KINGAZI BLOG: 04/23/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Saturday, April 23, 2016

VIDEO: Mafikizolo – “Colors Of Africa” ft. Diamond Platnumz & DJ Maphorisa



Fresh off the stables of South African group, Mafikizolo. Here is the highly captivating visuals to their previously released tune titled “Colors of Africa”. The record features fellow South African, DJ Maphorisaand Tanzanian act, Diamond Platnumz.

BOFYA HAPA KUONA VIDEO YA DIAMOND FT MAFIKIZOLO-COLOUR OF AFRICA.

Watch & Download (Official Video) Lady Jaydee - Ndi Ndi Ndi



Mwanadada mkongwe katika muziki wa bongofleva lady jay dee ameachia video ya wimbo wake Unaotamba uitwao  NDI NDI NDI.Video hiyo ameofanyia south afrika.bofya hapa chini kudownload video hiyo kali ya mwaka.USIIKOSE
 


NAFASI ZA KAZI TANZANIA NATIONAL ROADS AGENCY (TANROADS) TUMA MAOMBI KABLA YA TAREHE 10 MAY 2016


1. Axle Load Supervisor

2. Weighbridge Operators

3. Weighbridge Collectors

Uganda Yatangaza Rasmi Kutumia Bandari ya Tanga nchini Tanzania kusafirishia Mafuta Ghafi Yake

Hatimaye Serikali ya Jamhuri ya Uganda imetangaza rasmi uamuzi wake wa kutumia Bandari ya Tanga nchini Tanzania kusafirishia mafuta ghafi yake.

Uamuzi huo umetangazwa na Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Jamhuri ya Uganda wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa Ushoroba wa Kaskazini uliomalizika Jijini Kampala Uganda.

Mbowe ataja sababu 3 za UKAWA kususia Kikao cha bunge jana.


Kambi ya Upinzani bungeni jana imesusia kuwasilisha na kujadili hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu, huku kiongozi wake, Freeman Mbowe akitoka nje ya ukumbi huo, akitaja kasoro tatu zilizosababisha wachukue uamuzi huo.

Staili ya kususia kujadili hotuba hiyo ya bajeti ni mpya kwa kambi hiyo ya upinzani baada ya kutumia njia ya kutoka nje ya ukumbi wakati wa vikao vya Bunge la Katiba na baadaye kutumia njia ya kupiga kelele kukwamisha shughuli za chombo hicho wakati wa Bunge la Kumi.

Jana, Mbowe aliwaambia waandishi nje ya ukumbi kuwa kasoro zilizofanya wachukue uamuzi huo ni kukiuka masuala ya kisheria katika utekelezaji wa bajeti, kutotangaza kwenye Gazeti la Serikali mabadiliko ya wizara na kutorushwa kwa vipindi vya Bunge kwenye televisheni.

Mbowe, ambaye alikuwa akitarajiwa kusoma bajeti ya upinzani kuhusu Ofisi ya Waziri Mkuu, aliibuka na hoja hizo tatu kabla ya kuamua kutoka nje.

“Bajeti inakuwapo kwa sababu ni hitaji la kisheria. Inapokuwa Serikali inataka kupitisha bajeti, lakini haiheshimu bajeti hakuna sababu ya wabunge kukaa hapa kujadiliana, kutoa povu, kupitisha vifungu vya Katiba, halafu yenyewe haitekelezi wajibu wake kisheria,” alisema Mbowe nje ya ukumbi wa Bunge.

Alisema Serikali imekuwa ikikiuka sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri inayomtaka Rais kutengeneza mwongozo wa muundo wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake, ikiwa ni pamoja na kutangaza katika gazeti la Serikali mabadiliko ya wizara zake.

Alisema “Tulichelewa kuunda (Baraza Kivuli la Mawaziri) kwa sababu tulikosa instrument (nyaraka rasmi). Tukalazimika kuunda hivyohivyo. Sasa tumefika kwenye (Bunge bado Serikali haijaundwa officially (rasmi), kisheria. Haijawa gazetted (haijatangazwa kwenye Gazeti la Serikali),” alisema Mbowe.

“Mpaka leo Serikali hii inafanya kazi kwa kutumia instrument iliyosainiwa na Rais (wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya) Kikwete mwezi wa 12 mwaka 2010.

“Na wizara kuu kwa mujibu wa instrument ya mwaka 2010 ilikuwa ni Wizara ya Waziri Mkuu Tamisemi. Na Tamisemi ilikuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kwa hiyo baada ya uchaguzi wa 2010, Tamisemi imerudishwa Ofisi ya Rais, haiku tena Ofisi ya Waziri Mkuu. Lakini haijawa gazetted.”

Alitaja hoja nyingine kuwa ni uvunjwaji wa Katiba na sheria za nchi kuhusiana na bajeti unaofanywa na Serikali pamoja na kuminya uhuru na madaraka ya mhimili wa Bunge kwa kuzuia matangazo ya wasusia Bunge kurushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni.

“Hatutashiriki mjadala tunaendelea kutafakari hatua nyingine za kuchukua kama Serikali na Bunge hawatatafuta ufumbuzi wa masuala hayo matatu,” alisema Mbowe.

Mbowe aliingia ukumbini saa 9:56 alasiri akiongozana na mbunge wa Momba, David Silinde na alikwenda kusalimiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) George Masaju na Waziri wa Kilimo, Mwigulu Nchemba.

Mara baada ya kupewa nafasi na Mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge, Mbowe alieleza sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri ambapo alidai kifungu cha 5(1) kinaweka masharti kwa Rais kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu yake.

Alisema mpaka sasa Serikali inafanya kazi bila kuwa na mwongozo wa utendaji kwa wizara mbalimbali hivyo kazi nyingi za Serikali zinafanywa kwa kauli ya Rais.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo mpaka sasa mwongozo wa utendaji wa Serikali kwa kila wizara unaotumika ni uliochapishwa kwenye Gazeti la Serikali Namba 494 A la Desemba 17, 2010 ambao pia umetoa majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Kiongozi huyo alinukuu baadhi ya majukumu katika mwongozo huo kuwa ni kuratibu shughuli za Serikali, kiongozi wa Serikali ndani ya Bunge, kiungo kati ya Bunge na Serikali, shughuli za kisiasa na serikali na kuratibu sherehe na misaada mbalimbali.

“Kazi nyingine ni kusaidia urahisishaji wa mipango ya serikali katika kuhamishia makao makuu Dodoma, uwekezaji, uchumi, sekta binafsi na kusaidia maendeleo katika sekta za ndani,” alisema Mbowe.

Alisema Rais John Magufuli alifanya mabadiliko ya kuziunganisha wizara bila kubadili muongozo wa kisheria.

“Kitendo cha Serikali hii kuendesha kazi zake kwa mwongozo wa 2010 kina maana kwamba majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu bado ni yale yale ya mwaka 2010 kwa sababu gazeti hilo halijafutwa,” alisema.

Alifafanua kuwa jambo hilo ni uvunjwaji wa Katiba na sheria za nchi kuhusu bajeti unaofanywa na serikali na kwa mujibu wa Ibara ya 63 (3) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bunge limepewa mamlaka ya kujadili utekelezaji wa kila wizara na kuidhinisha bajeti ya Serikali.

Mbowe alisema ikiwa fedha zilizoidhinishwa na bunge hazikutosha kutekeleza majukumu, kifungu cha 41 (1) cha Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015 kinaelekeza kuwa serikali itawasilisha bungeni maombi ya idhini, bajeti ya nyongeza ya fedha zilizotumika ambazo zimezidi kiwango.

Alituhumu kuwa kumekuwa na uvunjwaji wa kifungu hicho na kutolea mfano bajeti ya Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano ya mwaka wa 2015/16 ilikuwa Sh 883.8 bilioni ambazo kati ya hizo, fedha za ndani zilikuwa Sh191.6 bilioni.

 “Jambo la kushangaza ni kwamba hadi kufikia mwezi Machi 2016 Wizara ilikuwa imeshapokea kutoka hazina Sh607.4 bilioni ikiwa ni fedha za ndani, kitendo kinachoonyesha kuwa na ongezeko kubwa la fedha za ndani,” alisema.

Alitaja kuwa tangu kuidhinishwa kwa bajeti ya Wizara ya Ujenzi, hakuna bajeti ya nyongeza iliyopelekwa bungeni na Serikali kwa ajili ya kupata idhini kutokana na matakwa ya Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015 au sheria ya fedha ya 2015.

 “Kitendo cha Serikali kuamua kuhamisha kiasi cha fedha ya bajeti bila ya kupata idhini ya Bunge ni dharau kwa bunge lakini mbaya zaidi ni uvunjwaji wa Katiba na sheria.” alisema.

 Nje ya ukumbi wa Bunge alisema:”Ukiwauliza wanapata wapi hizi fedha, wanasema ni maelekezo ya Rais kwamba fedha ziondolewe kwenye fungu hili, zipelekwe wizara hii.”

Vipindi vya Bunge
 Kadhalika, Mbowe alisema uamuzi wa Serikali kuminya uhuru na madaraka ya Bunge umewapora wananchi haki yao ya kupata habari kwa kuzuia mijadala bungeni kurushwa moja kwa moja na vyombo vya habari.

Alisema jambo hilo ni uvunjwaji wa Ibara ya 18 ya Katiba inayotoa uhuru kwa kila mtu kutoa maoni na kueleza fikra zake, kutafuta, kupokea na kutoa habari.

“Bunge ndipo mahali ambapo wananchi wanahoji na kuiwajibisha Serikali na wanajadili hoja za maendeleo kupitia wabunge wao waliowachagua, hivyo huwafuatilia kupitia kwenye luninga zao pia ubadhirifu wa miradi mingi uibuliwa huko,” alisema.

Alisema wapinzani wataendelea kutafakari kwa kina na makini hatua za kufuata na kisha akawasilisha.

“Kwa mazingira kama hayo, kambi rasmi ya upinzani bungeni haiko tayari kuendelea kushiriki katika uvunjaji Katiba, sheria na haki za msingi za wananchi,” alisema.

“Kambi rasmi haitakuwa tayari kuwasilisha hotuba yake katika mazingira haya na inaushauri uongozi wa Bunge kutafuta ufumbuzi wa haraka wa kadhia hii ili kurejesha heshima ya Bunge na haki za msingi.”

Baadaye, Chenge aliipinga kauli ya Mbowe kuwa Katiba imevunjwa na kusema alitumia maneno mazito na badala yake alimtaka atumie maneno kuwa Katiba ilitaka kuvunjwa.

Chenge aliitaka kambi ya upinzani kufuata taratibu kama wanaona kuwa wameonewa, badala ya kutumia maneno hayo na pia akata watafakari kama wangependa kuendelea na mjadala.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wa upinzani walionyesha kususia kwani hata walipoitwa na mwenyekiti hawakuchangia licha ya kuwapo ndani ya ukumbi wa Bunge.

Kauli ya Mbowe kwa wanahabari
Akizungumza na wanahabari Mbowe alisema uamuzi huo haujakiuka sheria kwa sababu Bunge liko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kwamba hawawezi kwenda mahakamani ili kupata tafsiri kuhusu suala hilo kwa sababu shughuli za Bunge zinatatuliwa na Bunge lenyewe si mahakama.

“Rais kama kiongozi wa nchi ana mamlaka ya kulisemea hili, atueleze kama ni yeye ndiye aliyeruhusu Bunge lisirushwe moja kwa moja. Awali walisema TBC hawatarusha ila kwa sasa vyombo vyote vimezuiwa,” alisema.

“Hivi sasa luninga zilizopo ndani ya Bunge zilizokuwa zikionyesha matangazo  nazo hazionyeshi kinachoendelea. Sasa watumishi wa Bunge watafuatilia nini?” alihoji Mbowe.

Kauli ya AG
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alisema: “Nitashukuru kama mtavuta subira majibu ya Serikali yatatolewa wakati wa kufanya majumuisho.”

Mtoto Mtanzania wa miaka 16 alivyoongea kwa kujiamini mbele ya viongozi wa dunia umoja wa mataifa


Mtoto Mtanzania mwenye umri wa miaka 16 Getrude Clement kutokea Mwanza amehutubia mbele ya viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa umoja wa mataifa akiwa mwenye kujiamini na kutoonekana kuwa na hofu japo anaongea kwenye jukwaa ambalo linatazamwa na viongozi mbalimbali.
Mataifa zaidi ya 150 yalitia saini makubaliano ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo Marekani ambapo katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki moon ndio alimkaribisha Getrude kuongea kwa kusema ‘ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana
Getrude alianza kwa kuwasalimia waalikwa huku ikiripotiwa Maraisi 60 walihudhuria na kisha akaeleza kuwawakilisha vijana na watoto ambapo alizungumzia mabadiliko ya tabia nchi, hatari yake na kwamba wamekua wakifikisha ujumbe kwa Wananchi juu ya mabadiliko hayo kama anavyoonekana kwenye hii video hapa chini.

Ukimya wangu umefanya nijipange zaidi - Marlaw


Msanii wa bongo fleva Lawrence Malima maarufu kama Marlaw ambaye alitamba na nyimbo nyingi kipindi cha nyuma kama Rita, Missing my baby, Bembeleza na nyinginezo amesema kuwa ukimya wake umempa nafasi nzuri ya kujipanga na kufanya kazi nzuri zaidi.
Msanii wa bongo fleva Raulence Malima, Marlaw
Marlaw ambaye aliweza kutambulisha style ya kiduku kwa mara ya mwisho alitamba na wimbo wake wa Pii-Pii ambao uliaandaliwa na mtayarishaji Tuddy Thomas na kuweza kubamba katika sehemu mbalimbali za nchi na kuchochea aina ya uchezaji ambao ulifahamika kama kiduku.
Baada ya wimbo huo Marlaw alikuwa kimya kisanaa na baadaye alifunga ndoa na msanii mwenzake wa Bongo fleva Besta.
Lakini Marlaw amewatoa wasiwasi mashabiki zake na kusema kuwa wakati wa ukimya wake kimuziki amepata nafasi nzuri ya kutosha kuandaa kazi zake za sanaa na kusema kuwa baada ya muda mfupi mashabiki wataweza kumsikia na kusikia kazi zake mpya na kuziona pia.
"Ni kweli mimi nipo na nipo vizuri kabisa maana Mungu anasaidia, ukimya wangu ni kwamba umenipa nafasi nzuri kuandaa tu kazi zangu kwa hiyo baada ya muda mfupi mashabiki wategemee kumsikia Marlaw na kuona maana nipo jikoni sasa nafanya mambo kwa ajili ya mashabiki zangu"

Gabo Zigamba ndiyo mrithi wa Kanumba?


Inawezekana si mara yako ya kwanza kusikia jina hili la Gabo Zigamba katika tasnia ya filamu nchini, wazazi wake walimpa jina la Salim Ahmed.
Msanii Gabo Zigamba
Muigizaji huyu kadili siku zinavyozidi kwenda anazidi kupenya masikioni mwa watu wengi na kuzidi kuonyesha uwezo wake katika uigizaji kiasi cha baadhi ya mashabiki kudai kuwa huyu ndiye mrithi wa Steven Kanumba katika tasnia hiyo kutokana

Pigo Jingine Kwa Waliotumbuliwa Na Wanaosubiri Kutumbuliwa Latangazwa,Mahakama ya Mafisadi Rasmi Mwezi Julai



WAKATI Rais John Magufuli akisisitiza kuwa utumbuaji majipu utaendelea kufanyika hadharani bila kificho, pigo jingine kwa waliotumbuliwa na wanaosubiri kutumbuliwa, limetangazwa.


Akisoma Mwelekeo wa Kazi za Serikali bungeni jana, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, mbali na kusisitiza kuendelea kushughulikia watendaji wazembe, wabadhirifu na wavivu, alitangaza kuwa Divisheni ya Mahakama ya Rushwa na Ufisadi imeanzishwa katika Mahakama Kuu na itaanza kazi zake Julai mwaka huu.


Hatua hiyo ni pigo kwa watuhumiwa wa ufisadi ambao tangu Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani, wamekuwa wakichukuliwa hatua hadharani ya kusimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zao, kiasi cha baadhi ya wanasiasa kushindwa kuvumilia na kujitokeza kulalamika.


Miongoni mwa wanasiasa waliojitokeza kulalamikia hatua ya watuhumiwa hao kuchukuliwa hatua ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu uliopita, Edward Lowassa.


Mahakama ya Rushwa
Mahakama hiyo ni moja ya ahadi zilizonadiwa na Dk Magufuli katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015-2020 wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana, akisema katika Hotuba ya Ufunguzi wa Bunge na kuirejea wakati wa uzinduzi wa Mwaka wa Mahakama na Siku ya Sheria Duniani.


Katika maandalizi ya uundwaji wake, Jaji Kiongozi, Shaban Lila, aliwahi kusema kwamba mahakama iliitisha wadau mbalimbali wa haki jinai, kuangalia namna ya kuanzisha mahakama hiyo, ambapo mjadala ulikuwa ni kuanzisha mahakama huru au kitengo maalumu ndani ya Mahakama Kuu, kitakachopewa kipaumbele cha kushughulikia mafisadi.


Akitangaza kukamilika kwa mchakato huo jana, Waziri Mkuu Majaliwa alisema: “Napenda kuliarifu Bunge kwamba Serikali imeanzisha Divisheni ya Mahakama ya Rushwa na Ufisadi katika Mahakama Kuu itakayoanza kufanya kazi Julai, 2016.”


Uharaka wa kesi
Mbali na kuanza kufanya kazi kwa mahakama hiyo, Waziri Mkuu Majaliwa pia alisema kuwa Serikali itaimarisha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), ili ziharakishe utoaji wa haki.


Uimarishwaji wa ofisi hizo pia unatokana na agizo la Rais Magufuli alilotoa siku hiyo ya uzinduzi wa Mwaka wa Mahakama na Siku ya Sheria Duniani, alipotaka kesi za uhujumu uchumi na ufisadi ziendeshwe kwa kasi, ili jitihada za Serikali za kupambana na matatizo hayo, zizae matunda.


Katika hotuba hiyo ya Siku ya Sheria Duniani, Rais Magufuli alielezea kushangazwa na kitendo cha ofisi ya DPP, kuchelewa kuwapeleka mahakamani watuhumiwa waliokamatwa na ushahidi.


Alitoa mfano wa watuhumiwa waliokamatwa na meno ya tembo, ambapo alitaja Mahakama ya Kisutu kuwa ilikuwa na kesi 26 za watu walioshikwa wakiwa na nyara za Serikali, lakini kesi hizo zikachukua zaidi ya miaka mitano bila kufanyiwa uamuzi.


Dk Magufuli alisema maelezo yaliyokuwa yakitolewa ni kwamba upelelezi bado unaendelea wakati wahusika wa kufanya upelelezi huo wapo na washitakiwa walishikwa wakiwa na vielelezo.


Alisema inawezekana hakimu akawa anataka kutoa hukumu, lakini DPP na Polisi wanaofanya uchunguzi, wanasema upelelezi unaendelea, jambo linaloonesha tatizo lililopo la ucheleweshaji kesi.


Utumbuaji kuendelea
Katika hotuba hiyo ya Majaliwa, iliyokwenda sambamba na makadirio ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2016/17, alisema Serikali itaendelea kuwawajibisha wale wote ambao hawataendana na Falsafa na Mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano, lakini akasisitiza kwamba serikali itachukua hatua kwa kuzingatia na kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma.


“Niwahakikishie Watanzania kwamba hakuna mtumishi au mwananchi atakayeonewa au kunyanyaswa katika hili. Hivyo wale wote ambao wako safi waendelee kutimiza wajibu wao bila woga. Kazi zifanyike kwa weledi na kwa kasi bila urasimu,” alisema.


Majaliwa alisema katika kutekeleza falsafa ya Hapa Kazi Tu na ili Tanzania ifikie uchumi wa kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 ni sharti kila mtu afanye kazi kwa bidii, maarifa na ubunifu wa hali ya juu.


“Ili yawepo mapinduzi ya kweli ya kuelekea kwenye uchumi wa Kati tunaodhamiria ni lazima tuimarishe uwajibikaji na maadili kwa viongozi, watendaji na kwa kila Mtanzania. Sote tumeshuhudia hatua zinazochukuliwa na serikali dhidi ya watumishi wasio waadilifu, wanaotumia fedha za umma na madaraka yao vibaya.

“Ndio maana tumeanza kwa nguvu kuimarisha nidhamu, uwajibikaji na matumizi sahihi ya fedha za umma ili zielekezwe kwenye shughuli zenye manufaa kwa Watanzania walio wengi na si vinginevyo,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.


Akizungumzia utekelezaji wa Sera ya Utoaji Elimu Bure kuanzia Darasa la Kwanza hadi Kidato cha Nne, Waziri Mkuu Majaliwa alisema ipo changamoto ya upungufu mkubwa wa madawati baada ya kuanza kuandikisha watoto shule bila malipo.


Kutokana na hilo, aliwaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini waliokamata mbao kutokana na makosa mbalimbali kutozipiga mnada mbao hizo na badala yake watumie mbao hizo kutengeneza madawati kuanzia jana na pia halmashauri kutumia rasilimali zake kutengeneza madawati kwa kila shule.

Rais Magufuli Awageukia Watumishi HEWA Ndani ya CCM



Rais John Magufuli juzi aliwazungumzia makada walioihama CCM wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliopita, alipoeleza kuwa kuondoka kwao pengine kulimsaidia kupata ushindi.


Bila kutaja majina ya waliokihama chama, Magufuli alisema ni vyema wana CCM wakasahau tofauti zilizojitokeza wakati wa uchaguzi huo na kuganga yajayo.


Rais alisema hayo kwenye mkutano na viongozi wa CCM wa mikoa na wilaya zote nchini, uliofanyika juzi Ikulu jijini Dar es Salaam.


Alisema kuna mengi yalitokea wakati wa uchaguzi huo na yalikidhoofisha chama na hivyo kuna haja ya kuyasahau yaliyopita na kuangalia mbele katika kukijenga chama.


“Lakini inawezekana wale walioamua kwenda kule walisaidia mimi kushinda,”alisema bila ya kufafanua.


Baadhi ya wana CCM waliokihama chama hicho wakati wa uchaguzi huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa kuanzia ndani ya chama hicho ni pamoja na mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowasa aliyehamia Chadema, Frederick Sumaye, ambaye kwanza alitangaza kujiunga na upinzani bila ya kutaja chama na mapema mwaka huu kukabidhiwa kadi ya Chadema.


Mwingine ni aliyekuwa kada mkongwe wa CCM, Kingunge Ngombale Mwiru, Balozi Juma Mwapachu, mawaziri, wabunge na madiwani, wengi wakijiunga na Chadema, ambayo ilimsimamisha Lowassa kuwa mgombea wake wa urais akiungwa mkono na vyama vya NLD, NCCR-Mageuzi na CUF vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).


Lowassa alionekana kuwa kinara kwenye harakati za urais ndani ya CCM, akichuana vikali na Bernard Membe, lakini jina lake halikufikishwa kwenye Kamati Kuu, ambayo ilitangaza majina matano, akiwamo Magufuli, yaliyopelekwa Halmashauri Kuu ya chama hicho.


Kitendo hicho kilifanya wajumbe wa Halmashauri Kuu kumpinga waziwazi mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na baada ya juhudi za wazee wa chama hicho, hali ilitulia na Magufuli akaongoza kwa kura nyingi. Baadaye Lowassa alitangaza kuhamia Chadema na kufuatiwa na wanachama kadhaa.


Alipotangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu, Magufuli alisema wakati akihutubia wanaCCM kwenye ofisi ndogo ya chama hicho Lumumba jijini, alisema uchaguzi huo ulikumbwa na hujuma zilizofanywa na wanafiki waliojificha ndani ya chama hicho.


Alisema ni vema wanafiki hao wakajisalimisha kwa kutubu kwa kuwa wamekigharimu chama hicho na kusababisha kiwe kwenye wakati mgumu.


Dk Magufuli alisema anaona ni bora kuishi na mchawi kuliko mnafiki, na kumuomba Kikwete asiwahurumie wanaokihujumu chama.


CCM walikidhoofisha chama

Juzi, akizungumza kwenye mkutano huo na viongozi wa CCM ambao katika hali isiyokuwa ya kawaida hawakuvaa sare zao za chama, Magufuli alisema waliokidhoofisha chama ni wana CCM wenyewe na ndiyo maana wapinzani walitumia udhaifu huo kukisaliti.


“Tulithamini fedha kuliko chochote. Wala hatukuuliza hizi fedha zimetoka wapi. Tuliowapa miradi, walituchezea, tumejikaanga CCM kwa mafuta yetu wenyewe. Kama tulifanya makosa, tusifanye tena,” alisema.


Aliwataka viongozi hao wa CCM kuanza kuzungukia maeneo yao ili kuwashukuru wananchi kwa ushindi na kukiimarisha chama.


“Kwa kifupi, nyinyi ndiyo Serikali. Kiongozi yeyote mnayemuona hatekelezi ilani yake, huyo hafai kwenye safari hii. Mimi niwaahidi hatutasita kuchukua hatua kwa wale mtakaoona hawafai,” alisema.


Awali Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana alisema Kamati Kuu ya CCM imepokea ripoti ya uchaguzi huo wa Oktoba 25 kutoka mikoa yote na wiki ijayo itafanyika tathmini ya maandalizi, mchakato wa kuwapata wagombea, matokeo, upigaji kura na utangazaji wa matokeo.


Azungumzia Watumishi Hewa  CCM

Kadhalika, Magufuli alimtaka Kinana kuanza kuchukua hatua za kuondoa wafanyakazi hewa ndani ya chama hicho.


“Na mimi nina uhakika katibu mkuu hata kwenye chama wapo wafanyakazi hewa kwa sababu watu ni wale wale, ni Watanzania wale wale. Kwa hiyo na wewe uanze kuchukua hatua dhidi ya wafanyakazi hewa walioko kwenye chama,” alisema.


Alisema Serikali inatumia zaidi ya Sh583 bilioni kulipa mishahara, lakini mpaka sasa kuna wafanyakazi 7,700 hewa wakati uchambuzi bado ukiendelea.

Adele Ndiye Mwanamuziki wa Kike Tajiri Zaidi Uingereza



KULINGANA na jarida la Kimataifa la Sunday Times Rich List, (orodha ya matajiri), staa wa R&B Adele anayetamba na ngoma zake kibao ikiwemo ile ya Hello ndiye mwanamuziki wa kike tajiri zaidi nchini Uingereza kwa sasa kwa kuwa na anautajiri unaofikia Euro milioni 85, sawa na Sh. trilioni 210 za Kitanzania.

Moto wa Magufuli wababua bungeni



SASA ni wazi kwamba kasi ya utendaji kazi wa Rais John Magufuli, imeanza kuisambaratisha Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, inayoundwa na vyama kutoka kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), baada ya jana wabunge hao kususa hotuba ya Waziri Mkuu.
         Mapema asubuhi, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliwasilisha Hotuba ya Mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi hiyo kwa mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
Hotuba hiyo iliwasilishwa baada ya kukamilika kwa mjadala kuhusu Mpango wa Maendeleo wa Taifa, uliowasilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, Aprili 20, mwaka huu bungeni mjini Dodoma.
            Katika mjadala huo, wabunge wa upinzani waliopata nafasi ya kujadili Mpango huo wa Serikali, walishindwa kujizuia na kukiri kuwa Rais Magufuli ni Rais wa mfano ambapo Mbunge wa Viti Maalumu, Upendo Peneza (Chadema), alikwenda mbali zaidi kwa kusema Tanzania imepata Rais sawa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
         Jana baada ya Waziri Mkuu kukamilisha hotuba yake kama ilivyo kawaida ya Kanuni za Bunge, hotuba hiyo ilifuatiwa na maoni ya Kamati za Kudumu za Bunge zinazoangukia katika Ofisi ya Waziri Mkuu.
         Katika mpangilio huo wa kawaida wa Bunge la Bajeti, taarifa ya kwanza ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Katiba na Sheria, Mohammed Mchengerwa na baadaye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ukimwi, Constantine Kanyasu aliwasilisha maoni ya Kamati hiyo kwa niaba ya Mwenyekiti wake, Hasna Mwilima.
Mbowe ‘ala kona’
Wakati ilipowadia zamu ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), kujitokeza mbele ya wabunge kuwasilisha Mpango Mbadala wa Maendeleo wa Taifa na maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni kuhusu hotuba ya Waziri Mkuu, kiongozi huyo hakutokea.
         Hatua hiyo ilimfanya Spika wa Bunge, Job Ndugai kutangazia Bunge kuwa tofauti na ilivyo kawaida, alikuwa hajapokea taarifa ya Kambi hiyo kuhusu hotuba ya Waziri Mkuu na kusema suala hilo ni la ajabu na halijawahi kutokea.
“Waheshimiwa Wabunge nafikiri mambo mazuri yaliyopo ndani ya hotuba ya Waziri Mkuu yamewaduwaza wenzetu wa Kambi ya Upinzani na kuwasambaratisha, maana hadi sasa sijapata hotuba ya maoni yao, kwani baada ya kukamilika kwa taarifa za Kamati wao ndio walipaswa kufuatia,” alisema Spika Ndugai na kuendelea; “Kwa vile hawa ni ndugu zangu na natambua mchango wao mkubwa kwa Bunge hili, nawapa nafasi ya kujipanga zaidi ili saa 10 wakati Bunge litakaporejea niwape nafasi ya kwanza ya kuwasilisha hotuba yao,” aliongeza Spika na kusitisha shughuli za Bunge mchana jana.
Bunge larejea, wasusa
Ilipofika saa 10 jioni jana, Bunge lilirejea kuendelea na kikao na kama ilivyotarajiwa, Mbowe alitakiwa kuwasilisha Mpango Mbadala wa Maendeleo wa Taifa na maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu mpango wa Serikali, pamoja na maoni ya Kambi hiyo kuhusu hotuba ya Waziri Mkuu.
                   Tofauti na matarajio hayo, Kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mbowe ambaye hivi karibuni ameonesha waziwazi kukerwa na utumbuaji majipu unaofanywa na Rais Magufuli, alisimama na kutangaza kususa Hotuba ya Waziri Mkuu.
              Akitoa sababu, Mbowe alisema wanasusa kushiriki mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu kutokana na sababu tatu; mosi, ikiwa ni madai ya Serikali kufanya kazi bila kuwa na mwongozo wa utendaji wake wa kazi kwa wizara mbalimbali. Madai mengine kwa mujibu wa Mbowe, ni uvunjwaji wa Katiba na sheria za nchi na kupokwa uhuru na madaraka ya mhimili wa Bunge.
Mwenyekiti awashauri
                         Kutokana na kauli hizo, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, alisimama na kutoa ufafanuzi wa madai hayo kwa kusema hoja zilizotolewa na wapinzani ni nzito na kuwashauri watafute msaada wa kisheria.
“Kwanza hoja iliyopo mezani ni mjadala wa hotuba ya Waziri Mkuu na ofisi yake, sasa hii hoja mliyowasilisha ni kitu tofauti kabisa na kinachojadiliwa, na kwa vile mmetoa madai mazito ya kuvunjwa kwa Katiba, niwashauri mkatafute msaada wa kisheria, hapa tuendelee na hoja iliyopo mezani,” alisema Chenge.
                            Alifafanua kwamba kwa kuwa wamedai Katiba imevunjwa, ni vyema baada ya kupata ushauri wa kisheria, waende katika mhimili wa dola unaotafsiri Sheria, ambao ni Mahakama kwa kuwa suala hilo la tafsiri bungeni si mahala pake.
                               Baada ya kuwapa ushauri huo, Chenge alisema ni vyema mjadala wa Waziri Mkuu uendelee kama ulivyokuwa kwenye ratiba ya mjadala na iwapo kambi hiyo itashiriki, ni sawa na iwapo hawatashiriki ni uamuzi wao pia.
Watoka, Mbowe afafanua
Kauli hiyo ya Chenge ilisababisha Mbowe akifuatwa na wabunge wa upinzani kuanza kutoka mmoja mmoja na walipofika nje ya ukumbi, waandishi wa habari wakamfuata kiongozi huyo, ili atoe ufafanuzi.
               Akizungumzia madai yao nje ya ukumbi wa Bunge, Mbowe alisema kambi hiyo, haitachangia chochote kwenye mjadala wa Waziri Mkuu ila hawataondoka bungeni.
Katika kile kinachodhihirisha mpango huo ulikuwa umeandaliwa ili kuwavuruga Spika Ndugai au Naibu Spika Tulia Ackson, Mbowe alieleza kushangazwa kuona viongozi hao kutokuwepo na badala yake Chenge, ambaye ni Mwenyekiti wa Bunge na Mwanasheria Mkuu wa zamani kukalia kiti cha Spika.
                    “Hatutaondoka bungeni ila tumekubaliana hatutachangia chochote kwenye wizara hii hadi pale ufumbuzi wa madai yetu utakapopatikana. Kwanza tunashangaa, tulijua anayeongoza kikao jioni hii ni Spika au Naibu Spika ila wamemuweka Mwenyekiti Chenge ambaye anajua Sheria ili atuvuruge,” alisema Mbowe.
               Akifafanua madai yao aliyowasilisha bungeni alisema Sheria ya mwaka 1980 ya Utekelezaji wa Majukumu ya Mawaziri kifungu cha 5 (1) inaweka masharti kwa Rais kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake na kuutangaza katika gazeti la Serikali.

Majipu yawagusa
Alidai mpaka sasa Serikali inafanya kazi bila kuwa na mwongozo wa utendaji wa kazi kwa wizara mbalimbali na kwamba hiyo ina maana kuwa Serikali inafanya kazi kwa kauli za Rais na mawaziri, ndio maana kinachoonekana ni mambo ambayo hayaeleweki ya utumbuaji majipu kwa kuwa Serikali haifuati mwongozo wowote wenye msingi na uhalali wa kisheria.
               Madai hayo ya Mbowe si mapya, kwani alianza kuyatoa mwishoni mwa Februari mwaka huu, ambapo wakati huo alionya alichoita fukuza fukuza ya watumishi wa umma bila utaratibu, huku akiomba viongozi wa dini kumsaidia kukemea.
Mbali na Mbowe, katika kile kilichoonekana kuwa hawaridhishwi na utumbuaji majipu, aliyekuwa mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa, mwanzoni mwa mwezi huu, alirejea kauli hiyo ya Mbowe, kwa namna nyingine.
                Lowassa yeye alidai kuwa utumbuaji majipu umesababisha hali mbaya ya maisha kwa wananchi, kwa kuwa watumishi hao wa umma wameachishwa kazi. Mgombea huyo alienda mbali zaidi na kudai kuwa, anasononeshwa anapoona watu wanaachishwa kazi katika mashirika ya umma.

Sh bilioni 6
Akizungumzia madai ya Serikali kuvunja Katiba na sheria kuhusu Bunge la Bajeti, Mbowe alidai Serikali imekiuka Katiba kwa kutumia fedha ambazo hazikuidhinishwa na Bunge na kusema jambo hilo linaua dhana ya madaraka ya Bunge ya kuisimamia na kuishauri Serikali.
         Mbowe katika hilo, alikuwa akizungumzia Sh bilioni 6, ambazo Bunge la Jamhuri ya Muungano katika kumuunga mkono Rais Magufuli, liliziokoa baada ya kubana matumizi katika maeneo mbalimbali, ikiwemo posho, safari za nje na viburudisho na kuzikabidhi kwa Rais Magufuli.
              Tayari Rais Magufuli alishaagiza fedha hizo zitumike kununua madawati kwa kila jimbo. Madai mengine ni yale ya Bunge kusitisha kuonesha shughuli za Bunge hilo moja kwa moja kwenye televisheni mbalimbali na hivyo kuwanyima uhuru wananchi wa kufuatilia.
                 Akizungumzia hoja hiyo, Mbowe alimuomba Rais Magufuli kuingilia kati ili matangazo ya Bunge yarejee kama ilivyokuwa awali.
        “Tunamuomba Rais Magufuli aingilie kati suala hili kwa sababu na yeye ana nguvu kisheria ya kuzungumzia hilo. Aseme kama ni yeye aliyetoa amri ya Bunge kutooneshwa live, basi aone haja ya kuamua matangazo hayo yarejee kwa manufaa ya umma,” alisema Mbowe.

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo Jumamosi ya April 23 2016 kwenye,Habari zaUdaku, Kitaifa,kimataifa na michezo.



  April 23 2016 naanza kwa kukuletea habari zote kubwa zilizobebwa kwenye Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye ,habari za kitaifa,kimataifa Michezo na udaku na stori nyingine kali ili ujue kilichojiri duniani.. usiache kukaa karibu kwenye kurasa zetu za mitandao ya kijamiiyaani facebook/tanzaniampyasasablog na twitter@tanzaniampyasasa.
20160423_051923
20160423_051936
20160423_052012
20160423_052026
20160423_052045
20160423_052055
20160423_052107
20160423_052118
20160423_052135
20160423_052145
20160423_052156
20160423_052207
20160423_052218
20160423_052231
20160423_052243
20160423_052253
20160423_052306
20160423_052315
20160423_052325
20160423_052334
20160423_052346
20160423_052355
20160423_052406
20160423_052421
20160423_052435
20160423_052445
20160423_052457
20160423_052508
20160423_052530
20160423_052540
20160423_052606
20160423_052619
20160423_052654
20160423_052705

Siwema wa Nay jela miaka miwili kwa kesi ya kutukana



Siwema akilia kwa uchungu baada ya kuona nyumba mpya ya mume wake


Mahakama kuu ya mkoani Mwanza imemuhukumu Siwema ambaye ni mzazi mwenzake na Nay Wamitego miaka miwili jela kwa kesi ya kumtukana mtu kwa njia ya mtandao.
Siwema alituhumiwa kumtukana matusi kwa njia ya mtandao mlalamikaji ambaye anafahamika kwa jina la Deo.
Akizunguza na kipindi cha Jahazi, kinachoruka kupitia Clouds FM, Nay Wamitego alisema ‘napambana kile nitakachoweza kuangalia kama kunauwezekano wa kumpa msaada’.
“Kuna vitu nafikiria kuvifanya ili kujaribu kumsaidia, baada ya kupata hizi taarifa kidogo kama siko sawa hivi. Ni mzazi mwenzangu mimi nay eye tulikaa muda mrefu, napambana kile nitakachoweza kuangalia kama kunauwezekano wa kumpa msaada mwingine kwa njia yeyote ili asiwe kwenye mazingira ambayo tayari ameshawekwa. Anayemshtaki najua anaitwa Deo, jina jingine silifaham,” aliongezea.
Nay na Siwema walifanikiwa kukaa kwenye mahusiano kwa kipindi kirefu na kufanikiwa kupata motto mmoja, Curtis kabla hawajachana na kila mtu kushika njia yake.

Raymond asimulia alivyopata tabu, ndugu zake walimkatia tamaa baada ya kuona hatoki (Video)



Kabla ya kuchukuliwa WCB, Raymond alikuwa msanii mwenye kipaji ndani ya Tip Top Connection lakini maisha yalikuwa yakimwendea kombo.
12530931_1134578353259492_799030960_n
Ilimlazimu kuvumilia na kusubiria zamu yake ya kutoka kwa muda mrefu kiasi ambacho hata ndugu zake kwao Mbeya walimkatia tamaa na kumsihi arudi tu.
“Namshukuru Mungu kwasababu nilishapata tabu sana. Kuna muda nilikuwa nakaa mwenyewe, sitaki kulia lakini machozi yananitoka kwasababu unapita kwenye situation ngumu, kuna muda unajiona una bahati mbaya,” anasema.
“Kuna watu unawaona kabisa huyu jamaa ananidharau kwasababu alishaniona tangu nahangaika, toka nateseka, kuna dharau zingine ukiziona zinauma. Ni vitu vingi ambavyo nilikuwa nakutana navyo nikivikumbuka.. kuna maneno ambayo nilikuwa nakutana nayo nikiyakumbuka yalikuwa yananiumiza moyo.”
“Ilikuwa wakati mgumu sana kwasababu kuna watu wengine nyumbani ‘wewe ulishaondoka nyumbani hatuoni nyimbo.’ Kwahiyo hadi nyumbani unapigiwa simu, mama, nani, kaka zangu. Nikawa naanza kujiona kama mla unga, yaani watu wamenikatia tamaa.”
Ray anasema ilifika hatua alikataa tamaa na kutaka kurudi Mbeya kiasi cha kumtumia Babutale ujumbe mrefu wa kulalamika uliosababisha wakosane kwa muda.
Anasema kwa sasa maisha yamebadilika kwa kiasi kikubwa kutoka kudharaulika hadi kuanza kuheshimika. Anasema hata mama yake anafurahia hatua aliyopiga.

bongo 5
 

Gallery

Popular Posts

About Us