KINGAZI BLOG: 06/28/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, June 28, 2016

Askari auawa baada ya kupigwa na wafugaji mkoani Tabora.

Watu watatu wameuawa kwa nyakati tofauti mkoani Tabora akiwemo Askali wa Jeshi la wananchi wa Tanzania,(JWTZ)aliyepigwa fimbo na wafugaji akiwa katika ujenzi wa nyumba yake,baada ya kuwalalamikia kuwa, ng’ombe wamevamia katika kiwanja chake na na kuharibu vitu mbalimbali vya ujenzi.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mkoani Tabora Kamanda wa polisi mkoani humo ACP Hamis Issa Suleiman,amemtaja marehemu kwa jina la Carritus Mkunozi (35) wa kikosi cha 212KJ,ambapo ugomvi ulitokea baada ya kupishana kauli na wafugaji,na ugomvi kuanza,ambapo alifariki akiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete muda mfupi,akipata matibabu.

Aidha amesema kuwa katika tukio hilo kundi kubwa la ng’ombe zaidi ya mia mbili,waliokutwa katika kiwanja cha marehemu huyo wanashikiliwa, na muuaji mmoja,huku akiwataja marehemu wengine,waliouawa kuwa ni mama mmoja,mganga wa kienyeji aliyepigwa fimbo kichwani baada ya kuwapa kisogo wauaji waliokuwa wamemwomba maji ya kunywa.

Katika hatua nyingine Kamanda Hamisi Issa Suleiman amesema huko kata ya kijiji cha Motomoto Vumilia wilayani Urambo kijana mmoja kibarua ambaye hakufahamika alipigwa ngumi kifuani na kufariki papo hapo, wakati wakigombea mgao wa posho ya kazi yao.

Gesi nyingine yagunduliwa Tanzania

Hifadhi Kubwa zaidi ya Gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa mataifa chache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi.
Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.

Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.

Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la bonde la ufa la Tanzania.
Katika taarifa kwa wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za kawi na teknolojia.

Kabla ugunduzi huo watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa 2035.

Mnamo mwaka wa 2010 Mwanfisikia mshindi wa tuzo la Nobel Robert Richardson alikuwa ametabiri kumalizika kabisa kwa gesi hiyo.

Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalamu kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura kama vile kwenye vibofu kutokana na hali ya kuwa gesi hiyo ya Helium ni nyepesi kuliko ile ya Oxygen.

''Gesi tuliyoipata huko Tanzania inaweza kujaza silinda za gesi milioni moja nukta mbili za mashine za MRI'' alisema Chris Ballentine kutoka chuo kikuu cha Oxford.

Yule Trafiki Aliyetukanwa na Mke wa Waziri Amepandishwa Cheo


Deogratius Mbango, askari wa kikosi cha usalama barabarani (trafiki) ambaye hivi karibuni alitukanwa na mke wa waziri wa serikali ya awamu ya tano (jina kapuni), baada ya kulikamata gari lake kwa kuvunja sheria za barabarani, hatimaye amepandishwa cheo ikiwa ni maagizo ya Rais Dk. John Magufuli.

Habari kutoka chanzo cha uhakika, zinasema kuwa askari huyo ambaye alilikamata gari la mke wa waziri huyo baada ya kuvuka sehemu ya waendao kwa miguu eneo la Namanga jijini Dar es Salaam, amepandishwa hatua moja mbele, kutoka koplo hadi sajenti.

Kitendo hicho cha kulikamata gari hilo, bila kujali utambulisho na matusi ya mwanamke aliyedai kuwa mke wa waziri, kilimfanya Rais Magufuli kumsifu na kumuona kuwa jasiri kazini kwake, hivyo kuliagiza jeshi la Polisi kumpa promosheni mara moja.

Juzi Jumapili, Uwazi lilimkuta trafiki huyo akiongoza magari maeneo ya Makumbusho katika lango la kuingilia daladala akiwa na cheo kipya cha usajenti.

Alipoulizwa kuhusu kuula huko, Mbango alikiri kutokea kwa jambo hilo na kumshukuru Mungu pamoja na uongozi wa Jeshi la Polisi kwa kumkumbuka, huku pia akilishukuru gazeti hili kwa kukumbushia katika toleo lake Na 993 lililoripoti juu ya kutotekelezwa kwa amri ya Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Gallery

Popular Posts

About Us