KINGAZI BLOG: April 2016

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Saturday, April 30, 2016

HIZI HAPA NAFASI ZA AJIRA KWENYE MAKAMPUNI MBALIMBALI HAPA NCHINI.

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo April 30 2016 kwenye,Habari zaUdaku, Kitaifa,kimataifa na michezo.


   April 30 2016 naanza kwa kukuletea habari zote kubwa zilizobebwa kwenye Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye ,habari za kitaifa,kimataifa Michezo na udaku na stori nyingine kali ili ujue kilichojiri duniani.. usiache kukaa karibu kwenye kurasa...

Jipya kuhusu kifo cha Pamba Wemba, tazama huyu jamaa kwenye video hii.

Taarifa  ambazo zinazidi kuenea kwenye vyombo vya habari Congo na mitandao ya kijamii hata hapa Tanzania ni msiba wa Papa Wemba lakini sasa mjadala umehamia kwenye namna kifo chake kilivyotokea
Kipande cha video kinachomuonesha jamaa akichukua mic halafu akairudisha kwenye stage na baada ya Pamba Wemba Kuanguka inadaiwa jamaa yuleyule badala ya kumsaidia alikimbilia mic ili isijulikane. Taarifa zinazoenea ni kwamba mic ile ilikuwa imewekewa sumu.
Hapa Mwanamuziki wa Congo anayeishi Tanzania, Papii Catalogue ameitafsiri video hiyo kwa lugha ya kiswahili, unaweza kuitazama

bofya hapa kutazama video

HII HAPA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA CHADEMA


CHADEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vincent Mashinji amesema kuwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi ndiyo msingi imara pekee unaoweza kuweka mifumo na taasisi kwa ajili ya maendeleo ya kweli yatakayogusa maslahi ya Watanzania wote badala ya nchi kuongozwa na kauli za viongozi.

Kutokana na umuhimu huo wa kuzingatia maoni ya wananchi yanayobeba matakwa yao katika mchakato wa Katiba Mpya, amesema kuwa CHADEMA hakitashiriki Kura ya Maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa ambayo ilipitishwa na Bunge Maalum la Katiba baada ya kubadili na kuondoa mapendekezo yaliyotolewa na wananchi kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya.
Badala yake, CHADEMA kitaendelea kuweka agenda ya kupigania Katiba Mpya na bora katika vipaumbele vyake, kwa sababu itatibu vidonda na kumaliza makovu yaliyoko katika jamii kutokana na matatizo mbalimbali kama vile ukosefu wa haki, migogoro ya ardhi, wananchi kukosa huduma za msingi za kijamii zikiwemo elimu, maji na afya.

Dkt. Mashinji ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipoukaribisha ujumbe wa Chama cha Centre Party cha Norway uliofika ofisini kwake jijini Dar es Salaam kutia saini makubaliano ya ushirikiano kati ya vyama hivyo kwenye Mradi wa Elimu ya Demokrasia awamu ya pili unaofanyika Wilaya ya Mtwara Vijijini.

Dkt. Mashinji pia amekishukuru chama hicho kwa kusaidia kutoa elimu ya uraia kwa Watanzania hususani maeneo ya vijijini katika mradi ambao unahusisha vyama vyote vya siasa vyenye uwakilishi ndani ya Bunge, huku akisisitiza kuwa CHADEMA kiko tayari kwa ushirikiano unaozingatia maslahi na matakwa ya wananchi hasa katika kukuza uelewa wa kudai haki, demokrasia na uongozi bora ndani ya nchi.

“Suala la Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi kama ilivyowasilishwa kwenye rasimu ya pili na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ni agenda muhimu kwa Watanzania wapenda nchi yao na sisi ni kipaumbele kwa mwaka huu na kuendelea hadi hapo nchi yetu itakapopata Katiba Mpya ya Wananchi.

“Jana na leo tumewasikia baadhi ya viongozi wa serikali wakisema kuwa wanajiandaa kuitisha kura ya maoni…hatutashiriki kura ya maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba. Tunajua Watanzania wengi wanataka Katiba Mpya iliyotokana na maoni yao, si ile iliyochakachuliwa bungeni.

“Katiba Mpya iliweka masuala kuhusu haki za wananchi, kuimarisha misingi na kuweka mifumo ya demokrasia na uongozi bora, walau kwa kuanzia. Hatuwezi kusema sasa tutatumia mikakati gani kuwahamasisha Watanzania kuidai Katiba Mpya…tutajua namna ya kuvuka tukishafika mtoni,” amesema Katibu Mkuu Dkt. Mashinji.

Aidha, Katibu Mkuu Dkt. Mashinji amesisitiza kuwa suala la nchi kuwa na misingi na mifumo imara ya demokrasia na uongozi bora ni muhimu kwa Tanzania, katika wakati ambapo nchi inaelekea kwenye uchumi mkubwa wa nishati ya gesi na mafuta, akisema vinginevyo ni hatari iwapo taifa lenye utajiri mkubwa wa rasilimali, litaendelea kuwa na wananchi waliokata tamaa kutokana na mfumo mbovu uliopo.

Akisisitiza umuhimu wananchi kuwa Katiba inayotokana na wananchi, Dkt. Mashinji alitolea mfano wa nchi ya Norway ambayo miaka mingi nyuma ilikuwa sawa na Tanzania, lakini ilifanikiwa kuondokana kuwa taifa maskini kutokana na uwepo wa uongozi bora, mifumo na taasisi imara za kidemokrasia ambazo ziliweza kusimamia ustawi wa taifa hilo kutokana na uchumi wa gesi na mafuta na sasa ni kati ya mataifa yaliyoendelea barani Ulaya na duniani kwa ujumla.

Kwa upande wake ujumbe huo uliokuwa ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Centre Party, Knut Olsen, umesema kuwa chama hicho kinashukuru kwa mradi huo kuingia katika hatua ya pili kuanzia mwaka 2016-2019 huku hatua ya kwanza ikiwa na mafanikio makubwa katika jamii ya wananchi wa maeneo ya pembezoni.

“Kama unavyojua, mradi huu kupitia TCD unahusisha vyama vyote vyenye uwakilishi ndani ya bunge, na lengo letu ni kuwajengea uwezo viongozi wa vyama hasa wanawake na vijana katika ngazi ya jamii kwenye vitongoji, vijiji, kata na bunge ili waweze kushiriki mchakato wa maamuzi. Tunatarajia kuendelea kupata ushirikiano katika hatua ya pili,” amesema Inger Bigum, ambaye ni Meneja wa Mradi hapa nchini.

Wengine waliokuwa katika ujumbe huo wa Centre Party ni pamoja ni Katibu Mkuu wa Vijana Sara Hamre, Katibu Mkuu wa Wanawake, Eline Stokstad-Oslan na Katibu Mkuu wa Wazee, Kristin Madsen.

Mradi huo wa Elimu ya Demokrasia katika Wilaya ya Mtwara Vijijini unaohusisha vyama vyenye uwakilishi bungeni kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) chini ya ufadhili wa chama hicho, katika awamu ya kwanza ulihusisha kata za Msangamkuu, Nanyamba, Ziwani na Mbembaleo na katika sasa awamu ya pili utakuwa katika kata za Mkunwa, Tangazo, Mayanga na Madimbwa.

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

LULU AAMUA KUONYESHA PETE YAKE YA UCHUMBA HADHARANI

Msanii wa filamu za kibongo Elizabeth Michael maarufu kama lulu amekuwa akipost picha mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii akiionyesha  pete aliyovalishwa iliyopo kwenye kidole chake huku akiweka baadhi ya maneno kwenye post hizo.hebu jionee hapa picha hizo,Na Haya ndo maneno aliyoyaandika.

Simplicity z the key.
Kwenye picha nyingine ameandika: Pale unaposikia Kwa…Kwa…Kwa…Kwa Ya Rihanna wakati WA kupiga picha #simplicityisthe.
:


Friday, April 29, 2016

VIDEO:Trump achekwa kwa alivyotamka Tanzania

Trump

Trump alishambulia sana sera ya kigeni ya Obama
Mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump amekejeliwa mtandaoni baada ya kuonekana akiboronga akitamka Tanzania wakati wa kutoa hotuba.
Bw Trump alikuwa akizungumzia mashambulio ya kigaidi yaliyotekelezwa katika mabalozi ya Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998 wakati wa kuzungumzia sera yake ya kigeni.
Badala ya kutamka vyema ‘Tanzania’ anasikika akitamka ‘Tan-zay-nia’.
Mashambulio hayo yalitekelezwa na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda.
Msemaji wa ikulu ya White House pia alimcheka Bw Trump alipoulizwa kuhusu vile mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York alivyotamka jina Tanzania.
“Kweli, yamkini jinsi ya kutamka huwa haijaelezwa kwenye kifaa cha kuonesha maandishi ya hotuba,” alieleza afisa wa habari wa ikulu Bw Josh Earnest.
Wakati wa hotuba hiyo, alizungumzia pia kuhusu kundi la Islamic State ambalo kwa sasa limeanza kunawiri nchini Libya. Kundi hilo hujulikana pia kama Isis.
“Na sasa Isis wanapata mamilioni na mamilioni ya dola kila wiki kwa kuuza mafuta ya Libya. Na wajua? Huwa hatuwawekei vikwazo vya kutouza, hatuwaangushiwi mabomu, hatufanyi lolote,” alisema.
“Ni kana kwamba nchi yetu haifahamu yanayofanyika, jambo ambalo huenda likawa kweli.”
Kwenye hotuba yake, Bw Trump alikosoa sera za kigeni za Rais Barack Obama.
Lakini Bw Earnest alipuuzilia mbali madai ya Bw Trump ambaye kwa sasa anaongoza miongoni mwa wagombea wanaotaka kupeperusha bendera ya chama cha Republican

.BOFYA HAPA KUONA VIDEO TRUMP AKICHEKWA BAADA YA KUSHINDWA KUTAMKA TANZANIA

Rais Magufuli Awasili Mkoani Dodoma Kwa Usafiri wa Gari.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma wakati akitokea mjini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Charles Kitwanga mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukielekea Dodoma kutokea mjini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Picha 9 za Jeshi letu la JWTZ Likiwa Katika Uwanja wa Mapambano Huko Congo DRC


Hapa  kuna Picha Kadhaa za Wanajeshi wetu wa JWTZ  Wakiwa  katika  uwanja wa Mapambano katika Misitu ya Ben Congo DRC.

Juzi kati, jeshi letu limetunukiwa  medani na MONUSCO Kwa umahili wake

==>Habari hii,picha pamoja na video ni kwa hisani ya  mwandishi na correspondent wa ITV anayeripoti toka Congo ndg. Eshongulu Eshongulu Eshongulu

Kumbe TID alishawahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu

TID




Msanii mkongwe wa muziki, TID amesema kipindi cha nyuma alikuwa anatoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu lakini baadae alitemwa hali ambayo ilimuumiza sana.

Akizungumza katika kipindi cha Clouds TV Ijumaa hii, TID amesema hali hiyo ilimfanya atoke na wasichana wengi.
“Nilikuwa ‘namdate’ Wema Sepetu akaniambia sikutaaki, tangu kipindi hicho nimekuwa na wasichana wengi. Ikitokea Wema anataka kurudi hakuna nafasi, I’m occupied,” alisema TID.
TID amesema katika kipindi hicho aliumizwa sana na jinsi magazeti yalivyokuwa yanamuandika vibaya.
“Wakati huo mitandao ya kijamii haikuwepo lakini wamagazeti walizichukua picha na kufanya yao, it was bad. Mimi nikasema sawa lakini niliumia sana,” alisema TID.
Muimbaji huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Confidence’ aliyomshirikisha Joh Makini pamoja na Dully Sykes.

Naibu Spika Achafua Hali ya Hewa Bungeni Baada ya Kumwita Mbunge BWEGE


Naibu Spika Tulia Ackson, ambaye katika vikao vya Bunge anatakiwa kusimamia mijadala kwenye chombo hicho cha kutunga sheria, jana alizua kizaazaa baada ya kumuelezea mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Selemani Said Bungara kuwa ni bwege, akimtaka aache kuonyesha hali hiyo.


Kwa mujibu wa toleo la pili la Kamusi ya Kiswahili Sanifu (Oxford) la mwaka 2004, neno bwege linamaanisha “mtu mjinga, mpumbavu, bozi, fala gulagula”.


Kitendo cha kutumia neno bwege kumuelezea mbunge huyo kilisababisha wapinzani wacharuke, na kuibua bungeni kesi ya mtu aliyefunguliwa mashtaka mkoani Arusha kwa kosa la kumuelezea Rais John Magufuli kuwa ni bwege.


Bila ya kuruhusiwa, mmoja alifungua kipaza sauti na kusema: “Hatimaye msamiati wa bwege watua bungeni sasa kutumika rasmi. Futa lugha ya kuudhi; bwege bwege.”


Hata hivyo, wabunge hao wa upinzani hawakushinikiza Dk Tulia kufuta kauliz yake, lakini baadaye wakiwa nje ya ukumbi waliponda kitendo hicho cha kiongozi huyo wa Bunge ambaye aligombea uspika kwa tiketi ya CCM kabla ya kujitoa na muda mfupi baadaye kuteuliwa na Rais Magufuli kuwa mbunge na hivyo kupata sifa ya kugombea nafasi hiyo ya naibu spika.


Dk Ackson aliamsha tafrani hiyo saa 5:48 asubuhi baada ya Bungara, ambaye ni maarufu kwa jina la Bwege, kusimama bila kufuata kanuni za Bunge, kupinga maelezo ya Waziri wa Habari, Nape Nnauye juu ya uamuzi wa Serikali kusitisha shughuli za Bunge kurushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni nchini.


“Na wewe Mheshimiwa Bwege, hebu kaa chini. Usionyeshe ubwege wako hapa,”alisema Dk Ackson kumzuia mbunge huyo asiendelee kuzungumza wakati mjadala ukianza kuwa mkali.


Mjadala huo uliendelea bila ya wapinzani kuhamaki, lakini baada ya Nape kutoa taarifa akieleza kuwa uamuzi wa kuanzisha studio za Bunge ulifanywa na Bunge la Kumi ambalo yeye hakuwamo, ndipo wapinzani walipokumbusha kauli hiyo ya naibu spika

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo April 29 2016 kwenye,Habari zaUdaku, Kitaifa,kimataifa na michezo.


   April 29 2016 naanza kwa kukuletea habari zote kubwa zilizobebwa kwenye Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye ,habari za kitaifa,kimataifa Michezo na udaku na stori nyingine kali ili ujue kilichojiri duniani.. usiache kukaa karibu kwenye kurasa zetu za mitandao...
 

Gallery

Popular Posts

About Us