KINGAZI BLOG: 07/30/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Saturday, July 30, 2016

Wezi wa Umeme Waendelea Kukamatwa

Shirika la Umeme Tanesco Mkoa wa Kinondoni limeendelea kuwakamata wananchi wanaotumia umeme wa wizi kujiunganishia umeme kinyume cha sheria pamoja na kuwekewa mita za Luku na Vishoka ambao siyo watumishi wa Shirika hilo.

Katika eneo la Mbezi jijini Dar es salaam, Mfanyabiashara wa Chakula Mariam Mjema amejikuta matatani baada ya kubainika kuwa mita ya Luku aliyowekewa ilikuwa ya wizi na haina kumbukumbu Tanesco, huku umeme aliowekewa ukipitishwa moja kwa moja kutoka katika nguzo ambapo ametumia umeme huo kwa zaidi ya mwaka mmoja bila kulipia.

Akijitetea mbele ya mbele ya maafisa wa Tanesco na polisi waliofika eneo hilo,Mfanyabiashara huyo amedai kuwa vijana waliojitambulisha kuwa mafundi kutoka Tanesco walifika na kumfungia mita hiyo ya Luku na kuwalipa bila kupewa risiti.

Akizungumza baada ya kubaini wizi huo huo Afisa wa Tanesco mkoa wa kinondoni Injinia Marsel Antony amewatahadharisha wananchi kuwa macho dhidi ya Vishoka na huduma zote za mita za luku pamoja na kuunganishiwa Umeme zinapatikana katika ofisi za Tanesco na sio mitaani.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi siku 23 tangu amteue




Taarifa Ya Bunge Kwa Umma Kuhusu Kamati Za Bunge




Lil wayne aipaisha kwa hotuba ya Clinton



Mashabiki wa mwanamuziki wa Marekani Lil Wayne wamekuwa wakidai kwamba huenda maneno ya wimbo wa msanii huyo yalitoa msukumo kwa hotuba ya bi Hillary Clinton.

"When there are no ceilings, the sky's the limit," {Iwapo hakuna paa la nyumba basi ,kikomo ni mbingu},Clinton aliliambia kongamano la chama cha Democrat.

Alikuwa akizungumza baada ya kukubali tiketi ya kuwania urais kupitia chama cha Democrat.

Mashabiki wa msanii huyo wa muziki wa rap sasa wamezua uvumi katika mtandao wa Twitter wakipendekeza kuwa huenda ameshinikizwa na wimbo huo unaosema kuwa iwapo hakuna paa kikomo ni mbingu.

Hakujakuwa na tamko lolote kutoka kwa Hillary Clinton ama timu yake lakini Lil Wayne amekuwa akihusisishwa.

Amewaambia maripota kwamba yeye hana tatizo lakini akakiri kwamba hajaiona hotuba hiyo.
Baadaye alichapisha ujumbe wa kumuunga mkono mgombea huyo wa urais

 

Gallery

Popular Posts

About Us