“Katika miradi 10 ya maendeleo, hakuna hata mradi mmoja uliotekelezwa kwa ufanisi. Utoaji huu wa fedha za maendeleo ni hatari kwa maendeleo ya sekta hii muhimu,” alisema kaimu mwenyekiti huyo.

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Bukombe (CCM), Dotto Buteko ameapa ‘kufa’ na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Magembe kama hatapata majibu kuhusu unyanyasaji unaofanywa na askari wa wanyamapori katika Hifadhi ya Kigosi Moyowosi.

Akichangia hotuba ya wizara hiyo bungeni jana, Buteko alisema asilimia 40 ya ardhi ya Wilaya ya Bukombe ni hifadhi na hakuna uhusiano mzuri na wananchi wa maeneo ya jirani.

Alisema Kijiji cha Iloselo katika Kitongoji cha Mpalala, maofisa hao wamechoma moto myumba 40, wakati kijiji hicho kinatambuliwa na Serikali.

“Watu walipigwa na kuharibiwa mazao yao. Halafu watu wanaendelea kujitapa mtatufanya nini? Nakwambia mheshimiwa waziri, jambo hili lisipopata majibu leo nakufa na wewe,” alisema.

Alisema ni lazima wananchi wa Bukombe wafutwe machozi kwa udhalilishaji waliopata kutoka kwa maofisa hao.

Buteko alisema jumla ya ng’ombe 215 na punda wanne walipigwa risasi na askari ya wanyamapori, na alitaka apewe majibu kwa kitendo hicho. Alisema ng’ombe 603 wametaifishwa na kwamba kwenye kundi hilo la wamiliki watano, watatu walikubali kutoa fedha na wakadanganywa kuwa watapewa ng’ombe wao mahakamani, lakini hawakupewa hadi leo.

Mbunge wa Kaliua (CUF), Magdalena Sakaya alisema hotuba ya waziri wa Maliasili imeonyesha kuwa kuna mapori ya akiba 28 na mapori tengefu 42, lakini ukweli ni kwamba yapo katika vitabu na si halisia.

“Kaliua vijiji 21 vilivyosajiliwa vipo katika mapori ya akiba. Waziri akija hapa kuhitimisha, atueleze nini wanafanya kwa watu hawa ambao wanaishi maisha ya hofu,” alisema.

Mbunge Kasulu Mjini (CCM), Daniel Nsanzugwanko alitaka sheria ya misitu kupitiwa upya kwa sababu imepitwa na wakati.

“Mapori ya akiba yangepitiwa ili mipaka ihuishwe kuepuka migogoro ya kati ya wafugaji na wakulima,” alisema.

Mtoto wa Kabwe Agoma Kushikana Mkono na RC Makonda.

Anna Kabwe, binti wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe amegoma kumpa mkondo Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

Tukio hilo la aina yake lilimfika Makonda aliposhiriki shughuli ya kuaga mwili wa Kabwe katika Viwanja vya Karimjee alipokuwa akitoa mkono wa pole kwa familia ya Kabwe.

Wakati Makonda akimpa mkono, Anna aliendelea kuchezea simu yake huku akipuuza mkono wa kiongozi huyo. Anna alifanya hivyo akiwa amekaa huku ndugu zake wengine wakiwa wamesimama wakati wakipokea mkono huo wa pole.

Kitendo hicho kimetafsirika kwamba, Anna alikumbuka tukio lililofanywa Aprili 19 mwaka huu wakati wa uzinduzi wa Daraja la Kigamboni ambapo Makonda alimtuhumu marehemu Kabwe (baba yake) kwamba amehusika na kusaini mikataba iliyoikosesha mapato serikali.

Kabwe alifariki tarehe 19 Mei mwaka huu kutokana na tatizo la ini. Mauli yalimkuta akiwa katika Hospitali ya Mama Ngoma jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu. Ameacha mjane na watoto watano; wanne wa kiume na mmoja wa kike.

Waziri Mkuu Akutana na Watanzania Waishio Zambia


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watanzania waishio Zambia kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo Lusaka Mei 24, 2016. Majaliwa alikwenda Zambia kumwakilisha  Rais John Magufuli kwenye Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika- ADB uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi.

Baadhi ya Watanzania  waishio Zambia wakimsikiliza Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa wakatia lipozungumza nao kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo Lusaka.  Majaliwa  alikwenda Zambia kumwakilisha Rais John Magufuli kwenye  mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB, Mei 24, 2016.

Baadhi ya Watanzania  waishio Zambia wakimsikiliza Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa wakatia lipozungumza nao kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo Lusaka.  Majaliwa  alikwenda Zambia kumwakilisha Rais John Magufuli kwenye  mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB, Mei 24, 2016.

Baadhi ya Watanzania  waishio Zambia wakimsikiliza Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa wakatia lipozungumza nao kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo Lusaka.  Majaliwa  alikwenda Zambia kumwakilisha Rais John Magufuli kwenye  mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB, Mei 24, 2016.

(Picha na  Ofisi ya Waziri Mkuu)

WATU 14 WAKAMATWA MAUWAJI YA WATU WATATU MSIKITINI MWANZA



Jeshi la Polisi Nchini linawashikilia watuhumiwa 14 kufuatia tukio la mauaji ya watu watatu lililotokea katika msikiti wa Rahman eneo la Ibanda relini mkaoni Mwanza, Mei 18 mwaka huu.
Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidizi Advera Bulimba alisema kuwa msako wa kuwakamata watuhumiwa wengine unaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.
Hivyo amewaomba wananchi kutoa ushirikiano mkubwa kwa jeshi hilo ili kufanikisha kuwakamata wale wote wanaotuhumiwa kuhusika na tukio hilo.
“Nitoe wito kwa wananchi kushirikiana kikamilifu na vyombo vya usalama katika kufichua wahalifu kwa kuwa ni watu tunaoishi nao, hivyo hakuna budi kutoa taarifa zao ili usalama na mali zetu uendelee kuimarika”, aliongeza Kamishna Msaidizi Bulimba.
Hata hivyo, alieleza kuwa hali ya usalama nchini iko shwari na kuwatoa hofu wananchi kwamba jeshi hilo limejipanga kikamilifu katika kuhakikisha hali ya usalama inaendelea kuwepo.
“Niwaombe wananchi kuondoa hofu juu ya hali ya usalama na wasiwasi na watoe ushirikiano kwa vyombo vya dola ili kuhakikisha kwamba wote wanaojihusisha na uhalifu wanakamatwa haraka”, alisema Kamishna Msaidizi  Bulimba.
Aliongeza kuwa uchunguzi zaidi wa matukio ya uhalifu nchini unaendelea ikiwemo matukio ya mkoani Tanga, Dar es Salaam na mikoa mingine ili kubaini na kuwakamata wahusika na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Hivi karibuni kumeripotia matukio mbalimbali ya uvunjifu wa amani katika mikoa mbalimbali  ikiwemo mauaji ya watu watatu waliouawa wakiwa msikitini jijini Mwanza.

Tuhuma za Kuwanyang'anya wananchi ardhi lowassa azungumza,Lukuvi naye aahidi mazito

Baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kueleza Bungeni kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alijimilikisha ardhi iliyotolewa kwa wananchi wilayani Monduli mkoani Arusha na kuahidi kuirejesha, Mwanasiasa huyo amejibu tuhuma hizo.

Lowassa amesema kuwa halijui shamba alilolizungumzia Waziri huyo na kwamba hakuna ardhi ambayo anaimiliki kinyume cha taratibu.

Alisema kuwa hana taarifa kamili kuhusu maelezo ya Waziri Lukuvi na kwamba ameomba Mbunge wa Jimbo la Monduli, Julius Kalanga (Chadema) kulifuatilia kwa karibu na kumpa taarifa ili aweze kulitolea ufafanuzi.

“Nashindwa kutoa maelezo kuhusu taarifa hizo kwa sababu sifahamu lolote kuhusu shamba hilo,” Lowassa anakaririwa na gazeti la Jambo Leo lililofanya nae mahojiano kwa njia ya simu. 

“Mimi sipo Bungeni, nimesikia hizo habari, lakini sijui zimetolewa lini na nani. Mbunge wangu analifanyia kazi kwa sababu sina shamba nilalolimiliki ambalo liko kinyume na taratibu,” aliongeza.

Akijibu hoja ya Mbunge wa Monduli kuhusu umiliki na uporaji wa ardhi unaofanywa na vigogo jimboni humo, Waziri Lukuvi alieleza kuwa kuna shamba ambalo lilidhaminiwa na Rais Benjamin Mkapa ili wapewa wananchi jimboni humo, lakini  Lowassa alijimilikisha.

“Lile Shamba la Makuyuni lilitolewa kwa wananchi litarudi kwao na ukae ukijua litakuwa kwao kwa sababu aliyejimilikisha ni Edward Lowassa,” alisema Lukuvi na kuahidi kulirejesha mikononi mwa wananchi hao.

Mkoa wa Mwanza Unategemea Kupokea Tani 500 za Sukari


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amesema mkoa wa Mwanza unategemea kupokea Tani 500 za Sukari zitakazo ingia katika mkoa huu zikitokea kiwanda cha sukari cha Kagera Sugar tarehe 24, Mei, 2016, ambazo zinaingizwa mkoani hapo na muagizaji na Msambazaji P.H  Shah.

Hata hivyo mkuu wa mkoa ameonya watu watakao uza sukari hiyo kinyume na bei elekezi kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja nakufikishwa katika vyombo vya dola.

Mongella amesema pia kwamba, kupitia kamati yakushughulikia sukari, tayari wametoa maelekezo kwa Wakuu wa wilaya jinsi yakushughulikia suala la sukari na kwamba wasambazaji wote katika Wilaya lazima wazingatie maelekezo bila kuvunja utaratibu utakao wekwa.

Mahitaji ya sukari katika mkoa wa Mwanza ni Tani 1,500 kwa wiki kwa matumizi ya kawaida kwa wananchi wake, hivyo kuwasili kwa tani 500 itasaidia kupunguza uhaba wa sukari  unao ukabili  mkoa huu kwa sasa..

Hata hivyo mkuu wa mkoa amewatoa wanachi hofu juu ya sukari kwakusema, tayari viwanda vya hapa nchini vimekwisha anza uzalishaji wa sukari na kwamba muda si mrefu tatizo la sukari litapungua kama sio kuisha kabisa.

Imetolewa na Atley J. Kuni

Afisa habari na Mahusiano, Ofisi ya mkuu wa Mkoa

MWANZA -24, Mei 2016

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo jumatano Mei 25 kwenye habari za kitaifa kimataifa na michezo

Karibu,tunakuletea kile kilichoandikwa kwenye magazeti ya tanzania leo ili ufahamu kilichojiri kwenye habari za leo.Usisahau kukaa nasi ku 'like' kwenye facebook/tanzaniampyasasa blog na twitter@tanzaniampyasasa.



 

Gallery

Popular Posts

About Us