KINGAZI BLOG: 08/02/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, August 02, 2016

Mwanafunzi UDOM auawa kwa kupigwa na wenzake Wakati Wakitoka Baa

Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza, Kitivo cha Sayansi ya Jamii katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Fredrick Joseph (25), ameuawa kwa kushambuliwa kwa kipigo na watu wanaosadikiwa kuwa ni wanafunzi wenzake wakati akitoka klabu ya pombe (Bar).

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika eneo la chuo hicho ambapo mwanafunzi huyo alisikika akipiga kelele ndipo walinzi wakafika na kumkuta akiwa anagalagala njiani.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, amesema mwanafunzi huyo ambaye ametokea Musoma mkoani Mara alishambuliwa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na watu wasiofahamika.

Amebainisha mwanafunzi huyo alikutwa majira ya saa 10 alfajiri katika eneo hilo la chuo hicho huku akisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu huyo alikuwa na ugomvi na watu hao katika klabu ya pombe ya Canival Pub iliyopo chuoni hapo.

“Alipoondoka kurudi bwenini akiwa njiani alishambuliwa na watu hao wasiofahamika na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake, kipigo kilichosababisha kifo chake wakati alipokimbizwa kutibiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma,” alisema Mambosasa

Amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo kwa uchunguzi zaidi na hadi sasa hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo.

Alipoulizwa kuwa taarifa za mwanafunzi huyo kushambuliwa na wenzake, Mambosasa alisema kwasababu inadaiwa haifahamiki upelelezi bado unaendelea.

“Kwa sababu mwenye bar si yupo, kama kuna ugomvi ambao ulikuwa unaendelea tutajua tu, nimemuelekeza OCD kufuatilia ni nani waliokuwa wanakunywa kwenye hiyo bar chuoni, ni lazima tu watakuwa wanachuo ili tuwabaini,”

Kamanda huyo amesema ameelekeza uchunguzi wa kina ufanyike kama kulikuwa na ugomvi ndio hao hao walienda kumtegea njiani.

Chanzo cha habari ambacho hakikutaka kutaja jina lake kwa madai kuwa  siyo msemaji wa polisi kimesema kuwa marehemu Joseph alikuwa anakunywa pombe pamoja na marafiki zake lakini baada ya kulewa walianza ugomvi ambao hata hivyo waliamuliwa.

“Baada ya kuamuliwa ule ugomvi wa awali ndipo wenzake walipokwenda kumsubiria kwa mbele kwenye kichaka ambapo walimvamia na kumshambulia na kumwacha karibu ya kufa,” kilisema chanzo hicho.

Kiliongeza kuwa, baada ya kumwacha hapo na kutoweka ndipo walinzi wa chuo hicho waliokuwa doria walimuokota na kumfikisha kwenye kituo kidogo cha polisi kilichopo Chimwaga ambapo alikimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma alipofariki wakati akipatiwa matibabu.

Chanzo hicho kimesema hakuna mtuhumiwa hata mmoja anayeshikiliwa na polisi kwa kuwa wote waliomshambulia walitoroka na hawajulikani walipo.

Waziri Mkuu akataa madawati ya Wakala wa Misitu TZ "

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekataa kupokea msaada wa madawati uliotolewa na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) baada ya kubaini yametengenezwa chini ya kiwango.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekataa kupokea msaada wa madawati uliotolewa na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) baada ya kubaini yametengenezwa chini ya kiwango.

“Ofisa Elimu njoo kagua haya madawati yaliyo mazuri nitayapokea na yaliyobaki yarudishwe karakana yakatengenezwe upya huu si wakati wa kupokea vitu vibovu,“ amesema.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Agosti 02, 2016) wakati alipowasili katika kiwanja cha Mabau, Mtibwa kwa ajili ya kuzungumza na wananchi ambapo alikabidhiwa madawati hayo na Meneja wa TFS….

Alisema anatambua dhamira ya TFS ya kuunga mkono jitihada za Serikali za kumaliza tatizo la upungufu wa madawati lakini hawezi kupokea kupokea madawati yaliyotengenezwa chini ya kiwango.
Baada ya Ofisa Elimu (Msingi) wa Wilaya ya Mvomero, Michael Ligola kukagua madawati 102 yaliyoletwa uwanjani hapo madawati 84 yalibainika kuwa ni mabovu na 14 tu ndiyo yalikuwa mazima.

Waziri Mkuu alisema hawezi kupokea madawati hayo yaliyotolewa na Meneja wa Msitu wa Mtibwa, Hamza Kateti na kuuagiza uongozi wa wilaya ufuatilie suala hilo kwa kuwa walitakiwa kuyakagua kabla ya yeye kukabidhiwa.

Katika hatua nyingine aliwasisitiza wazazi na walezi wa wilaya hiyo kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule na atakayeshindwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Serikali imewapunguzia mzigo kwa kuwaondolea michango na ada hivyo tumieni fursa hiyo kwa kuwapeleka shule watoto wote waliofikia umri wa kwenda shule na wasimamie masomo yao,” alisema.

Awali mbunge wa jimbo la Mvomero, Saddiq Murad alisema miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili wilaya hiyo ni pamoja na wafugaji kuingiza mifugo katika mashamba hivyo amemuomba Waziri Mkuu kuingilia kati suala hilo.

Akizungumzia namna Serikali ilivyojipanga kutatua changamoto ya migogoro baina ya wafugaji na wakulima Waziri Mkuu alisema wafugaji wenye mifugo mingi watahamishiwa katika vitalu vinavyomilikiwa na ranchi za Taifa na wenye mifugo michache watatengewa maeneo katika vijiji.

!

Mch. Msigwa asems lazima atalipa kisasi


KEJELI za Rais John Magufuli dhidi ya vyama vya upinzani lazima zijibiwe, tena bila hofu

Ni kauli ya Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini leo alipozungumza na mtandao huu kuhusu mashari aliyopewa kuhusu kufanya mkutano wake wa hadhara kwenye jimbo hilo.

“Magufuli (Rais Magufuli) amekuwa akitukashfu kuwa vyama vya upinzani ni vya hovyo hovyo na ameua nyoka imebaki mikia inachezacheza. Mimi sitoogopa, nitaongea kama ambavyo rais amekuwa akitukashfu,” amesema Mchungaji Msigwa.

Katika taarifa ya jeshi hilo yanye kumbukumbu Na. IRI/A.24/9/VOLXIII/273 iliyojibu barua ya Msigwa yenye kumbukumbu Na. MB/IR/M/O5 ya tarehe 1 iliyokuwa ikitoa taarifa ya kufanya mikutano ya hadhara mjini humo kuanzia tarehe 3- 22 mwezi huu, imempa masharti ya kuendesha mikutano hiyo.

Sehemu ya barua hiyo inasomeka “mikutano yote hiyo kibali kimetolewa kwako kama Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, sitarajii mtu mwingine kutoka nje ya Mkoa wa Iringa kuja kusemea kuhusu maendeleo ya jimbo lako ama kuja kupokea kero za wananchi wako na kuzijibia wakati hiyo ni kazi ya mwenye himaya ambaye ni wewe.

“Kashfa, kejeli, matusi na maneno ya uchochezi kwa viongozi wa serikali vitahesabika ni uvunjifu wa amani na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yako na zitapelekea kuzuiliwa kufanya mikutano yako inayoendelea.”

Mchungaji Msigwa amesema, kauli iliyotolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Iringa, SP Mjengi katika barua yake iliyohusu kufanya mikutano ya hadhara Iringa Mjini ni ya kipuuzi.

“Hii ni kauli ya kipuuzi. Jeshi la Polisi linatoa matamko bila kufuata sheria badala yake linamuogopa Rais Magufuli,” amesema Mchungaji Msigwa.

 

Gallery

Popular Posts

About Us