KINGAZI BLOG: 08/22/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, August 22, 2016

PICHAZ++ LOWASSA BAADA YA KUTUA KWA KISHINDO MBEYA












 








Mwanariadha Usain Bolt apata skendo ya picha, za, utupu na mwanafunzi

 Mwanariadha wa Jamaica, Usain Bolt (30) ameingia kwenye kashfa baada ya picha zake kadhaa akiwa na mwanafunzi wa kike wa Rio wa miaka 20 kusambaa mtandaoni.

Mwanafunzi huyo ambaye ametambulika kwa jina la Jady Duarte alisambaza picha kadhaa kwenye mtandao wa Whatsapp akiwa na Bolt kwenye pozi mbalimbali za kimahaba huku picha nyingine zikiwaonyesha wakiwa kwenye klabu ya usiku ya Barra de Tijuca iliyopo jijini Rio de Janeiro.

 Bolt akiwa na Jady Duarte kwenye klabu ya usiku

Akiongea na gazeti la Extra, Duarte amedai kuwa hakuwa anafahamu kama mwanariadha huyo ni maarufu zaidi duniani ndio maana ikawa rahisi kwake kusambaza picha hizo.

 Picha ya Jady Duarte

Aidha Bolt anadaiwa kuwa na mahusiano na Kasi Bennett (26) kwa takribani miaka miwili sasa na tayari walikuwa kwenye mikakati ya kufunga ndoa.

Hata hivyo hayo yakiendelea kutokea Bolt anasherehekea kusaini dili jipya na kampuni ya kutengeneza vifaa vya michezo ya Nike kwa mkataba wa miaka 10 ambao atakuwa akiingiza kiasi cha dola milioni 30 kila mwaka akiungana na mcheza kikapu, Kevin Durant aliyesaini na kampuni hiyo mwaka 2014.

Taarifa ya Jeshi la Polisi Kwa Vyombo Vya Habari na, umma


Katika siku za hivi karibuni, kumekuwepo na mitazamo tofauti miongoni mwa jamii kufuatia kuonekana kwa askari polisi wakifanya mazoezi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kufuatia hali hiyo, jeshi la polisi nchini, linatumia fursa hii kuwatoa hofu wananchi kwamba mazoezi hayo ni ya kawaida kwa askari wa jeshi la polisi

Aidha, jeshi la polisi linawataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kawaida kwa sababu mazoezi hayo hayalengi kuzuia shughuli zozote halali zinazofanywa na wananchi.

Imetolewa na:

Advera John Bulimba – Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP)

Msemaji wa Jeshi la Polisi,

Makao Makuu ya Polisi.

MREMBO RUBY AJA NA KAULI HII KUHUSU YEYE KUTOKWENDA FIESTA MWANZA

Muimbaji wa ‘Na Yule’ Ruby amesema hakwenda Mwanza kutumbuiza kwenye Fiesta licha ya ‘kusajiliwa’ kwenye msimu mpya wa tamasha hilo maarufu, kwasababu waandaji hulipa fedha ‘kiduchu.’
Kauli yake inakuwa mkuki kwenye moyo kwa Clouds FM ambao ndio waliomfikisha hapo alipo kwa kukivumbua kipaji chake.
Akiongea na tovuti ya Tizneez, Ruby alidai kuwa kutolewa kimuziki na Clouds Media, hakumaanishi kuwa ataendelea kuwatumikia kama wanavyotaka kwakuwa naye ana maisha yake kwa sasa.
“Kisa ni Clouds ndio nisiwe free na kuongea?” alihoji muimbaji huyo ambaye kwa miaka mingi sauti yake imekuwa ikisikika kwenye matangazo kibao ya kituo hicho maarufu cha redio nchini. Amedai kuwa show ya Fiesta ni kubwa kuliko maslahi wanayolipa na kwamba yangemwacha katika wakati mgumu kuandaa show yake.
Anadai kuwa hahofii vita yoyote na kituo hicho chenye nguvu kilichowahi kuingia kwenye mgogoro na wasanii kibao ambapo wapo walio kubali yaishe kwa kupiga magoti na kuomba msamaha, isipokuwa Lady Jaydee ambaye bado ana vita nao iliyodumu kwa miaka mingi.
Ruby anasema mwisho wa siku ni maisha yake ndiyo ya muhimu zaidi. Ruby alipatikana kupitia shindano la Supa Diva liliondaliwa na Clouds kupitia tamasha la Fiesta na kusainishwa chini ya kampuni ya THT iliyoanzishwa na Ruge Mutahaba.
“To be honest naumia dana sababu they don’t care,” anasema. “So if someone hakujali, what can you do? Tatizo ndio kama hilo unakuwa na management ambayo haijali maslahi yako kwenye maisha yako. Tunajikuta tunakuwa na management ambazo zinajali umabavu, zinaendesha wasanii kimabavu kuliko kiakili ya kutimiza malengo ya wasanii wao ambapo sisi wasanii wa kike tunaonewa sana. Unadhani kwanini Lady Jaydee wanamuita komando?” amehoji Ruby.
“Because ni mtoto wa kike, ni mwanamke ambaye amesimama kweli kweli na kujitetea, lakini wachache sana wanafanya hivyo.”
Kukiwekea kidonda chumvi, Ruby ambaye kwenye Instagram amepost video akiimba wimbo wa Lady Jaydee, amedai kuwa ana mpango wa kufanya naye kazi. “Nitafanya naye sababu ni muimbaji mzuri, ana sauti nzuri.”

Uamuzi wa Ruby kuisusia show hiyo hata hivyo unazua maswali mengi hasa kwakuwa kama wasanii wengine waliopo kwenye orodha ya waliosajiliwa, alionesha furaha kujumuisha na kupost picha takriban tatu akisaini mkataba. Haijulikani ni kwanini aliamua kuvaa nguo licha ya kuzivua akiwa tayari kuyaoga maji.
“Thank you 🙏 @cloudsfmtz @cloudstv @bdozen @sirballatz 
Nakila shabiki wa kazi yangu na wote wanaosapoti kazi ninayoifanya 
# TigoFiesta 2016 Imoooooooo,” aliandika.
Bila shaka Clouds watakuwa na upande mwingine wa shilingi kuelezea mkasa huu.

UVCCM Waitisha Maandamano Nchi Nzima Agosti 31

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamidu.

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wanatarajia kufanya maandamano ya Amani nchi nzima Agosti 31 kwa ajili ya kueleza utendaji kazi wa Rais Dk.John Pombe Magufuli kwa Watanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo, Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa wameshamwandikia barua mkuu wa jeshi la Polisi kwa ajili ya kupata ulinzi siku hiyo

Amesema kuwa wasipopata ulinzi watafanya kwa kujilinda wenyewe ikiwa ni lengo la kufikisha ujumbe kwa wananchi juu ya utendaji kazi wa Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Shaka amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli amefanya watendaji kuwa na utii pamoja na maadili katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Aidha amesema kuwa katika maandamano hayo wanaawalika na vijana wa vyama vingine kushiriki kwa lengo moja tuu,la kuunga mkono utendaji wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli.

MREMBO RUBY AJA NA KAULI HII KUHUSU YEYE KUTOKWENDA FIESTA MWANZA

Muimbaji wa ‘Na Yule’ Ruby amesema hakwenda Mwanza kutumbuiza kwenye Fiesta licha ya ‘kusajiliwa’ kwenye msimu mpya wa tamasha hilo maarufu, kwasababu waandaji hulipa fedha ‘kiduchu.’
Kauli yake inakuwa mkuki kwenye moyo kwa Clouds FM ambao ndio waliomfikisha hapo alipo kwa kukivumbua kipaji chake.
Akiongea na tovuti ya Tizneez, Ruby alidai kuwa kutolewa kimuziki na Clouds Media, hakumaanishi kuwa ataendelea kuwatumikia kama wanavyotaka kwakuwa naye ana maisha yake kwa sasa.
“Kisa ni Clouds ndio nisiwe free na kuongea?” alihoji muimbaji huyo ambaye kwa miaka mingi sauti yake imekuwa ikisikika kwenye matangazo kibao ya kituo hicho maarufu cha redio nchini. Amedai kuwa show ya Fiesta ni kubwa kuliko maslahi wanayolipa na kwamba yangemwacha katika wakati mgumu kuandaa show yake.
Anadai kuwa hahofii vita yoyote na kituo hicho chenye nguvu kilichowahi kuingia kwenye mgogoro na wasanii kibao ambapo wapo walio kubali yaishe kwa kupiga magoti na kuomba msamaha, isipokuwa Lady Jaydee ambaye bado ana vita nao iliyodumu kwa miaka mingi.
Ruby anasema mwisho wa siku ni maisha yake ndiyo ya muhimu zaidi. Ruby alipatikana kupitia shindano la Supa Diva liliondaliwa na Clouds kupitia tamasha la Fiesta na kusainishwa chini ya kampuni ya THT iliyoanzishwa na Ruge Mutahaba.
“To be honest naumia dana sababu they don’t care,” anasema. “So if someone hakujali, what can you do? Tatizo ndio kama hilo unakuwa na management ambayo haijali maslahi yako kwenye maisha yako. Tunajikuta tunakuwa na management ambazo zinajali umabavu, zinaendesha wasanii kimabavu kuliko kiakili ya kutimiza malengo ya wasanii wao ambapo sisi wasanii wa kike tunaonewa sana. Unadhani kwanini Lady Jaydee wanamuita komando?” amehoji Ruby.
“Because ni mtoto wa kike, ni mwanamke ambaye amesimama kweli kweli na kujitetea, lakini wachache sana wanafanya hivyo.”
Kukiwekea kidonda chumvi, Ruby ambaye kwenye Instagram amepost video akiimba wimbo wa Lady Jaydee, amedai kuwa ana mpango wa kufanya naye kazi. “Nitafanya naye sababu ni muimbaji mzuri, ana sauti nzuri.”

Uamuzi wa Ruby kuisusia show hiyo hata hivyo unazua maswali mengi hasa kwakuwa kama wasanii wengine waliopo kwenye orodha ya waliosajiliwa, alionesha furaha kujumuisha na kupost picha takriban tatu akisaini mkataba. Haijulikani ni kwanini aliamua kuvaa nguo licha ya kuzivua akiwa tayari kuyaoga maji.
“Thank you 🙏 @cloudsfmtz @cloudstv @bdozen @sirballatz 
Nakila shabiki wa kazi yangu na wote wanaosapoti kazi ninayoifanya 
# TigoFiesta 2016 Imoooooooo,” aliandika.
Bila shaka Clouds watakuwa na upande mwingine wa shilingi kuelezea mkasa huu.

Jeshi la Polisi Lamkamata Kijana akiuza fulana za UKUTA.......Latoa Onyo Kali Kwa Waliojipanga Kuandamana Septemba 1


Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema limejiandaa kudhibiti maandamano ya Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) yanayotarajiwa kufanyika Septemba Mosi mwaka huu.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro amewatoa hofu wakazi wa mkoa huo kuwa hakuna mtu na au kikundi chochote cha watu kitakachofanya maandamano siku hiyo.

“Habari ya Ukuta haipo,umeshabomoka na kama haujabomoka utabomoka, wakazi wa Dar es Salaam msiwe na hofu, fanyeni kazi na hata siku hiyo hakuna mtu atakayejitokeza barabarani kuandamana,”amesema.

Kamanda Sirro amedai kuwa siasa zinatakiwa kufanywa kwa amani na utulivu na kwamba wanasiasa wanaoitumia siasa kufanya vurugu hawatafanikiwa.

“Mimi niwahakikishie kwamba tunajiandaa kwelikweli kuhakikisha watu wanafuata sheria , anayetaka kuvunja sheria kwa kufanya maandamano aanze yeye ili nasi tuanze naye,” amesema.

Ameongeza kuwa ” Suala la utii wa sheria ni la msingi,kama kuna watu au kikundi cha watu kinataka kuitumia siasa kufanya uvunjifu wa amani wajue kwamba nafasi hiyo kwa Dar es Salaam haipo.”

Aidha,Kamanda Sirro amesema August 20 2016 Jeshi la Polisi lilipata taarifa toka kwa raia wema kuwa maeneo ya Kinondoni kuna duka linauza flana zenye maneno ya uchochezi yaliyoandikwa‘’TUJIPANGE TUKATAE UDIKITETA UCHWARA’’ , ‘UKUTA’ ‘
  
Amesema  Polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa aitwaye YORAM SETHY MBYELLAH miaka 42, mfanyabiashara na mkazi wa Mburahati akiwa anauza fulana hizo dukani kwake

 

Gallery

Popular Posts

About Us