KINGAZI BLOG: 04/17/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, April 17, 2016

Mzimu wa Anne Kilango Wazidi Kuwatesa Wananchi Shinyanga,Vilio Kila Kona,Wakata Tamaa



 
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kuwa ni mzimu wa "Anne Kilango",simanzi imeendelea kuwagubika wakazi wa Shinyanga kufuatia rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutengeua uteuzi wa aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Anne Kilango Malecela. 


Wakazi hao wa Shinyanga wameeleza kusikitishwa na kitendo hicho na kueleza kukata tamaa kama watapata tena kiongozi mchapakazi kama Kilango kwani walikuwa na imani kubwa na mwana mama huyo machachali.

Uteuzi wake ulitenguliwa baada ya Machi 20, mwaka huu, kudai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna mtumishi hewa wa serikali hata mmoja. 


Ikulu ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa katika taarifa za awali kuna watumishi hewa 45, huku kazi ya uhakiki ikiendelea katika wilaya za Ushetu na Shinyanga. 

Hata hivyo wakazi wa Shinyanga wakiwemo mama ntilie,waendesha bodaboda,wakulima,waumini wa madhehebu ya dini wameeleza uamuzi uliochukuliwa na rais kuwa ni wa haraka sana kudai kuwa kutokana na ugeni wa Kilango,aliyepaswa kuwajibishwa alikuwa ni katibu tawala wa mkoa kwani ndiyo mtendaji mkuu wa mkoa.

Wakizungumza na waandishi wetu kwa nyakati tofauti ,baadhi ya wakazi wa Shinyanga wameeleza kukataa tama ya kupata mkuu wa mkoa mwajibikaji kama Anne Kilango Malecela aliyeonesha upendo kwa wananchi wa mkoa huo mara tu baada ya kuwasili mkoani humo. 

Mama Ntilie Wazungumza
Baadhi ya akina mama lishe/ntilie wanaofanya shughuli zao katika soko kuu la Shinyanga walisema kutokana na kuondolewa kwa Mama Kilango hawaamini tena kuwa watapata mkuu wa mkoa mchapakazi kama Kilango. 

"Kwa hali ilivyo katika mkoa wa Shinyanga sasa,anatakiwa kiongozi kama Kilango,kwani ni mwanamke jasiri sana,hapa wamepita wakuu wa mikoa 18 wanaume,huyu mama kwa jinsi ninavyomjua,hakika angekimbiza maendeleo ya mkoa huu kwa kasi ya ajabu",alisema Mwanaisha Abdalah.

“Jamani tusifichane,tumepoteza mpiganaji,huyu mama ni jembe kwani tumekuwa tukimuona hata bungeni jinsi anavyopambana,kwanza alionesha upendo kwa wakazi wa Shinyanga,akaitisha hadi mkutano wa hadhara na kuahidi kuwatembelea wananchi walau mara moja kwa wiki ili kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua”,alieleza Halima Shaban,mmoja wa mama lishe hao. 

Wakulima Watoa ya Moyoni 

Baadhi ya wakulima kutoka kijiji cha Imesela katika wilaya ya Shinyanga walisema walipata mshtuko kusikia mkuu wa mkoa kaenguliwa nafasi hiyo na kudai kuwa rais hajatenda haki kwani ni mgeni mkoani humo waliopaswa kuwajibishwa ni maafisa utumishi na makatibu tawala. 

Boda boda wanena
Waendesha bodaboda nao walisema kuwa kilichofanyika ni kuponzwa kwa Kilango na watendaji wa serikali wanaomsaidia katika ofisi. 

“Tunamuomba mheshimiwa rais atuonee huruma wanashinyanga kwa kuturidishia kipenzi chetu Kilango,tulikuwa na imani naye ya kutukomboa wananchi,mi nafikiri Pengine mama yetu alikuwa amechanganyikiwa kutokana mme wake Mzee John Malecela kuwa ni mgonjwa hivyo akaamini kila taarifa aliyopewa na katibu tawala wake”,alisema Juma Hatibu. 

Hali halisi katika ofisi za mkoa
Uchunguzi tulioufanya umebaini kuwa wafanyakazi wa mkoa wa Shinyanga hawana furaha kutokana na mkuu wao kuondolewa kwa mkuu wao

Baadhi ya wafanya kazi wa ofisi hiyo waliokataa kutajwa majina yao walisema Kilango alionesha upendo kwao baada ya kuwasili mkoani na kuamini kuwa ndiye kiongozi pekee mwenye uwezo wa kumaliza matatizo ya wananchi na hata wafanyakazi kitendo kilichowafanya watoe machozi baada ya kupata taarifa za kuenguliwa kwa mkuu wao.

Akiwasalimia waumini wenzake juzi, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, mjini Shinyanga, baada ya kupewa fursa ya kusema neno, Kilango alisema anamshukuru Mungu kwa kila jambo kwa yote yaliyomtokea.

“Ndugu waumini wenzangu, hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu, hata mtu unapojifungua mtoto akafariki dunia, unamshukuru Mungu kwani hayo ni mapenzi ya Mungu.


"Ukiona mzazi wako kafariki dunia pia, unamshuruku Mungu. Tunao wajibu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema kwa maneno mafupi na kisha kuketi, huku akiacha simanzi miongoni mwa waumini wenzake, wakiwamo viongozi wa kanisa.

Baadhiya waumini wa kanisa hilo waliozungumza na waandishi wetu walisema uamuzi uliofanywa na mheshimiwa rais yanaumiza kwani wakazi wa Shinyanga walitegemea Kilango kuwa kiongozi wa mfano wakiamini uchapakazi wake utausaidia mkoa kupiga hatua. 


"Tunamuomba mheshimiwa rais abadilishe mawazo na kuturudishia mkuu wetu wa mkoa Anne Kilango,tuna imani kubwa na Mama huyu,hatuoni kosa lake,hana kosa aliyepaswa kuondolewa ni katibu tawala kwani ndiyo mtendaji mkuu",walisema waumini hao.

Ofisi ya Bunge Yalivaa Gazeti la Nipashe Habari ya LUGUMI,Yalitaka Liombe Radhi



Ofisi ya Bunge imebaini upotoshwaji mkubwa Katika habari iliyochapishwa na Gazeti la Nipashe toleo la Aprili 16, 2016 yenye kichwa cha habari kisemacho “ Bunge sasa laufyata mkataba wa Lugumi”. 

Habari hiyo imeandikwa kufuatia ufafanuzi uliotolewa na Bunge jana kuhusu maagizo yaliyotolewa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) dhidi ya utekelezaji wa mkataba wa Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd  kuhusu mradi wa utambuzi wa alama za vidole (AFIS) (Automated Fingerprint Identification System.)
 
Ndani ya habari hiyo pia, Gazeti hilo limeeleza kuwa kamati ya PAC iliwahi kuliandikia Jeshi la Polisi kulitaka liwasilishe mkataba huo mbele ya Kamati, jambo ambalo si kweli bali ni upotoshwaji wa makusudi wenye lengo la kujenga hisia mbaya kuhusu mwenendo wa shughuli za Bunge mbele ya Umma.
 
Ukweli ni kwamba PAC haijawahi kuliandikia jeshi la Polisi kama inavyodaiwa na Gazeti hilo. Nukuu ya  maelezo ya PAC katika Hansard kwa Afisa Masuhuli kuhusu jambo hilo inasema kama ifuatavyo:
 
“Kamati inamuagiza Afisa Masuhuli kuwasilisha maelezo ya kina kuhusu utekelezaji wa Mkataba baina ya Jeshi la Polisi na  Kampuni ya Lugumi Enterprises  kuhusu mradi wa AFIS. Maelezo hayo yawasilishwe kwa Ofisi ya  Katibu wa Bunge kabla ya Jumatatu tarehe 11 Aprili, 2016”.
 
Katika agizo hilo PAC haikuwa imeandika kwa maandishi kuhusu agizo lake hilo hadi tarehe 12 Aprili, 2016 ilipo mweleza Katibu wa Bunge aweze kuwasilisha agizo hilo kwa maandishi ili liweze kupata Kinga chini ya Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge ambapo barua iliandikwa na kuwasilishwa kwa Afisa Masuhuli ili kupatiwa maelezo hayo kabla ya tarehe 18 Aprili, 2016.

Aidha, Mwandishi pia amelituhumu Bunge kuwa lina nia ya kuficha ukweli kuhusu jambo hili kwa kusema   taarifa ya ufafanuzi iliyotolewa na Bunge ni “kama kufunika kombe mwanaharamu apite kwa kujaribu kupotosha maagizo ya yaliyotolewa na kamati ya PAC ambayo inataka kuuona mkataba huo”

Ni vyema ikafahamika kuwa si jambo jema kwa mwandishi au chombo chochote cha habari kulituhumu Bunge linapotekeleza majukumu yake kwa kuwa Bunge linafanya kazi zake kwa kwa kuzingatia kanuni zake za Kudumu ikiwa ni pamoja na Sheria.  
 
Ofisi ya Bunge inalisihi Gazeti la Nipashe kuomba radhi kutokana na taarifa yake hiyo iliyojaa upotoshwaji mkubwa kwa uzito ule ule au kurekebisha taarifa yake kulingana na ukweli ulivyo haraka iwezekanavyo.

Imetolewa na;
Ofisi ya Bunge,
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano,
S.L.P 9133,
DAR ES SALAAM.
16 Aprili, 216.

DARAJA la Kigamboni Laanza Kutumika Kwa Mbwembwe...Wengine Wafanya Kama Sehemu ya Kivutio


Baada ya Serikali kuruhusu matumizi ya daraja jipya la Kigamboni kwa watembea kwa miguu na magari kwa majaribio, hatua hiyo imepeleka neema kwa wakazi wa mji huo, huku ikipunguza idadi ya vyombo vya moto katika vivuko.

Jana asubuhi, mwandishi wetu alishuhudia magari yakipita katika daraja hilo, kama ilivyo katika barabara zilizozoeleka za Mandela na Morogoro, huku baadhi ya madereva wakiendesha na kujipiga picha kwa simu za mkononi.

Watembea kwa miguu nao hawakuwa nyuma na idadi yao ilizidi kuongezeka mchana baada ya mvua zilizokuwa zikinyesha kuisha na sehemu kubwa walionekana kama watalii waliokuwa wakipiga picha na kuzunguzunguka katika eneo hilo.

“Sasa hivi mtu anakuwa na chaguo apite wapi anapoona atafanikisha safari yake kulingana na mahitaji,” alisema mmoja wa madereva waliotumia daraja hilo, Emmanuel Nzera.

Alisema kufunguliwa kwa daraja hilo ni neema kwa kuwa litaondoa usumbufu wa foleni katika vivuko upande wa Kigamboni na Feri na kwamba, kinachosubiriwa sasa ni gharama ya kulipia itajwe.

Mkazi wa Kigamboni, Ashura Ally alisema matumizi ya daraja hilo yatarahisisha usafiri kwa kuruhusu daladala kupita, jambo ambalo litawapunguzia gharama za bodaboda.

“Sasa kutakuwapo na wingi wa watu, hivyo na magari yatakuwa na safari za huku ambazo zitatusaidia kufika Feri na mjini kwa urahisi,” alisema.

Awali, mitumbwi ambayo ilikuwa ikitumika kuvusha abiria kabla kutoka Kigamboni kwenda Kurasini ilionekana ikiwa imeegeshwa kwenye ufukwe chini ya daraja hilo.

Hata wakati magari mengi na watu wakikimbilia katika daraja hilo la kisasa, hali ilikuwa tofauti katika eneo la Kivukoni kulikoshuhudiwa magari machache yakiingia kwenye vivuko vya Mv Kigamboni na Mv Magogoni.

Idadi kubwa ya watu iliyozoeleka kuwapo katika eneo la kusubiria vivuko mwishoni mwa wiki ilionekana kupungua na hakukuwa na pilika za abiria kuwahi kuingia kwenye vivuko.

Mmoja wa madereva waliokuwapo Kivukoni, Mussa Nzilo alisema ataendelea kutumia vivuko kwa kuwa kuna watu wanakaa maeneo ya karibu na Feri, hivyo kutumia daraja itakuwa safari ndefu kwao.

“Mimi nakaa hapo Feri kwenye kota za Bandari nikisema nipite kule Kurasini nitapoteza muda, ikizingatiwa kwamba huku hakuna foleni kama unavyoona sehemu kubwa ya watu wamekimbilia darajani,” alisema Nzilo.

Pamoja na watu wengi kuhamasika kutumia daraja hilo, kulikuwa na mkanganyiko wa baadhi ya watumiaji kushindwa kufahamu njia sahihi wanazotakiwa kupita.

Wafanyabiashara katika eneo hilo walisema huenda daraja likawa neema kwao kutokana na kuongezeka kwa watu, hivyo mzunguko wa fedha unaweza ukaongezeka.

“Japokuwa sijaona kituo, lakini hata kitendo cha watembea kwa miguu kupita hapa kwa wingi inaashiria baada ya kuzinduliwa rasmi pengine idadi ya watu itaongezeka na kusababisha kupanuka kwa biashara,” alisema Neema Nditi.

Daraja hilo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi Jumanne ijayo na Rais John Magufuli.

Msanii TUNDA MAN apata AJALI mbaya ya gari Mkoani Iringa.Habari za Kifo na Majeruhi soma Hapa.


Kama ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii utakua umekutana na taarifa inayomhusisha Tunda Man kupata ajali  akiwa Mkoani iringa Asubuhi ya April 17 chanzo cha habari kimempata Tunda Man mwenyewe na amekubali kutuelezea.


Maelezo ya mwanzo ya Tunda Man amesema
‘Tulikua tunatoka Njombe baada ya kumaliza show yetu na tukasema bora tusilale tuwahi kufika Dar,tumetoka Njombe saa 10 alfajiri mimi nikawa nasikia usingizi nikamwambia mwanangu hebu tuendeshe kidogo,kufika kijiji cha Idetelo kilomita kama 20 au 30 kabla ya kufika Mafinga tukiwa tumelala tukashtuka Gari inaingia porini tukasikia mshindo mkubwa gari imepiga puuuh Dereva hapo hapo akawa amefariki‘

Tunda Man anamalizia kwa kusema
‘Tulikua watu watano kwenye gari aliyekaa mbele na Dereva amevunjika mkono na nyama zimechanika,kuna mtu aliyekua nyuma mapafu yamepasuka,Mimi nipo poa,kwa sasa hivi tuko Mafinga hapa Hospitali ya Wilaya tunaangalia taratibu za kuchukua mwili tuupeleke Kilosa kwa ndugu zake,marehemu aliyefariki anaitwa Mussa lakini watu wengi wanamjua kwa jina la Man katuzo.

chanzo;Millard ayo.com
 

Gallery

Popular Posts

About Us