KINGAZI BLOG: 07/24/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, July 24, 2016

JINSI YA KUOMBA KOZI MBALIMBALI ZA CHETI &DIPLOMA THROUGH NACTE 2016/2017

The System allows you to apply for Admission into Further and Higher Education for academic year 2016/2017.
Available Application Categories:- 

  • - Admission into Certificate/Diploma and Higher Diploma
    • Administration, Business, Law, Planning, Social Work, Community Development, Tourism and related Programmes :-Deadline 05/08/2016
    • Agriculture, Livestock, Engineering, ICT and other related Sciences :- Deadline 05/08/2016
    • Health and Allied Sciences (Including Community Health, Health Records etc) :- Deadline 05/08/2016
    • Teacher Education :- Deadline 05/08/2016

IMPORTANT NOTES:
You are advised to select your most preferred category according to prior qualifications that you hold, because your selection depends on your choices and qualifications.
To proceed with the this application you must have the following 
  • 1. Valid and Working Email Address
  • 2. Valid Phone Number
  • 3. Payment Mpesa Confirmation Code
Read Guide Book:
To know exactly requirement of programmes you wish to apply, it is highly recommended to carefully read admission guidebook. Click here to download.

APPLICATION FEE (Non refundable): Application fee for this academic year are as in following categories:- 
  • - For Certificate/Diploma And Higher Diploma in
    • Administration, Business, Law, Planning, Social Work, Community Development, Tourism and related Programmesalone :- TShs 20,000/=
    • Agriculture, Livestock, Engineering, ICT and other related Sciences alone :- TShs 20,000/=
    • Health and Allied Sciences (Including Community Health, Health Records etc) alone :- TShs 30,000/=
    • Teacher Education alone :- TShs 20,000/=
    • NOTE: For More than one professional area e.g Teacher Education and Agriculture, Livestock, Engineering, ICT and other related Sciences professional areas shall be TShs 30,000/=
Which shall be paid through M-PESA or Airtel Money using the following menu:- Note: Payment Instructions: Please follow the steps below to pay through M-Pesa or Airtel Money:
Payment Instructions Using Vodacom Mpesa:Malekezo ya Jinsi ya kulipia kwa Vodacom Mpesa:
  • 1. Dial *150*00#
  • 2. Select 4. Payments
  • 3. Select 4. Enter business number
  • 4. Enter the business number (607070)
  • 5. Enter reference No. (1234)
  • 6. Enter Amount (e.g 50,000/=)
  • 7. Enter PIN
  • 8. Press 1 to Confirm:
  • 1. Piga *150*00#
  • 2. Chagua 4. LIPA kwa M-Pesa
  • 3. Chagua 4. Weka namba ya kampuni
  • 4. Tafadhali weka namba ya kampuni No. (607070
  • 5. Weka namba ya kumbukumbu ya malipo No. (1234)
  • 6. Weka kiasi (e.g.50,000/=)
  • 7. Weka namba ya siri.
  • 8. Bonyeza 1 kuthibitisha:
After confirmation you will receive a message from Vodacom (e.g. "BA54KP432 Confirmed. Tshs. 50,000 sent to business NACTE for account 1234 on 14/4/14 at 2:33 PM New M-Pesa balance is Tsh 200"). 
*Use the confirmation code at the beginning of the message to enter on payment details text box (BA54KP432).

Baada ya kutuma utapokeo ujumbe kutoka vodacom (Mfano "CB02AK669 Imethibitishwa. Tsh. 20,000 imetumwa kwa NACTE kwenye akaunti namba 1234 tarehe 29/3/16 saa 12:38 PM salio lako la M-PESA ni Tsh. 200"). 
*Tumia Uthibitisho wa malipo mwanzoni mwa ujumbe mfupi ulutumwa kutoka vodacom kuingiza kwenye kiboxi cha uthibitisho wa malipo (CB02AK669).

Payment Instructions Using Airtel Money:Malekezo ya Jinsi ya kulipia kwa Airtel Money:
  • 1. Dial *150*60#
  • 2. Select 5. Make Payments
  • 3. Select 3. Enter business Name
  • 4. Enter the business Name (607070)
  • 5. Enter Amount (e.g 50,000/=)
  • 6. Enter the reference Number. (1234)
  • 7. Enter PIN to confirm Paying 607070
    TShs 50000 with reference number 1234
  • 1. Piga *150*60#
  • 2. Chagua 5. Lipia Bili
  • 3. Chagua 3. Weka Jina la Kampuni
  • 4. Tafadhali Andika Jina La Biashara. (607070
  • 5. Ingiza Kiasi cha Pesa (e.g.50,000/=)
  • 6. Ingiza Namba ya kumbukumbu. (1234)
  • 7. Ingiza namba ya siri kulipia 607070,
    Tshs 50000 kumbukumbu rejea namba 1234.
You will receive a message from Airtel (e.g. " Txn Id:MP160506.0908.A07884 You have paid 50000.00Tshs to NACTE: Your available Airtel Money balance 200.00Tshs."). 
*Use the Txn Id: (MP160506.0908.A07884,) to enter on payment details text box.

Baada ya kutuma utapokeo ujumbe kutoka Airtel (Mfano "Kitambulisho rejea: MP160506.0908.A07884, Umelipa 50000.00Tshs Kwenda NACTE.Salio lako jipya ni 200.00TShs."). 
*Tumia Kitambulisho rejea: wa malipo (MP160506.0908.A07884) mwanzoni mwa ujumbe mfupi ulutumwa kutoka Airtel kuingiza kwenye kiboxi cha uthibitisho wa malipo.

NB: All applicants are advised to keep in safe place their confirmation number from Vodacom M-PESA payment or Txn Id from Airtel Money for future reference. Applicants are advised to read carefully the admission requirements of each programme they anticipate to apply in the guidebook before finalizing the application process in order to avoid problems that may arise due to failure to follow appropriate instructions.

REGISTRATION: To apply for mentioned category you must be registered to CAS follow the below link to proceed.


  • If this is your first time click here to start your application.
  • If you are already registered please click here 

Mchungaji Feki na Waombewaji wawekwa Mikononi mwa Polisi DSM

Anayejiita mchungaji David Mwamkinga amejikuta mikononi mwa polisi jijini Dar es Salaam baada ya ndugu wa baadhi ya wafuasi wa mchungaji huyo kuamua kuwatoa ndugu zao waliofungiwa ndani kwa zaidi ya miaka 10 , kwa lengo la kufanyiwa maombi kutokana na maradhi yanawasumbua.

Hatua hiyo inafuatia kilichoelezewa kuwa ni kuzidi kudhoofika kwa hali za waombewaji hao ambapo jeshi la polisi limeingilia kati na kufanikiwa kumkamata mchungaji huyo pamoja na wafuasi wake eneo la Magomeni Kagera na kuelekea nao kituoni.

credit

 MUUNGWANA BLOG

MAFANIKIO YA RAIS MAGUFULI KATIKA KIPINDI CHA MIEZI 8 ILIYOPITA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAREHE 23/06/2016

UTAFITI 

MIEZI 8 TOKA MHE RAIS JOHN MAGUFULI AMECHAGULIWA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Ndugu waandishi wa habari habari za leo na pole kwa majukumu mazito ya ujenzi wa Taifa. Taarifa yetu itajikita katika maeneo makuu mawili, Mkutano Mkuu wa CCM na UTAFITI wa Miezi 8 ya Mhe Rais John Magufuli.

Taasisi ya CZI ni taasisi huru isiyo ya kiserikali ambayo inajihusisha na ushauri wa mambo ya HABARI na kijamii, pamoja na tafiti mbalimbali. Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, tulizunguka nchi nzima na kuuliza wananchi maswali ya papo kwa papo, ama kwa njia ya simu ama kwa kuhoji kimakundi kulingana na umri wa wahusika.

Tulihoji Watanzania 2,3oo wa kada mbalimbali katika maeneo kadha wa kadha tuliyotembelea kuanzia umri wa miaka 14 hadi 18 na kuanzia wenye umri wa miaka 18 hadi 30 na kuanzia miaka 30 hadi 60.

KUNDI LA 1 UMRI MIAKA 14-18

Kundi hili baada ya kuhojiwa wanaamini Rais John Magufuli ataleta mageuzi makubwa ya kiuchumi, na atarejesha nidhamu ya masomo shuleni kuanzia shule za awali, msingi nasekondari kwa vijana wenye umri kuanzia miaka 7 hadi 18.

Asilimia 78 ya vijana hao kwenye ngazi ya elimu ya msingi na sekondari wanaamini Mhe Rais Magufuli atasaidia kuleta mageuzi kwenye elimu ikiwa ni pamoja na kuondoa tatizo la madawati, mitaala na nidhamu ya walimu, huku asilimia 22 ya vijana hao wakisema Mhe Rais huenda asifanikiwe kwenye harakati zake za mageuzi kwenye sekta ya elimu. Pia kundi hili linaamini kuondolewa kwa michezo shuleni kutazidi kudidimiza maendeleo ya michezo nchini.


KUNDI LA II UMRI MIAKA 18-30.

Watanzania kuanzia miaka 18-30, asilimia 82 wanaamini serikali ya Rais Magufuli italeta mageuzi kwenye elimu hususan kwenye mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu pamoja na kumaliza tatizo la mabweni ya kulala wanafunzi wa vyuo vikuu. Pia kada hiyo inaamini rais anaweza kupunguza tatizo la ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu pamoja na vijana nchini Tanzania. Sababu kuu ambayo inawafanya waseme hayo inatokana na kupambana na wafanyakazi hewa katika taasisi za serikali ambazo zimekuwa zikichangia kukosekana kwa ajira kwa vijana. Lakini sababu nyingine ya kuongezeka kwa ajira ni msimamo wa serikali wa kufufua na kuanzisha viwanda vipya, hasa vya mazao ya kilimo ili kuongeza mnyororo wa thamani kwa mazao ya kilimo.

Aidha asilimia 18 ya kada hii haiamini kama serikali ya awamu ya tano italeta mageuzi yoyote nchini na wanasema ni kawaida ya serikali kuwapa matumaini wananchi wake lakini mwishoni mambo hubaki vilevile kama awamu zilizopita.

KUNDI LA III UMRI MIAKA 30-60

Watanzania wenye umri wa miaka 30-60 waliohojiwa wanasema kuna uwezekano watumishi wa umma wakarejesha imani kwa serikali kutokana na juhudi za Mhe. Rais anavyopambana na ufisadi na rushwa kwa dhati.

Aidha kada hii asilimia 89.0 wanaamini Mhe Rais atamaliza matatizo ya wazee kwa kuanza kuwalipa posho kwa mwezi lakini pia wanaamini nidhamu ya watumishi itaongezeka miongoni mwa watumishi wa umma pamoja na binafsi kutokana na namna serikali inavyopambana na watumishi hewa na utumbuaji majipu unaoendelea kwenye serikali ya awamu ya tano.

Aidha kada hii inaamini umoja na mshikamano wa Watanzania utaendelea kuimarika na moyo wa kusaidiana kwa wananchi wa Tanzania utadumu na kuimarika pia.

Vile vile kada hii inasema Rais Magufuli anazidi kuwa maarufu huku wapinzani wakionekana kupoteza umaarufu kutokana na kushindwa kubuni mbinu mpya ya mapambano ya kisiasa.

Asilimia 11 ya kada hii inaamini serikali ya awamu ya tano haitaleta mageuzi yoyote kwa wazee na nidhamu kwa watumishi wa umma haitabadilika kutokana na aina ya viongozi wanaowasimamia watumishi hao ambao wengi wao siyo waadilifu na siyo watendaji na wafuatiliaji wa mambo kwenye maeneo yao ya kazi.

Kwa ujumla wake mhe rais anakubalika kwa asilimia 89% huku akiwa amewapiku Edward Lowasa na Mhe Jakaya KIkwete ambao wao wamegawana zilizobaki. Jakaya Kikwete akiwa na asilimia 7% huku Edward Lowasa akiwa na asilimia 4%.

Mikoa ambayo tulikwenda ni Dodoma, Mara, Geita, Ruvuma, Arusha, Manyara, Kusini Pemba, Wete Pemba, Kaskazini Unguja, Tabora, Kigoma, Pwani, Morogoro, Simiyu, na Tanga, na kuhoji wananchi takriban 2,300.


MAFANIKIO YA MIEZI NANE (8) YA UTAWALA WA RAIS DK. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI 

Mara tu baada ya kutangazwa mshindi hata kabla ya kuapishwa Novemba 5, 2015 watu wengi walibeza kama angeweza kutekeleza yale aliyoyasema. Wapo waliosema kwamba asingeweza kupambana na rushwa na ufisadi kwa sababu mfumo huo umeanzia ndani ya CCM. Walizungumzia kuhusu suala la kufumua mfumo wa uendeshaji wa Serikali, kuijenga upya CCM, pamoja na namna ya kushirikiana na upinzani. Wengine wakahoji muundo wa baraza la mawaziri utakavyokuwa hasa kwa vile lililopita lilikuwa kubwa mno.

Hata hivyo, katika kipindi cha miezi nane tu, amefanya mambo makubwa mengi kana kwamba amekuwepo madarakani kwa muda mrefu na kwa kiasi kikubwa hata ahadi zake nyingi amekwishazitekeleza na nyingine anaendelea kuzitekeleza. Tutajaribu kukumbusha machache kati ya mengi aliyoyafanya katika kipindi hicho.

Alielekeza Shs. 225 milioni zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla ya pongezi za Wabunge Dodoma kutumika kununua vitanda vya hospitali ya Muhimbili na Shs. 15 milioni tu ndio zitumike kwa ajili ya sherehe hiyo.


1. MPANGO MAHUSUSI WA KURUDISHA NIDHAMU KATIKA UTUMISHI WA UMMA (UTUMBUAJI MAJIPU)


Kurudisha nidhamu kwa watumishi wa umma ilikuwa moja ya agenda zake na ahadi aliyoirudia Zaidi ya mara 100 wakati wa kampeni zake na hata sasa bado anaendelea kusema. Watanzania wamekuwa na kilio cha muda mrefu kwamba wamekuwa wakishindwa kupatiwa huduma muhimu na watendaji wa serikali, ambao wengi wao hawatekelezi wajibu wao ipasavyo.

Itakumbukwa kwamba, hata kabla hajaunda Baraza lake la Mawaziri, Rais Magufuli alifanya mambo makubwa kadhaa ambayo hayakutegemewa. Kwanza alifanya ziara mbili kubwa za kushtukiza ambapo Novemba 6, 2015 ikiwa ni siku moja tu baada ya kuapishwa alitembea kwa miguu kutoka Ikulu hadi Wizara ya Fedha ambako alipita katika ofisi moja baada ya nyingine na baadaye alifanya kikao na watendaji. Novemba 9 alifanya ziara nyingine ya kushtukiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alivunja Bodi ya Wakurugenzi, alimwondoa Kaimu Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dk. Hussein Kidanto na kuamuru mashine muhimu za vipimo za CT-Scan na MRI kutengenezwa haraka huku akitoa sehemu ya mshahara wake kumlipia mgonjwa mmoja aliyekuwa anahitaji kufanyiwa kipimo cha CT-Scan.

Ni katika kipindi hicho ambapo Serikali, katika zile zile ziara za kushtukiza zilizofanywa na Rais mwenyewe na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Watanzania walishuhudia vigogo wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiswekwa ndani, kusimamishwa, kutenguliwa teuzi zao na wengine kufikishwa mahakamani kwa makossa mbalimbali, yakiwemo uzembe, rushwa na ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka. Tumeona watendaji wa mamlaka nyingi za umma wakiendelea kusimamishwa/kufukuzwa kazi kama Kamishna Mkuu wa TRA, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, UHAMIAJI na TRL. Hii imerudisha nidhamu kwa watumishi wa UMMA na kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.


2. MPANGO WA KUBANA MATUMIZI

Itakumbukwa kwamba, Rais Magufuli alipunguza kupunguza sherehe na dhifa za kitaifa na Jumatatu ya Novemba 23, 2015, alitangaza kufutwa kwa Sherehe za Uhuru Desemba 9 na kuagiza fedha za maandalizi ya sikukuu hiyo zitumike kutatua matatizo mengine, ikiwemo kufanya upanuzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge huku akiagiza siku hiyo itumike kusafisha mazingira ili kupunguza matatizo ya kipindupindu nchini. Alifuta sherehe za Muungano na kuelekeza kwamba fedha hizo zitumike kupanua barabara ya kutoka Uwanja wa Ndege jijini Mwanza hadi mjini. Aliagiza pia taasisi hizo zifanye vikao vyao katika kumbi maalum za idara zao badala ya kwenda mikoani ama kukodi kumbi za hoteli huku watu akijilipa posho nyingi wakati vikao hivyo ni vya kiutendaji tu.

Tumeshuhudia katika uteuzi wa viongozi wa serikali ya Awamu ya 5, Mh. Rais amezuia shamlashamla za kupongezana viongozi wa serikali wanapoteuliwa na kufanya uteuzi wa serikali ya awamu ya Tano kutumia bajeti ndogo katika siku hizo za uteuzi. Mfano, uteuzi wa Wakuu wa wilaya, Mawaziri na wakuu wa Mikoa hakukuwa na shamlashamla kama ilivyozoeleka katika awamu zilizopita.

Hili limesaidia kuokoa fedha nyingi ambazo zimekwenda kufanya shughuli za maendeleo ya wananchi. Wale waliodhani kwamba utendaji wa Dk. Magufuli ni mfumo wa kujilundikia majukumu bila utekelezaji (Slack Management Style) walikosea sana, kwa sababu tangu wakati ule tumeshuhudia watendaji wengi wazembe, wala rushwa na mafisadi wakiwajibishwa huku wengine wakifikishwa mahakamani.

3. WATUMISHI HEWA

Suala la kuwepo kwa watumishi hewa, ambalo lilikuwa linalalamikiwa kwa muda mrefu, safari hii Rais Magufuli alilitumbua ambapo tulishuhudia kwamba kumbe kulikuwa na watumishi hewa zaidi ya 12,000 waliokuwa wanalipwa mabilioni ya fedha ambazo ziliingia kwa maofisa wajanja. Kuonyesha kwamba hakuwa na mzaha hata kidogo, alimfuta kazi mara moja Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga baada ya kugundua kwamba alimdanganya kwamba mkoa wake haukuwa na mtumishi hewa hata mmoja wakati haikuwa hivyo. Mabilioni mengi ya fedha yameokolewa kutokana na zoezi hilo katika Serikali za Mitaa.

4. SAFARI ZA NJE KWA WATUMISHI WA UMMA NA VIONGOZI WA KISERIKALI

Rais Magufuli alianza mara moja kwa kutangaza kufuta safari zote za nje za mafunzo na ziara kwa maofisa na watendaji wa Serikali katika harakati za kubana matumizi huku akibainisha kwamba, safari hizo zililigharimu Taifa mabilioni ya fedha wakati nyingi hazikuwa na tija. Akasema yeyote ambaye alitaka kusafiri ilikuwa lazima apate kibali maalum kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi au kwake yeye. Siyo siri kwamba hili limeondoa zile ‘safari za kufanya shopping’ ambazo maofisa wengi wa serikali walizitumia kutafuna fedha za umma na kuitia doa Serikali ya CCM.

Uamuzi wa Mh. Rais kurudisha utaratibu wa vibali vya kwenda nje, umeokoa pesa nyingi sana ambazo zilikuwa zinatumika na viongozi mbalimbali wa serikali kusafiri kwenda nchi za nje safari ambazo zilikuwa hazina tija kwa taifa. Kwa kulitekeleza hili hata yeye mwenyewe katika kipindi cha miezi 8 ya utawala amesafiri mara 2 tu, kwenda Rwanda na Uganda. Huu ni mfano ambao unatakiwa kuigwa na kuungwa mkono na watanzania wote walio na dhamana katika sekata ya umma.

5. ELIMU BURE (CHEKECHEA MPAKA KIDATO CHA NNE)

Katika kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015, ameweza kupeleka TShs bilioni 18 kwa ajili ya kutekeleza mpango huo wa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari. Hivi sasa tunashuhudia idadi kubwa ya udahili wa wanafunzi wa shule za msingi na kuongeza idadi kubwa ya uhitaji wa madawati hasa kwa shule za msingi. Wazazi wengi wameitikia na kuamua kupeleka watoto wao shuleni haya ni matokeo ya Utekelezaji wa Sera ya Elimu bure katika ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015.


6. PUNGUZO LA KODI KWA WAFANYAKAZI (PAYE) UKUSANYAJI WA MAPATO

Serikali makini hukusanya kodi! Rais Magufuli katika kipindi kifupi tu ameweza kusimamia vyema ukusanyaji wa kodi akianza kwa kuwabana wafanyabiashara wakubwa ambao walikuwa wakwepaji sugu. Lakini pia Serikali imeweza kupunguza kiasi cha kodi ya PAYE kwa 2% katika mishahara ya wafanyakazi kila mwezi na kuondoa makali ya kodi kwa wafanyakazi wake.

7. VITA DHIDI YA MAFISADI

Mh. Rais pia ameweza kuanzisha mahakama ya mafisadi kwa lengo la kupambana na mafisadi ambao wamelifikisha taifa la Tanzania kwa wizi mkubwa wa mali za umma pamoja na matumizi mabaya ya fedha za serikali. Hili alilisema katika kampeni na amelitekeleza kwa asilimia 80 akionyesha dhamira yake ya kushughukia watu wa namna hiyo.

Katika sherehe za kuanza mwaka wa kimahakama Mh. Rais aliweza kuahidi na kutoa jumla ya Tshs Bilion 12 ili kuharakisha utendaji wa mahakama jambo ambalo halijawahi kufanyika na kila mwaka awamu zilizopita bajeti haitoshelezi kwa muhimili huu. Fedha hizo zilikabidhiwa kwa Idara hiyo mwezi Februari 2016.

Ajabu ni kwamba, kasi ya kuwawajibisha watumishi wa umma ikaanza kupingwa na baadhi ya wapinzani, hususan wale ambao walikuwa wanaahidi kwenye kamepni zao kwamba wangeweza kupambana na ufisadi! Siyo siri kwamba, tayari kasi yake hiyo ilikuwa imewapoteza wapinzani hata kabla hajaunda baraza la mawaziri – wakati huo akiwa na wasaidizi watatu tu – Katibu Mkuu Kiongozi, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu!


8. UJENZI WA MABWENI KWA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

Mh. Rais amehaidi kujenga mabweni kwa ajili ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam jambo ambalo lilipigiwa kelele sana na wanafunzi katika awamu zilizopita lakini leo litafanyika kupitia Mh. Rais wa awamu ya Tano kama alivyo ahidi.

Yako mengi sana aliyoyatekeleza ambayo hayawezi kutosha hapa, lakini Rais Magufuli, ambaye kimsingi ameisongesha mbele Tanzania katika kipindi kifupi, anaweza kufanya mambo makubwa zaidi hasa atakapokabidhiwa uenyekiti wa taifa wa CCM, chama tawala na kikongwe kabisa barani Afrika, kwa sababu huko nako ataondoa mfumo mbovu wa uongozi unaokifanya chama hicho kilalamikiwe na kiwe agenda kuu ya wapinzani kila mara.

Wale wanaobeza utendaji wake wanapaswa kukaa kimya, kwani Wananchi waliomweka madarakani ndio watakaompima na kumhukumu, kwa sababu hakuna aliyetegemea kama serikali hii ingeweza kuondoa Service Charge kwenye umeme wa majumbani ambapo wananchi walikuwa wanaumizwa sana na hili jambo.

Mwenye nia njema na maendeleo ya taifa hili, anapaswa kuiunga mkono kwa dhati kabisa serikali ya Dk. Magufuli kwa utendaji huu na siyo kumhujumu, kumbeza ama kutoka visingizio vyovyote vile.



KUELEKEA MKUTANO MKUU WA CCM TAIFA JULAI 23 MWAKA HUU.

Ndugu zangu Watanzania, wakati wanachama wa CCM wakijiandaa na Mkutano Mkuu wa chama hicho kikiwa na ajenda moja tu kumkabidhi Rais John Magufuli uenyekiti wa CCM, wanachama wa chama hicho wanapaswa kutambua mambo kadhaa ambayo yanampa umuhimu wa kipekee Rais Magufuli kupewa nafasi hiyo na wajumbe wa mkutano mkuu, pamoja na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.

Chama cha Mapinduzi kina rasilimali nyingi:

1. Rasilimali watu

2. Rasilimali Ardhi, Majengo na Viwanja

3. Wananzuoni wa kila taaluma

4. Wafanyabiashara ndogondogo (machinga)

5. Wafanyabiashara wa kati na wakubwa

6. Wanachama wake wanaozidi milioni 9

7. Mashabiki wake wanaozidi milioni 28.9

8. Wakulima

9. Wavuvi

10. Wafugaji nk.

Lakini pamoja na utajiri huo, bado chama hicho hakiwezi kujiendesha na wanategemea Ruzuku kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, pamoja na wafadhili ambao wengine siyo wasafi kwenye rekodi za kodi.

Ndugu waandishi wa habari, baada ya kutafakari kwa kina tumegundua kwamba, Mhe Rais Magufuli anazo agenda nzuri za kukiendeleza chama hicho kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo pindi atakapopewa chama hicho.

Agenda hizo ni:

Mosi: Kuhakikisha chama kinajitegemea kwa kuanzisha miradi ya maendeleo ambayo itakifanya kijiendeshe chenyewe bila kutegemea wafadhili.

Pili: Miradi ambayo ipo tayari ijulikane na iwekwe wazi na iwanufaishe wanachama na wananchi kwa ujumla.

Tatu: Kuongeza wanachama zaidi wa chama hicho.

Nne: Kuwa na wanachama wanaokipenda chama hicho na wenye uzalendo na chama hicho na nchi yao.

Ndugu waandishi wa habari, kwa mtazamo huo tunawaomba wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, pamoja na wajumbe wa Mkutano Mkuu waone umuhimu wa kumpa Mhe Rais Magufuli kura za kutosha ili awe mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi.

Aidha, kuna taarifa za baadhi wa wanaCCM wachache ambao wamekuwa wanazunguka mikoani na wilayani wakieneza taarifa za uongo kwamba Rais Magufuli mwenyewe ndiye hataki kuwa mwenyekiti wa chama.

Ndugu wananchi na waandishi wa habari, tunawaonya hao wanaoeneza uongo huo waache mara moja kwa kuwa uongo na uzushi huo haulengi kukijenga chama na watu hao huenda wakajikuta kwenye wakati mgumu kama wataendelea kuzusha na kueneza uongo huo.

Tunawaomba Watanzania wazidi kumuombea rais wetu kwa kuwa anaonyesha nia ya dhati kuhakikisha nchi inapata maendeleo, kwani hata wakati aliposhiriki jubilee ya miaka 50 ya Benki Kuu ya Tanzania alisikika akiwataka benki kuu kuhakikisha wanalinda thamani ya shilingi pamoja na kushusha mfumko wa bei.

Kama mnavyojua, moja ya matatizo makubwa kwa watanzania hasa wa kipato cha chini ni mfumko wa bei ambao umekuwa unawatesa kila mwaka bila serikali kutafuta njia mbadala za kupunguza mfumko huo, lakini rais wa awamu ya tano Mhe Magufuli na serikali yake wanapambana kuondoa kero hiyo kubwa kwa Watanzania.

Tudumishe umoja, mshikamano na Amani. Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania!


Imeandaliwa na:

David Saire Manoti-Mwanasiasa Kijana

Raphael Nyang’i Awino- Mwanasiasa kijana

Cyprian Musiba Nyamagambile- Mwandishi/Mtafiti

Dotto omary Nyirenda - Mwanadiplomasia kijana

Daniel Mahelela - Mtafiti

Juma George Chikawe-Mwanasheria

Sumaye,Lowassa,na Gwajima wachambuliwa Dodoma


VIGOGO mashuhuri wa Chadema waliowahi kuwa mawaziri wakuu; Edward Lowassa na Frederick Sumaye, jana waligeuka gumzo ndani ya Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kumchagua Rais John Magufuli, kuwa Mwenyekiti wa tano wa chama hicho.

Gumzo hilo, lilianzishwa na Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba, alimpomtaka Askofu wa Kanisa la Ufufuko na Uzima, Josephat Gwajima, asimpotoshe Magufuli ili yasije yakampata ya Sumaye, ambaye sasa anachezea mchangani Kibaha.

Sumaye mchangani

“Hata akina Sumaye hawakuunda vyama vyao. Bado wanahangaika; na sasa Sumaye anacheza mchangani Kibaha,” alisema Makamba.

Sumaye ambaye aliwahi kuwa mjumbe wa Kamati Kuu na NEC ya CCM, kwa sasa anawania uongozi wa Kanda ya Pwani katika Chadema. Kabla ya kusema kuwa Sumaye anahangaika na siasa za mchangani, Makamba alimtaka Gwajima kuacha uongo na kusingizia viongozi wa CCM.

“Wewe siyo wa kwanza kukataa kazi hii. Hata watangulizi wako Kikwete na Benjamin Mkapa nao walifanya hivyo hivyo,“ alisema Makamba ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).

Makamba alisema hata manabii na mitume wengi, kama Haruni, Mussa, Yona au Yunus na Yeremia walifanya vivyo hivyo, walipopewa utume au unabii na Mungu, kwani waliogopa kufanya kazi hizo lakini, alisema mara zote Mungu aliwaagiza kuwa wasiogope kuwa manabii na mitume, kwani atatia maneno kwenye vinywa vyao.

Aidha, Makamba alitaka viongozi wa dini mfano Askofu Gwajima, waache kumfitini Kikwete eti kwamba alikuwa hataki kumpa uenyekiti Magufuli.

“Mzigo wa chama ulikuwa umebebwa na Mkwere Kikwete ambaye sasa anaondoka; na kwa kuwa kuna msemo kuwa ‘mzigo mzito mpe Mnyamwezi au Msukuma, nawaomba wajumbe wote sasa mzigo wa chama tumpe Msukuma Magufuli,” alisema na kauli yake hiyo ilishangiliwa na wajumbe.

Lowassa na ufisadi

Akielezea aina ya kiongozi anayetoka CCM na anayeingia, Makamba alisema kuwa anayetoka, Kikwete ni mpiganaji wa ufisadi, kwa kuwa alifikia hatua ya kumtosa rafiki yake Edward Lowassa, kuwa hafai kuwa Rais kwa kuwa anatuhumiwa kwa ufisadi.

Alisema kada wa chama hicho anayeingia baada ya Kikwete, Dk Magufuli yeye ndiye muasisi wa Mahakama ya Mafisadi, ambayo tayari imeshaanzishwa kwa Sheria ya Bunge. Kwa mujibu wa Makamba, Kikwete ni kiongozi aliyepiga vita umasikini na anapoondoka, anayeingia Dk Magufuli msimamo wake ni asiyefanya kazi na asile.

Kumchinja Kobe

Naye mmoja wa vigogo wa Chadema aliyerejea CCM, Fred Mpendazoe, alikuja na dhana ya namna ya kumchinja kobe, akifananisha na utaratibu uliotumika, kukata jina la Lowassa katika majina 38 ya wagombea urais.

Mpendazoe alisema Kikwete alifanya ‘timing’ sana kushughulikia ufisadi ndani ya chama hicho, kwa kuwa kati ya makada hao 38 waliokuwa wakiwania urais, baadhi akiwemo Lowassa walikuwa na tuhuma za ufisadi na kukatwa kwa majina yao, kulifanyika kwa wakati sahihi.

Gia angani

Mpendazoe alisema anashangaa kusikia Magufuli anabana demokrasia na kuhoji kati ya chama kilichotangaza nafasi ya urais na kuruhusu wagombea 38 kugombea, huku mchujo ukifanyika hadharani na kilichompata mgombea kwenye chopa (helikopta), ni kipi chenye demokrasia?

Akifafanua zaidi, Mpendazoe alisema Chadema ilimpata mgombea wake angani ndani ya helikopta, na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe alipokwenda katika vikao, akasema chama hicho kimebadilisha gia angani.

CCM B

Naye Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema alihoji yeye kuitwa CCM B, baada ya Rais Magufuli kumteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole na kusema inakuwaje yeye aliyetoka katika chama hicho mwaka 1995, apewe jina hilo.

Alisema kama kupewa cheo na Magufuli, ndio sababu ya kuitwa CCM B, basi hata Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi na Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, ni CCM B kwa kuwa aliteuliwa kuwa Mbunge na Rais Jakaya Kikwete.

Mrema alisema kama kuitwa kwake CCM B ni kutokana na kutoka ndani ya CCM; basi Lowassa na Sumaye ni CCM A, kwa kuwa wao wametoka mwaka jana wakati yeye ametoka tangu 1995.

Haeleweki

Naye Magufuli alisema alimshangaa Rais mstaafu Benjamini Mkapa, kwa kumteua mtu mmoja kuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 mfululizo, wakati waliofanyakazi na Waziri Mkuu huyo, akiwamo yeye waliona kuwa ni mtu asiyeeleweka. Waziri Mkuu wa Mkapa, alikuwa Frederick Sumaye.

credit-habari leo

Alichokiandika Zitto Kabwe baada ya Rais Magufuli kupewa uenyekiti wa CCM

Jana July 23 2016  Rais John Pombe Magufuli alikabidhiwa rasmi nafasi ya uenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM   baada ya kupigiwa kura za ndio 2398  kutoka kwa wanachama wa chama hicho ambapo hakuna kura hata moja ya hapana wala iliyoharibika

Baadhi ya viongozi wakiwemo wa vyama vya upinzania walishiri akiwemo mwenyekiti wa TLP Augustino Mrema, lakini wapo pia waliotamani kufikisha hisia zao kuhusu tukio hilo na mmojawapo ni mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe kupitia account yake ya facebook aliandika maneno haya…

"Napenda kumpongeza Rais John Magufuli kwa kuchaguliwa kwake kuwa Kiongozi wa Chama chake cha CCM akiwa Mwenyekiti wa Tano chama hicho. CCM imeendelea kudumisha utamaduni wa kukabidhiana Uongozi kila baada ya muda

"Jambo ambalo ni la kujifunza hasa kwa vyama vya Siasa nchini na barani Afrika. Nataraji kwamba Rais na Mwenyekiti mpya wa CCM ataona umuhimu wa Vyama vya Siasa kuendelea kufanya Siasa bila vikwazo na kwa mujibu wa Sheria za Nchi yetu.

"Demokrasia inaimarisha Amani kwa kupaza sauti za HAKI. Karibu kwenye changamoto za kuongoza Vyama vya Siasa ndugu Rais." –Zitto Kabwe

Alichokisema Rais Magufuli Baada ya Kuchaguliwa Kuwa Mwenyekiti wa CCM

MWENYEKITI wa tano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais John Magufuli, amewaomba wanachama wa chama hicho kumuombea kwa Mungu ili apate uvumilivu wa mtangulizi wake, Mwenyekiti mstaafu, Jakaya Kikwete.

“Mzee Kikwete wewe una moyo wa uvumilivu. Sina hakika kama mimi ninao uvumilivu kama wako...umetupa fundisho kubwa sana,” alisema Magufuli wakati akizungumza kwa mara ya kwanza baada ya kuchaguliwa kwa kura asilimia 100 kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.

Katika kuonesha tofauti yake na Kikwete katika uvumilivu, Magufuli alikumbusha changamoto aliyokutana nayo Kikwete, wakati alipoingia katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM mwaka jana, kupeleka mapendekezo ya majina ya wagombea watano wa urais waliokuwa wamepitishwa na kikao cha Kamati Kuu, ili wapigiwe kura.

Ndani ya kikao hicho wakati Kikwete, wajumbe wa Kamati Kuu na wa Baraza la Wazee la Ushauri wakiingia, baadhi ya wajumbe wa kikao hicho walikiuka utaratibu wa siku zote wa chama hicho, kwa kuimba kuwa na imani na mmoja wa wagombea wa urais, Edward Lowassa, ambaye jina lake lilikatwa katika kikao cha Kamati Kuu.

Kupotezwa  

“Siku ile umeingia ukumbini, watu wakawa wanaimba kuwa wana imani na mtu mwingine, siku hiyo hiyo robo au nusu yao wangepotea...sifahamu, umetoa fundisho kwa sisi vijana kwamba saa nyingine uvumilivu ni kitu muhimu,” alisema akimaanisha kama hali hiyo ingemkuta yeye ndiye Mwenyekiti, hayo ndiyo yangetokea.

Kutokana na uvumilivu aliouonesha Kikwete katika mkutano huo, Magufuli aliwataka wanachama hao wa CCM kumuombea kwa Mungu, ili apate angalau nusu ya uvumilivu wa Kikwete, ili katika uongozi wake mambo yaende salama.

Kuzushiwa JK

Alimsifu Kikwete kwa kutumia hekima ya uvumilivu, kwa kuwa kiongozi huyo mstaafu, amesemwa mambo mengi, akazushiwa na hata kutukanwa kutokana na hatua, uamuzi na vitendo vyake Magufuli.

“Umesemwa mengi, umetukanwa mengi na umezushiwa mengi kwa ajili yangu, lakini kwa upendo wako na kwa kumtegemea Mungu, ukakaa kimya...sina cha kukulipa, bali nitafanyia kazi Watanzania na hasa wana CCM kwa nguvu zote,” alisema Dk Magufuli.

Alitoa mfano wa Kikwete kuzushiwa alikuwa akikataa kumkabidhi Dk Magufuli uenyekiti wa CCM kwa kufuata desturi ya chama hicho, akasema Mwenyekiti huyo mstaafu amemshawishi mara nne, lakini yeye ndiye aliyekuwa akikataa.

“Nakumbuka umeniambia mara nne, ya kwanza ulikuja kuniambia nikakukatalia bosi wangu, ulinipigia simu na mimi nikawa naanzisha mjadala mwingine. Nakupa pole na unisamehe sana kwa kuwa kukukatalia kulisababisha utukanwe,”alisema Rais Magufuli.

Serikali Dodoma

Kabla ya kumaliza hotuba yake, Magufuli alitangaza ahadi kwa wanachama hao, kuwa amebakiza miezi minne na miaka minne kabla ya kumaliza kipindi chake cha miaka mitano na kusema kabla ya kumaliza kipindi hicho, atakuwa amehamishia serikali yote Dodoma.

Magufuli alisema kwa sasa miundombinu ya Dodoma inawezesha serikali kuhamia huko, kwa kuwa barabara za kutoka Makao Makuu hayo ya serikali kwenda sehemu mbalimbali nchini, zinapitika kwa lami.

Mbali na barabara, alisema pia huduma kwa ajili ya maisha ya watu nazo zinapatikana kwa kuwa mkoa huo una uzoefu wa kuhudumia wabunge, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM na mikutano mingine, huku mkoa huo ukiwa na Chuo Kikuu cha Dodoma, ambacho ndio kikubwa kuliko vyote nchini.

Alisema, akihamia yeye katika Ikulu ya Chamwino ambayo alisema ina kila huduma anayohitaji, anatarajia Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, mawaziri na serikali nzima itamfuata.

Babu wa demokrasia

Magufuli alisema CCM ndio chama kilicholea demokrasia hapa nchini na kinaendelea kutoa ulezi huo na kufafanua kuwa chama hicho ndio babu na bibi wa demokrasia; baba na mama wa demokrasia na kaka na dada wa demokrasia kwa vyama vyote nchini.

Alisema kwa kuwa Serikali anayoiongoza inatekeleza Ilani ya chama hicho, hivyo chama hicho ndio mabosi wa mabosi wote serikalini na kuonya kuwa ambaye hataki hilo, ataondolewa.

Kupendekezwa kwake

Awali wajumbe wa Mkutano huo Mkuu Maalumu wa CCM wapatao 2,398 walimpigia kura ya kumchagua Magufuli kuwa Mwenyekiti mpya wa chama hicho.

Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Kikwete ndiye aliyesoma pendekezo la NEC kwa wajumbe wa mkutano huo kuhusu mgombea wa nafasi hiyo.

“Madhumuni ya mkutano huu ni kuchagua mwenyekiti mpya. Sisi katika Halmashauri Kuu tunampendekeza kwenu Mheshimiwa Dakta John Pombe Joseph Magufuli ashike nafasi hiyo,” alisema Kikwete saa 7:10 na kauli yake hiyo kupokelewa kwa shangwe, vifijo na vigelegele.

Akimwelezea Magufuli, Kikwete alisema ana imani isiyo na hata chembe ya shaka kuwa atafanya kazi hiyo vizuri, kwa sababu ya imani na mapenzi yake makubwa kwa chama hicho na Watanzania.

Alisema Magufuli ametumikia Taifa na wananchi kwa miaka mingi kwa uaminifu na uadilifu mkubwa, katika wadhifa mbalimbali aliokuwa nao. Alisema Magufuli amekuwa mbunge na waziri kwa miaka 20, ambapo miaka 10 wakati wa serikali ya Rais Benjamin Mkapa na mingine 10 wakati wa serikali yake.

Alisema pia Magufuli amekuwa mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya na mkoa, mjumbe wa mkutano mkuu wa wilaya na mkoa na mjumbe wa mkutano mkuu wa taifa kwa miaka 20, hivyo anakijua mno chama.

Kikwete alisema Magufuli ameongoza nchi kwa uaminifu na uadilifu mkubwa katika kipindi kifupi cha miezi 8 tangu alipochaguliwa, hivyo sasa anafaa kuvaa kofia zote mbili.

“Kichwa chake sasa kinatosha avae kofia zote mbili - ya urais na uenyekiti wa chama. Nawaomba wajumbe wote tumuunge mkono. 

“Tumpe kura zote za ‘Ndiyo’ na isipotee hata moja,” alisema Kikwete ambaye ameng’atuka baada ya kuongoza Chama tangu Juni 2006. 

“Mimi naondoka na bila shaka yoyote namwachia Chama Cha Mapinduzi Rais Dakta John Pombe Joseph Magufuli. Nakiacha Chama Cha Mapinduzi katika mikono salama na nina hakika kitapata maendeleo makubwa ya haraka,” alisema.

Kura zatangazwa

Kazi ya kupiga kura na kuzihesabu ilipokuwa ikiendelea, viongozi wakuu wa CCM na wastaafu baada ya baadhi yao kupiga kura, waliondoka kwa ajili ya mapumziko.

Baada ya mapumziko, walirejea ambapo baada ya salamu za wageni na baadhi ya wanasiasa waliorejea CCM baada ya kukimbilia upinzani kumalizika, Kikwete alisoma matokeo.

Akitangaza matokeo hayo, Kikwete alisema kura zilizopigwa zilikuwa 2,398, zilizoharibika sifuri na hivyo kura halali zikawa 2,398. 

Kikwete aliendelea kuwa matokeo yameonesha kuwa, kura za Hapana ni sifuri na kura za ndio ni 2,398, na hivyo Magufuli amepitishwa na wajumbe wa CCM kwa nidhamu ya juu ya kumpa asilimia 100 ya kura.

Makamu wenyeviti

Awali, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alisema mkutano mkuu huo usio wa kawaida, unafanyika kwa mujibu wa Kifungu cha 7 (103) (4) cha Katiba ya CCM na ajenda yake ni kumchagua mwenyekiti mpya, kufuatia uamuzi wa Kikwete kung’atuka, akitekeleza utamaduni wa chama kuachiana madaraka, ili kumpisha Rais John Magufuli.

Aidha, alisema kwa mujibu wa Kifungu 7 (105) (5) (a) cha Katiba hiyo, unapofika wakati wa uchaguzi kazi mojawapo ya mkutano mkuu ni kuchagua makamu wenyeviti. 

Lakini, alisisitiza makamu wote wawili wa sasa, muda wao haujamalizika kikatiba na utamalizika mwezi Novemba 2017“Makamu wote wawili hawajamaliza muda wao. Muda wao utamalizika Novemba 2017, hivyo hakuna sababu ya kuwachagua tena. Hapa leo tunachagua mwenyekiti peke yake,”alitangaza Kinana.

Makamu Mwenyekiti wa CCM kwa upande wa Bara ni Phillip Mangula na upande wa Zanzibar ni Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.

Viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Rais wa Zanzibar Dk Shein , mawaziri wakuu wastaafu Mizengo Pinda, Cleopa Msuya, Dk Salim Ahmed Salim, Jaji Joseph Warioba, John Malecela, Makamu wa Rais mstaafu Mohamed Gharib Bilal na makatibu wakuu wastaafu wa CCM, Yusuf Makamba na Wilson Mukama.

Picha 8: Mwigizaji Jackline Wolper atangaza kuhama CHADEMA na kijiunga na CCM

Mwigizaji wa filamu nchini Tanzania Jackline Wolper aliyakuwa akimuunga mkono Edward Lowassa katika uchaguzi Mkuu 2015, ametangaza kujiunga na CCM rasmi jana

Wolper alikaribishwa na mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Jakaya Kikwete baada ya kutangaza kujiunga na CCM.

Kitendo hicho kilifanyika katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM uliofanyika jana Julai 23, mkoani Dodoma.


Magazeti ya Leo Jumapili ya July 24 kwenye headlines za kitaifa,kimataifa,michezo na udaku

 




Tukio la Ujambazi lililofanikiwa zaidi, kusisimua na kuushangaza Ulimwengu

Mwaka 2003 lilitokea tukio kubwa zaidi la ujambazi ambalo labda ndio lililotumia akili na maarifa zaidi pengine kushinda tukio lolote la ujambazi kwa miaka 50 iliyopita.. Tukio hili lilishuhudia wahusika wakitokomea na vitu vyenye thamani ya zaidi ya Bilioni 200 (100 mln USD)!
Uthubutu, ubunifu, akili na maarifa yaliyotumika kutekeleza tukio hili limefanya mpaka kampuni ya utengenezaji filamu ya Paramount Pictures kununua haki za hadithi ya tukio hili ili watengeneze filamu itakayo husu mkasa mzima wa tukio hili..

TUKIO LENYEWE

Mwanzoni mwa mwaka 2000 mfanyabiashara wa madini (almasi) Leonardo Natarbartolo alifungua ofisi mjini Antwerp nchini ubelgiji, mji ambao ndio kituo cha biashara ya madini ya almasi ulimwenguni.. Ofisi yake ilikuwa katikati kabisa ya kitovu cha mitaa ambayo ndio hasa biashara ya almasi hufanyika. Natarbartolo alijihusisha hasa katika manunuzi ya kiwangi cha kawaida cha almasi (small deals) lakini jambo ambalo watu hawakulifahamu ni kwamba walikuwa wamemkaribisha moja kati ya manguli wa wizi wa almasi ulimwenguni!
Kutokana na kujitambulisha kama mfanya biashara mwenzao, Natarbartolo alipata fursa ya kuingia katika Kuba (vault) za wafanyabiashara wengine ili aweze kukagua mali kabla ya kuinunua na aliutumia fursa hii kuyasoma mazingira ya Ofisi hizo zilizo hifadhi madini na kuja kufanya uhalifu kesho yake..
Natarbatolo aliishi hivi mjini Antwerp kwa miezi kadhaa kabla hajakutana na mfanyabiashara ya almasi Myahudi ambaye kukutana kwao kulipelekea kufanikisha tukio ambalo liliushangaza ulimwengu na limeendelea kuushangaza ulimwengu mpaka leo hii..



MAANDALIZI

Mwaka mmoja baada ya Natarbatolo kuingia Antwerp, siku hiyo akiwa kwenye mgahawa akinywa kahawa alifuatwa na Mfanyabiashara wa Kiyahudi ambaye alimuomba wazungumze faragha kuhusu biashara muhimu. Baada ya kukaa nae chemba Myahudi akamueleza amza yake kuwa anataka amshirikishe katika tukio la ujambazi na alimuuliza kama anahisi Vault ya Antwerp Diamond Center inaweza kuibiwa... Natarbartolo akamjibu kwa kifupi kuwa atamjibu swali hilo kama yuko tayari kumlipa dola laki moja! Na Myahudi huyo akakubali

Siku mbili baadae Natarbatolo alielekea ilipo Main Vault ya Antwerp Diamond Center (kumbuka kutokana na yeye kujitanabaisha kama mfanyabiashara ya almasi kwa mwaka mmoja aliokaa Antwerp hivyo alifanikiwa kujisajili ili aweze kuhifadhi almasi zake katika Main Vault ya Antwerp)..
Kitu ambacho watu wote wakiwepo walinzi hawakikugundua ni kwamba katika mfuko wa pembeni wa suti yake aliweka peni ambayo inaonekana kama peni ya kawaida lakini ilikuwa ni peni maalumu iliyokuwa na kamera ndogo ya siri.. Kamera hii ilimsaidia Notarbartolo kurekodi mandhali yote ya ndani ya vault na jinsi ulinzi ulivyo...
Kesho akajutana na yule myahudi na kumpa jibu lake kuwa ni immposible kuvunja na kuiba main vault ya Antwerp inayohifadhi almasi zote zilizopo katika mji huo.. Akampa ile peni ambayo imerekodi mandhali ya Vault pia akampa na maelezo ya mdomo kwanini haiwezekani kuiba katika ile vault na akamsisitiza zaidi juu ya matabaka ya ulinzi (security levels) ambayo yana protect vault hiyo. Matabaka hayo yapo kama ifuatavyo..

1) Combination dial ambayo unatakiwa uingize tarakimu nne za siri

2) Sehemu ya kuingiza funguo maalum

3) Sensor ya mitetemo (seismic sensor)

4) geti la Chuma lililo sambamba na mlangi

5) sensor ya sumaku (magnetic sensor)

6) Kamera ya nje ya mlango

7) Keypad ya kuzima alarm

8) sensor ya mwanga (light sensor)

9) Kamera ya ndani ya vault

10) sensor ya joto na mjongeo (heat & motion sensor)

Jumlisha; walinzi na ulinzi unaozunguka jengo hilo.. Natarbartlo akmsisitizia yule myahudi "..it is immposible to rob the Antwerp diamond center vault"..

TUKIO LILIVYOTEKELEZWA

Miezi kama mitano ikapita ndipo Notarbartolo akapokea simu kutoka kwa yule myahudi na safari hii alimuomba wakutane nje kidogo ya mji wa Antwerp... Baada ya kuonana yule myahudi alimchukua Notarbatolo mpaka kwenye nyumba moja inayofanana na ghala kubwa.. Ndani yake Notarbatolo alikuta kitu ambacho hakutegemea kabisa... Yule myahudi alikuwa ametengeneza replica inayofanana kabisa na main vault halisi ya kuhifadhia almasi ya hapo mjini Antwerp.. Pia akamtambulisha kwa watu watatu ambao pia aliwakuta hapo! Natarbartolo amekataa kabisa mpaka leo hii kutoa majina halisi ya watu hawa lakini anawasimulia kwa nicknames walizokuwa wanatumia, kulikuwa na The genius (huyu ni mtaalamu wa mambo ya kidigitali na eletroniki), kulikuwa na The monster ( huyu alikuwa ni mekanika na mtaalamu wa umeme) na kulikuwa na mzee wa makamo ambaye walimuita The King of Keys (huyu ni mtaalamu wa kufungua vitasa na makufuli ya aina zote pamoja na kufoji funguo)..
Yule myahudi aliwaambia kazi ya ile replica ni wao wafanye mazoezi na kuitafiti na hatimae wajue namna gani wataweza kuingia ndani ya vault ya Antwerp pasipo kugundulika..

Iliwachukua miezi mitano Natarbartolo na wenzake kufanya mazoezi na kutengeneza perfect plan itakayowawezesha kuingia katika vault na kuiba pasipo kugundulika..


SIKU YA TUKIO..

Siku moja kabla ya tukio, yaani February 14 2003 Notarbartolo alienda mchana kwenye vault kana kwamba kuna almasi ameenda kuhifadhi lakini akajitahidi akae karibu na kifaa cha kuhisi joto na mjongeo (heat/motion sensor) na kwa kutumia hair spray aliyoificha ndani ya jaketi lake akapulizia juu ya kifaa hicho hivyo kukifanya kisiwe na uwezo wa kuhisi mabadiliko yoyote ya joto au movement ndani ya vault...

Ilipowadia siku ya tukio lenyewe.. February 15
Notarbartolo na wenzake waliendesha gari mpaka karibu kabisa na jengo lenye vault! Jengo lilikuwa na ulinzi mkali kwa mbele lakini nyuma ya jengo hakukuwa na ulinzi mkubwa kwani watu wa ulinzi walikuwa na imani kubwa sana na teknolojia yao inayosaidia kulinda jengo lao..
Wote wakashuka kwenye gari isipokuwa Notarbatolo alibaki kwenye gari! Baada ya kushuka wote wakazunguka nyuma ya jengo ambako walitumia ngazi ambayo The genius alikuwa ameificha hapo mchana wake wakapanda mpaka ghorofa ya pili.. Baada ya wote kupanda katika balcony ya ghorofa ya pili ilibidi wakae mbali na madirisha kwani yote yalifungwa vifaa vya kuhisi joto na movement na vikigundua tu kuwa kuna mabadiliko ya joto au movement basi alarm inalia..
Alichokifanya The genius alichukua kitambaa kirefu kilichotengenezwa kwa polyester kujifunika na kusogolea kifaa kile cha heat and motion sensor.. Kutokana na yeye kujifunika kwa nguo yenye material ya polyester hii ilipelekea kifaa kile kushindwa kudetect kilichokuwa kinatokea na alipokifikia karibu kifaa kile akakifunika kabisa na nguo ile kwahiyo korido ikawa iko salama kwa wao wote kupita.. Wakafungua madirisha wakaingia ndani na kuanza kushuka ngazi kuelekea chini kwenye vault..

Baada ya kufika chini nje ya mlango wa vault ambako kulikuwa na giza kutokana na kuzimwa taa.. Wakatumia fursa hiyo kuzifunga kamera kwa mifuko meusi na kisha wakawasha taa.. Baada ya kuwasha taa ilikuwa sasa ni jaribio la kufungua mlango na hapa ndio wanatakiwa kuwa makini zaidi kwani wakikosea kitu kimoja tu maana yake alarm italia na mchezo utaishia hapo..

Itaendelea wakuu..

CREDIT TO JAMII FORUM
 

Gallery

Popular Posts

About Us