KINGAZI BLOG: 05/17/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, May 17, 2016

Mambo saba yazuia hotuba ya Ukawa bungeni

.

Hotuba ya Godbless

sakata la mkataba wa Jeshi la Polisi na kampuni ya Lugumi jana lilitikisa Bunge wakati msemaji wa kambi ya upinzani, Godbless Lema alipogoma kusoma hotuba ya maoni mbadala ya Wizara ya Mambo ya Ndani kutokana na kutakiwa kuondoa vipengele kadhaa, likiwamo suala hilo.
Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu alikatisha shughuli za chombo hicho jana asubuhi akieleza kuwa kwenye meza za wabunge kulikuwa hotuba ya Kamati ya Bunge pamoja na ya upinzani, lakini ya upinzani ijadiliwe kwanza na Kamati ya Kanuni za Bunge kama inakidhi maudhui ya Bunge.
Baadaye jioni alieleza kuwa baada ya Kamati ya Kanuni za Bunge kupitia hotuba hiyo, imebaini kasoro kadhaa na kupendekeza baadhi ya aya ziondolewe na ndipo alipomruhusu Lema kusoma hotuba hiyo ya maoni mbadala bila ya kujumuisha vipengele hivyo.
“Mheshimiwa mwenyekiti, kwa mwongozo wako huo, maana yake ni kwamba hotuba yangu yote nitakuwa nimeiondoa,” alisema Lema baada ya kusomewa maagizo ya kuondoa aya ambazo Zungu na kamati yake waliona zinakiuka kanuni.
“Basi mimi nishukuru tu kwa mke wangu kufika bungeni na tuendelee na shughuli nyingine.”
Lugumi Enteprises na Jeshi la Polisi walisaini mkataba wa Sh37 bilioni wa kufunga mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole kwenye vituo 108, lakini ilimudu kufunga kwenye vituo 14 tu, wakati ilishapewa asilimia 99 ya fedha hizo kinyume cha mkataba.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga anahusishwa kwenye sakata hilo kwa kuwa anadaiwa kuwa ni mbia kwenye kampuni ya Infosys iliyotakiwa kufunga vifaa hivyo.
Tayari Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) imeunda kamati ndogo kufuatilia suala hilo na kutoa taarifa baada ya wabunge kuhoji sakata hilo na kutaka mkataba huo uwasilishwe PAC.
Akiwa nje ya ukumbi wa Bunge jana, Lema alisema ni lazima waziri Kitwanga ajiuzulu ili uchunguzi wa kamati ndogo ya PAC ufanyike kwa ufanisi.
“Kampuni yake ndiyo iliyofunga vifaa vya LugumI kwenye vituo vya polisi na mimi nina nyaraka ambazo nimepewa na haohao Jeshi la Polisi, nyingi za kutosha. Sasa leo kamati inazunguka kwenye vituo vyote vya polisi wakati IGP alishasema vifaa vyote vilifungwa,” alisema na kuongeza:
“Kwa vile IGP alishasema vifaa vyote vilishafungwa, hiyo kamati inakwenda kumuhoji nani?”
Baada ya kurejea saa 10:00 jioni jana, Zungu alisoma maelekezo yaliyopendekezwa na Kamati ya Kanuni za Bunge kuwa yaondolewe kwenye hotuba hiyo ya upinzani kwa kuwa yanakiuka Kanuni za Bunge.
Zungu alisema baada ya kupitia hati zilizowasilishwa jana, alibaini kuwa taarifa ya upinzani imezungumzia mambo ambayo kwa maoni yake yanakiuka Kanuni za Bunge hivyo aliagiza Kamati ya Kanuni za Bunge ikutane ili kupitia na kujadili maudhui ya hotuba ya msemaji wa kambi ya upinzani bungeni na kumpa mapendekezo.
Zungu alisema kamati hiyo imebaini hotuba hiyo ilikiuka baadhi ya Kanuni za Bunge, hivyo imependekeza maeneo yote ambayo yamekiuka kanuni yarekebishwe.
Alisema maagizo hayo ni kuondoa kipengele kinachozungumzia mauaji ya viongozi wa kisiasa na maeneo yote yaliyoendana na kipengele hicho kuanzia ukurasa wa saba hadi wa tisa.
“Kwa eneo linalozungumzia mkataba tata wa Lugumi na Jeshi la Polisi, kamati inapendekeza maneno yote yanayoanzia ukurasa wa 10, aya ya nne hadi ukurasa wa 14 aya ya kwanza, yaondolewe,” alisema Zungu.
Alisema eneo jingine la kuondoa ni maneno yanayomhusu Rais John Magufuli katika sakata la uuzwaji wa nyumba za Serikali ambalo lilikuwa ukurasa wa 15, aya ya kwanza hadi ya tatu, badala yake kuweka neno “Serikali”.
Nyumba hizo ziliuzwa na Serikali ya Awamu ya Tatu wakati Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi.
Zungu alisema kipengele kinachohusu rushwa na Bunge kutumika kulinda wahalifu, kiondolewe kuanzia ukurasa wa 15 hadi 17 kwani kinakiuka masharti ya Kanuni za Kudumu za Bunge.
Pia, alisema kamati ilipendekeza kuondolewa kwa maneno yote yaliyoko kuanzia ukurasa wa 19 hadi 20 kwenye eneo linalohusu tabia ya Rais Magufuli na usalama wa nchi kwa kuwa yanakiuka kanuni.
“Baada ya kupitia maoni na ushauri wa kamati, naomba kutoa mapendekezo yafuatayo. Kwa kuzingatia masharti ya Kanuni ya 64(1) ambayo imekataza kuzungumzia jambo lolote ambalo linasubiri uamuzi wa Mahakama, kutotumia jina la Rais kwa dhihaka, kutozungumzia mwenendo wa Rais, kutosema vibaya au kutoa lugha ya matusi kwa mbunge yoyote.
“Baada ya kutafakari na kuzingatia maamuzi mbalimbali ya Spika na kuzingatia masharti ya Kanuni ya 64, namwelekeza msemaji wa kambi ya upinzani bungeni, aondoe maneno yote hapo juu,” alisema Zungu na kumwita Lema ili asome maoni mbadala, lakini akakataa.
Kutokana na msimamo huo wa Lema, Zungu aliruhusu majadala uendeleee na wabunge wakaendelea kuchangia hotuba hiyo.
Wakati akichangia, Lema alianza tena kuzungumzia suala la Lugumi, akimhusisha Waziri Kitwanga na kampuni ya Infosys, jambo ambalo Zungu alilizuia tena akisema tayari mambo hayo yameshapigwa marufuku.
Lema alikubali na kuahidi kuyaepuka masuala hayo huku akionya siasa zisifanyike bungeni kwa kuzuia mambo muhimu kuzungumzwa kwa kuwa hakuisaidii serikali yoyote.
Lema alimwambia Kitwanga ajibu hotuba yake na kwamba anayetafutwa si Lugumi, bali waziri mwenyewe ambaye alidai ana urafiki na Rais Magufuli, kauli ambayo ilimfanya Zungu amkatishe tena kwa kuwa ameshakatazwa kutumia jina hilo bungeni.
Zungu alimkatisha tena Lema na kumtaka ajikite katika mjadala bila kugusa watu, jambo lililomfanya ajiulize atazungumzia nini zaidi, huku akishangiliwa na wabunge wa kambi ya upinzani.
Kutokana na hali hiyo, Lema alisema ameanza kumkumbuka Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kwa kuwa alisemwa sana, lakini hakuwahi kuliingilia Bunge hata siku moja.
Jaribio la kuzungumzia sakata la Lugumi pia lilifanywa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba lakini naye alizuiwa na mwenyekiti.
Nje ya ukumbi, Mbunge wa Bunda (Chadema), Ester Bulaya alisema si vizuri kwa hotuba ya maoni mbadala kutosomwa kwa sababu ya kumlinda mtu mmoja.
“Kama kweli Mheshimiwa Rais hana hana upendeleo, angemwambia Waziri Kitwanga resign (jiuzulu) ili isitie doa hizo jitihada ambazo yeye anasema anazifanya kwa masilahi ya Watanzania,” alisema Bulaya, mmoja wa wabunge wanaochangia hoja bila ya woga tangu alipokuwa CCM.
“Leo hii waziri anapewa tenda kwenye wizara anayoiongoza, halafu tutegemee kuna haki itatendeka? Yaani kumlinda mtu mmoja eti ndiyo kunafanya kambi rasmi ya upinzani, ishindwe kutoa maoni mbadala?

Bajeti ya Mambo ya Ndani
Awali, akisoma hotuba ya makadirio na matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani, Waziri Kitwanga aliomba Sh864 bilioni kwa shughuli za wizara hiyo kwa mwaka 2016/17, lakini hakuzungumzia sakata la Lugumi na Jeshi la Polisi.
Alipohojiwa na waandishi wa habari nje ya ukumbi kuhusu sababu za kutolijumuisha, alisema kuwa hakulizungumzia kwa sababu ni suala ya kiutendaji na liko sawa.
Pamoja na Kitwanga kutozungumzia suala hilo, Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ililigusia.
Mwenyekiti wake, Balozi Adadi Rajabu alisema matarajio ya wengi ni kusikia kamati yake inazungumzia mitambo ya kuchukulia alama za vidole iliyoagizwa na Jeshi la Polisi.
“Naomba kulijulisha Bunge hili kuwa kamati inatambua uzito na umuhimu wa suala hili. Hata hivyo, kwa kuwa suala hilo ni hoja iliyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Bunge limeipa jukumu Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za umma katika wizara za Serikali yaliyoainishwa katika taarifa ya CAG, hivyo basi ni vyema PAC ikaachwa iendelee kushughulikia hoja ya CAG,” alisema Balozi Rajabu.
Awali, kabla ya agizo hilo la kuondoa maneno hayo kwenye hotuba ya Lema, Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa aliomba mwongozo akieleza kuwa kambi ya upinzani huandaa hotuba kama kambi hivyo haiwezekani wakapangiwa nani wa kwenda kwenye kamati na kama kuna udhaifu basi Serikali ijibu.
Akijibu hilo, Zungu alisema ndiyo maana amemtaka msemaji wa kambi hiyo pamoja na kiongozi wa kambi ya upinzani kukutana na Kamati ya Kanuni za Bunge kujadili suala hilo.
Zungu aliagiza tena Kamati ya Kanuni za Bunge na wajumbe wote wakutane na Lema ambaye ndiye msemaji wa kambi hiyo kwa Wizara ya Mambo ya Ndani na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe ambaye awali hakuwapo na kuwakilishwa na Mchungaji Msigwa.

NAFASI ZA KAZI Good Neighbors Tanzania


Job Vacancy > Accountant
Location > Dodoma 
Position Type > Full Time 
Organization Type > NGO

Good Neighbors Tanzania

Application Deadline: 04 Jun 2016

ACCOUNTANT POSITION DESCRIPTION:

Position Description Document (download) 

APPLICATION INSTRUCTIONS:

Mode of Application
Interested and qualified Tanzanians are invited to send their applications with only enclosed:

• Cover letter showing your competence and why you want to work with Good neighbors Tanzania and not any other NGOs
• Detailed curriculum vitae containing the complete names of candidate, complete addresses (postal, email, phone); together with names and complete contact details of three referees. Your CV should indicate the experience which are related to the administration and management and not just any experience.
• Reference letter/ Certificate of Service from the organization that you have worked at least 3years and it must be stamped.

The application should be addressed to Managing Director, GOOD NEIGHBORS TANZANIA, Makulu Street, House No; 8, Dodoma. E-mail through apply now button below 

Deadline: Submission of applications should reach the management not later than 4th June, 2016.

Note that: Only shortlisted applicants will be contacted through their active mobile numbers and email from 4th~10th June and the candidates will have to take care their expenses for transport and accommodation during the interview, there will be no any refund for any expenses incurred.

AVOID SCAMS: NEVER PAY TO HAVE YOUR CV / APPLICATION PUSHED FORWARD. 
ANY JOB VACANCY REQUESTING PAYMENT FOR ANY REASON IS A SCAM. IF YOU ARE REQUESTED TO MAKE A PAYMENT FOR ANY REASON, PLEASE USE THE REPORT ABUSE, OR CALL +255 768 982 800 TO REPORT THE SCAM.

IF YOU ARE QUALIFIED FOR THIS POSITION

 Apply Now

Serikali Kuajiri Askari Wapya 3700....... Askari 7000 na Wakaguzi 1300 Watapandishwa Vyeo


Serikali  inatarajia kumwaga ajira kwa askari  katika mwaka ujao wa fedha.Taarifa juu ya ajira hizo, zilitolewa jana bungeni  na  waziri  mwenye dhamana.

Akiwasilisha Makadirio ya Mapato ya Matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2016/17 kuhusu ajira za askari, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga alisema wataajiriwa askari wapya 3,700 katika mwaka wa fedha 2016/17.

Waziri Kitwanga alisema mbali ya kuajiri askari hao, pia watawapandisha vyeo askari 7,140, wakaguzi 1,325 na maofisa 991.

Alisema katika mwaka 2015/16, jumla ya askari polisi wapya 3,882 waliajiriwa, na askari wakaguzi na maofisa 4,065 wa vyeo mbalimbali walipandishwa vyeo kwa kufuata utaratibu wa ajira.

“Aidha, serikali imeendelea kuhuisha viwango vya mishahara na posho mbalimbali, ikiwemo posho ya chakula ambayo iliongezwa kutoka Sh 180,000 hadi kufikia Sh 300,000 kwa mwezi,” alieleza Waziri Kitwanga.

Alisema katika mwaka ujao wa fedha, Jeshi la Polisi litaongeza umakini katika kusimamia nidhamu kwa askari wake kwa kufanya uchambuzi wa kina (vetting) kwa kuchukua vijana waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wanaoomba kujiunga na Jeshi la Polisi ili kuwa na askari wenye nidhamu na moyo wa dhati wa kulitumikia Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wa Jeshi la Magereza, alisema linatarajia kutoa mafunzo kwa maofisa na askari 4,975 katika ngazi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na yale ya Taaluma ya Urekebishaji.

Alisema ili kukabiliana na changamoto ya uchache wa miundombinu ya makazi kwa askari Polisi, serikali kupitia mkopo kutoka Serikali ya China inakusudia kujenga nyumba 4,136 chini ya usimamizi wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi.

Akizungumzia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, alisema jeshi hilo linahitaji vituo 152 Tanzania Bara, lakini kwa sasa lina vituo 57 na kati ya hivyo, 38 vipo katika miji na 19 katika viwanja vya ndege.

Alisema huo ni upungufu wa vituo 95 hali inayosababisha maeneo mengi kukosa huduma za zimamoto na uokoaji.

Inategemea kujenga kituo kimoja cha zimamoto na uokoaji katika eneo la Kigamboni katika Jiji la Dar es Salaam na kuendelea na ujenzi wa Jengo la Makao Makuu Tazara - Mchicha, Dar es Salaam.

Aidha, alisema Jeshi la Polisi litaendelea kupambana na makosa yanayovuka mipaka hususani ugaidi, uharamia, biashara ya dawa za kulevya, biashara haramu ya kusafirisha binadamu, wizi wa vyombo vya moto hususani magari, wizi wa kutumia mitandao ya Tehama, bidhaa bandia, na biashara haramu ya silaha na uchafuzi wa mazingira.

MPYA KUHUSU VIJANA WALIOMALIZA KIDATO CHA SITA KUJIUNGA NA JKT MWAKA 2016

Mama atumiwa picha bintiye akidhalilishwa

Dar es Salaam. Mama mzazi wa binti mmoja mkazi wa Dakawa wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro hivi karibuni alipokea ujumbe wa picha ya video katika simu yake ya mkononi na haraka aliifungua akiwa na shauku ya kuitazama.
Lahaula! Shauku yake ya kuitazama video hiyo aliyodhani ni sawa na nyingine za matukio ambazo amekuwa akiziona zikisambazwa mitandaoni, iligeuka huzuni na fedheha kubwa alipoona ikimwonyesha bintiye akidhalilishwa na wanaume huku akilalamika asirekodiwe bila mafanikio.
Mama huyo alijizoazoa haraka na simu yake akatimua mbio hadi Polisi kuripoti tukio hilo lililolenga kumdhalilisha binti yake na kuifedhehesha familia nzima. Hicho ndiyo kiini cha vijana 11 wa Dakawa kukamatwa ili waisaidie Polisi kuhusu walioshiriki tukio hilo na walioisambaza video hiyo kwa mama huyo na kwenye mitandao ya kijamii hasa WhatsApp.
Katika video hiyo, wakati mwanamme mmoja akimdhalilisha huyo binti, mwingine alikuwa akirekodi na baada ya kukamilisha tendo hilo lisilo na utu tena bila huruma waliwatumia watu wengine katika eneo la Dakawa.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa aliliambia gazeti hili jana kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuona video ile alikuwa mama wa msichana. “Alikimbia polisi kwenda kutoa taarifa,”alisema Betty.
Baada ya kufika Polisi, Betty alisema polisi walimwambia mama huyo hawawezi kuandika maelezo hadi mhusika ambaye ni binti yake afike kituoni. Walisema hivyo kwa sababu ni mtu mzima hivyo anatakiwa kutoa maelezo mwenyewe. Saa chache baada ya kuandikisha maelezo yake, polisi waliwakamata vijana wawili kwa tuhuma za kuhusika na unyama huo. Betty alisema watuhumiwa hao walikamatwa juzi na leo watafikishwa mahakamani.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na kwamba hadi jana watuhumiwa 11 walikamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Kamanda Matei alisema tisa kati yao wanaoshikiliwa ni kwa kosa la kusambaza picha za utupu huku vijana wawili ambao ni Zuberi Thabiti (30) na Iddy Adamu (32) ni kwa kosa la kufanya mapenzi na msichana huyo kwa nguvu huku wakirekodi.
Ilivyokuwa
Akisimulia tukio hilo, Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao walifanya kitendo hicho Aprili 28 mwaka huu majira ya saa 1.00 usiku katika nyumba ya kulala wageni yenye jina la ‘Titii’ iliyopo Dakawa.
Kamanda Matei alisema kuwa binti huyo aliitwa kwenye nyumba hiyo ya wageni na Thabiti ambaye ni mkazi wa Mbarali wilaya ya Mbeya ambaye alikuwa na uhusiano naye kimapenzi. Baada ya kuingia chumbani alimkuta pia Adamu mkazi wa Makambako, Njombe ambao walimlazimisha kufanya mapenzi huku mmoja akimrekodi picha za video na baadaye kuzisambaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.
Wanaoshikiliwa kwa kosa la kusambaza picha za utupu ni Rajabu Salehe (26), Said Athman (26), Musi Ngai (36), Said Muhammed (24), John Peter (24), Hassan Ramadhan (27), Ramadhan Ally (26), Lulu Peter (38) na Magreth Njonjone (30).
Wote ni wakazi wa Dakawa, Morogoro na wamevunja Sheria ya Makosa ya Mitandao, kifungu namba 14, kifungu kidogo (1) (a)
Kamanda Matei alisema wakati wa tukio hilo watuhumiwa hao walimtisha binti huyo kwa kisu ili asipige kelele wakati akidhalilishwa na walimtaka asitoe siri hiyo vinginevyo watamuua.
Kamanda alisema wawili hao ni marafiki  wa msichana huyo na kwamba Thabiti ambaye ni mpenzi wa sasa wa msichana huyo alipanga na Adamu ambaye ni mpenzi wake wa zamani kumkomesha.
Alisema Thabiti alimwambia mpenzi wake wakutane hotelini. Msichana alipofika aliwakuta chumbani huku Adamu akiwa ameshika kisu na kamera. “Wakamlazimisha afanye vile na kumtishia kumuua kama angekataa,”alisema Matei.
Hata hivyo, Betty alisimulia kisa hicho na kusema watuhumiwa hao walifanya unyama huo kwa sababu ya usaliti wa mapenzi. Alisema msichana alidaiwa kujihusisha kimapenzi na dereva wa mpenzi wake.
Kwa mujibu wa Betty, baada ya mpenzi wake kugundua alipanga njama ili kuwakomoa wote wawili. Alisema mpenzi wake alimwambia wakutane hotelini na alipofika alimkuta Zuberi pamoja na dereva wa mchumba wake hotelini.
 “Akawambia wafanye kile kitendo huku akirekodi video,”alisema Betty. “Nia yake ilikuwa kuwakomoa…kwa nini atembee na dereva wake,”alisema Betty na kwamba baada ya hapo picha hizo zilianza kusambaa.
Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema hali hiyo inaonyesha jinsi maadili yanavyozidi kuporomoka katika jamii.
“Hilo siyo kosa la kisheria peke yake ni udhalilishaji mkubwa,”alisema.
Dk Hellen alisema licha ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kukemea suala hilo ni vyema jamii ikazingatia suala la maadili.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa), Edda Sanga alisema vyama vya kutetea haki za wanawake vinafanya mkutano wa pamoja kujadili suala hilo.
“Leo (jana) tumekutana ili tujadili na kuja na tamko la pamoja,”alisema Sanga na kuongeza kwamba jambo hilo halivumiliki kwa sababu vitendo kama hivyo vinaendelea kujitokeza mara kwa mara.

Jeshi la Polisi lawanasa Mahausigeli 15 waliokuwa wakipelekwa Oman.


JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewakamata wasichana 15 katika nyumba iliyopo maeneo ya Ukonga, waliokuwa tayari kusafirishwa kwenda Oman kufanya kazi za ndani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi wa kanda hiyo, Simon Sirro, alisema wasichana hao walikamatwa baada ya Polisi kupata taarifa toka kwa msiri kuwa kuna mtu amewaweka wasichana kwa ajili ya kuwasafirisha.

Sirro alisema Polisi walifuatilia na kufika katika eneo hilo na kufanikiwa kuwakuta katika nyumba ya Hadija Mohamed (40) wakiwa wamegawanywa katika vyumba viwili.

Alisema uchunguzi wa awali, umebaini kuwa mwanamke huyo anashirikiana na mwenzake Salma Habibu (43) mkazi wa Temeke kuwatafutia masoko nchini Oman na wao ni mawakala wanaoletewa kutoka mikoani na kuwapokea kwa ajili ya kuwasafirisha.

Aidha alisema watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.

Pia ametoa onyo kwa watu wenye tabia hiyo kuacha, kwani wasichana hao wakifikishwa nje ya nchi hufanyiwa vitendo vya kikatili na unyanyasaji.

Katika tukio jingine, Polisi kanda hiyo imewakamata vijana 75, ikiwa ni muendelezo wa msako wa vijana wanaofanya matukio ya wizi wa majimbani nyakati za usiku.

Magazeti ya Leo Jumanne ya May 17 2016

 


Walimu 35,411 Kuajiriwa Mwezi wa 7 Mwaka Huu


Walimu 35,411 nchini wataajiriwa katika shule za msingi na sekondari katika mwaka wa fedha 2016/2017.

Watakaokaidi kwenda kuripoti katika mikoa ya pembezoni, hawataajiriwa na serikali.

Hatua hiyo imeelezwa kwamba imetokana na serikali kupokea maombi mengi ya kazi kwa walimu, ambao mwaka jana hawakuripoti katika vituo walivyopangiwa pembezoni mwa miji kwa kutegemea kuajiriwa na shule binafsi, lakini hawakufanikiwa.

Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jaffo alisema hayo alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali (CUF) aliyetaka kufahamu serikali inafanya nini kwa walimu waliopangiwa kwenda mikoa ya pembezoni, ikiwemo Lindi na kwingineko, lakini hawakuripoti.

Jaffo alisema ni kweli kuna walimu wengi ambao hawakuripoti katika mikoa ya pembezoni. Alisema si Lindi peke yake, bali na mikoa mingine, ikiwemo Katavi na Kigoma.

Alisema kwa mwaka huu, wataajiri walimu 35,411, lakini ambaye hataripoti katika mikoa hiyo na kuishia mijini tu, hawataajiriwa tena serikalini, kama wanavyoomba tena baada ya kukosa katika shule binafsi.

JE VIPODOZI VYAKO UNAVYOTUMIA KUPENDEZESHA NGOZI YAKO


Ndugu msomaji wa kila siku wa makala zangu leo ningependa kusema yafuatayo katika makal yangu ya leo inayo husu namna ya kuchagua kitunza ngozi ambacho ni salama kwa afya yako.
ZIFUATAZO NI FIKRA POTOFU KUHUSU NGOZI YAKO NA VIPODOZI
1. Kipodozi ambacho kinachubua ngozi ndicho huitwa kipodozi chennye KEMIKALI. Hii fikra potofu ina angamiza afya za watu ungana name ujue kipodozi kipi ni kemikali na kipi sio cha kemikali.
2. Kupatwa kwa chunusi uso mzima ambazo zinashamiri kila siku kuhusisha vipodozi unavyotumia na hatimaye kubadili vipodozi kila siku. Leo hii utajifunza namna gani sumu katika mfumo wa chakula husababisha chunusi sugu na namna gani ya kuondoa tatizo na kukuepusha hatari ya kubadili vipodozi kila siku.
3. Kubadili vipodozi kila mara kwa dhumuni la kuondoa chunusi sio suluhisho kwa ngozi yako.

KIPODOZI CHA KEMIKALI NI KIPI?

Hiki ni kipodozi ambacho kina kiambata ambacho kinaweza kuathiri afya ya binadamu na kusababisha magonjwa na hatimaye ulemavu wa kiafya. Sio kweli kwamba vipodozi vyenye kemikali ni vile tu vyenye KUCHUBUA NGOZI YAKO bali vipodozi vingi tu vimekuwa vikipewa jina la kibishara kuwa ni vya ASILI na sisi watumiaji hutumia bila kuangalia kuwa vina viambata gani ambavyo haviwezi kudhuru miili yetu.

VIPODOZI VYA ASILI NI VIPI?

Hivi ni vipodozi ambavyo vimetokana na vitu asili ambavyo havina mathara kwa kumtumiaji na haviwezi kubadili utendaji kazi wa mwili pia afya ya mgonjwa. Vinaweza kutokana na mimea,matunda na wanyama pia mazao yatokanayo na wanyama kama asali, mafuta nk

VISABABISHI VYA CHUNUSU SUGU 
Ni dhahiri kuwa watu wengi tunajua kuwa chunusi husababishwa na utengenezwaji wa mafuta mengi ya sebum ambayo hutengenezwa na tezi iliyopio chini ya ngozi. Mafuta haya yakizidi kiwango huweza kuziba vitundu vidogo vya ngozi na hatimaye ngozi kutopumua vizuri kwani haitaweza kupitisha jasho ipasavyo na hatimaye kutengeneza mkusanyiko wa uchafu kwenye njia ya jasho. Mkusanyiko huu unaweza kuvamiwa na bacteria na hatimaye usaha kutungwa. Lakini hii sio kisababishi kikubwa cha chunusi sugu kwetu sisi binadamu ingawaje pia ni moja wapo ya kisababishi. Zingatia yafuatayo kama visababishi vikubwa vya chunusi sugu
1. Kuzidi kwa vichocheo vya androgen mwilini. Hivi ni vichocheo vinavyo shughurika na uzazi endapo vinapozidi husababisha utengenezwaji wa mafuta ya sebum kwa wingi. Vichocheo hivi huongezeka hasa wakati wa kubarehe ndio maana wengi chunusi hushamiri sana kipindi hiki. Lakini vichocheo hivi huweza kuvurugwa na utumiaji wa vyakula vyenye sukari sana kama soda, na vyakula vingine vya viwandani kama mikate, sambusa, danati na vingine vingi. Hivyo watu wengi hupatwa na matatizo ya chunusu sugu hasa ndogo ndogo hii ni kutokana na mvurugiko wa vichocheo hivi kutokana na maisha tunayo ishi nayo. Kitendo cha kutibu chunusu kwa kutumia sabuni za kupunguza mafuta ni dhahiri kuwa unaweza kupata nafuu lakini tatizo halitakwisha. Hivyo kuhakikisha kuwa unatibu tatizo la mvurugiko wa vichocheo hivi ndipo suluhisho la chunusu sugu litakuwa limeisha.
2. Kuchafuka kwa mfumo wa chakula kutokana na sumu kama mercury, arsenic na sumu zingine nyingi ambazo huathiri mfumo wa chakula mzima. Pia utumiaji wa vyakula vya ngano vyenye kwani vina protini iitwayo GLUTEN kwani ndio kisababishi kikubwa cha cha mfumo wa chakula kutofanya kazi ipasavyo na hatimaye kuharibu mifumo mingi ya utendaji kazi wa mwili. Hivyo watu wengi ambao hupata chunusi vidogo vidogo kama allergy kisababishi kikubwa ni utumiaji wa vyakula vya ngano vyenye GLUTEN.
3. Utumiaji vyakula vya sukari nyingi kwani ndio kisababishi kikubwa cha kuongezeka kwa sukari mwilini na kusabaisha insulin kuongezeka kwenye mzunguko wa damu. Kuongezeka kwa insulin huharibu vichocheo vingine na hatimaye kusababisha madhara makubwa ya mwili katika ndozi yako. Hapa ndipo utakuta watu wanene kupita kiasi haishiwi na vipele vidogo vidogo usoni hii ni kutokana na kwamba ameanza kupata dalili za mwanza za kisukari aina ya pili kwani ni ishara kuwa insulin haifanyi kazi ipasavyo.

4. Maambukizi kwenye ngozi. Kuna watu ambao imekuwa ni kawaida yao pindi tu wanapopatwa na chunusi huenda madukani kununua cream zenye antibiotics kama TETRACYCLINE CREAM, getriderm Na wengine hukimbilia kununua cream kama SONADEMA na nyinginezo. Unachotakiwa kujua ni kwamba sio kwamba hizi tube ni mbaya la hasha!!! Tube hizi zinashauriwa kutumika pale tu unapokuwa na chunusi zenye kutunga usaha. Hivyo tunakushauri utumie antibiotics cream hizi. Hivyo tufuate mashati ya matumizi ya dawa hizi zenye kemikali tuachane na matumizi mabovu na fikra potofu kila chunusi lazima uende phamarcy.

5. Mchafuko wa damu. Kama wewe huwezi kuondolea mwili sumu zinazo ingia mwilini kupitia ngozi, hewa, chakula mwili utaanza kuzito hizo sumu kupitia ngozi. Hivyo kuchafuka kwa ngozi yako ni dalili moja wapo kuwa umelemewa na sumu nyingi mwilini mwako unatakiwa kuzitoa tu hizo sumu kwa kutumia viondoa sumu yani anti oxidant. Hivyo kitendo cha kubadili vipodozi kila siku kwa dhumuni kuwa vimekukataa ni upotevu wa mali na kudhizidi kuingiza sumu zingine mwilini kupitia ngozi hiyo hiyo.

Basi leo ningependa nizungumzie sumu au kemikali ambazo zipo kwenye vipodozi vyetu vya kila siku na madhara yake. Kwani nimeamua kufanya hili baada ya kugundua kuwa watu hawajui nini hasa ya neon kipodozi chenye kemikali. Wengi wetu wamekuwa wakifikili kuwa kipodozi chenye kemikali ni kile ambacho kinachubua ngozi pekee lakini ukweli utajibiwa na maelezo yafuatayo kwa kina yanayo elezea jinsi vipodozi vingine ambavyo havichubui lakini vimebeba kemikali zinazo hatarisha afya zetu

ZIFUATAZO NI AINA ZA KEMIKALI ZINAZO HATARISHA AFYA ZETU KWENYE VIPODOZI

Vipodozi vyenye kemikali hupimwa ukali wa kemikali iliyomo humo kwa kutumia kipimo kiitwacho ENVIRONMENTAL WORKING GROUP au EWG. Hiki ni kipimo kinacho onesha uwezo wa kemikali kudhuru afya ya binadamu. Hiki kipimo kina madaraja makuu matatu yanayo onesha ukali wa kemikali husika kwenye kipodozi au vyakula kama ifuatavyo

1. EWG 0-2- ina madhara kidogo kwa binadamu
2. EWG 3-6- ina madhara ya kati kwa binadamu
3. EWG 7-10 – Inamadhara makubwa kwa binadamu.

Baada ya kuona madaraja ya kubaini viwango vya madhara vya kemikali mbali mbali kwenye vipodozi kulingana na ENVIRONMENTAL WORKING GROUP. Basi hebu naomba tuongelee kemikali mbali mbali zilizopo kwenye vipodozi vyetu vya kila siku na viwango vyake na madhara yake.

1. 1,4 DIOXINE
Hii ni kemikali amabayo hutumika kupunguza sumu ya kemikali kali ambazo zinatumika kutengeneza vipodozi au bidhaa yoyote kwa matumizi ya ngozi.
Ina kiwango cha EWG cha 8 tafsiri yake ni sumu kali zaidi 

MADHARA YAKE

a) Inasababisha kansa yani ni CARCINOGENIC kwani ina uwezo mkubwa wa kubadilisha seli za binadamu na kuwa kansa.
b) Ina ua figo yako yani ni kidney toxicant
c) Ina angamiza mfumo wa fahamu wa binadamu hasa ubongo na kusababisha magonjwa ya kusahau ovyo
d) Ina sababisha magonjwa ya mfumo wa upumuaji kama asthma ya ukubwani kutokana na madhara yake katika mapafu

INAPATIKANA WAPI

Aina hii ya kemikali ipo kwa wingi sana katika SHAMPOO na BODY LOTION tunazo tumia kila siku na kusema kuwa ni alama kwani hazichubui.
SOMA HAYA KUJUA KUWA KIPODOZI HIKI KINA 1,4 DIOXINE
a) Vipodozi vyote vyenye viambata hivi, eth, myreth,oleth,laureth na ceteareth ukiona hivi ujue kuwa hii kemikali ilitumika kuziandaa hizi kwa kuzipunguzia makali ya sumu.
b) Vipodozi vyenye PEG
c) Vipodozi vyenye, polyethylene glycol
d) Vipodozi vyenye, polyoxyethylene na Oxynol
Vipodozi vyote vyenye ingredient kama hizo ujue kuwa zina hii kemikali ambayo hadi sasa inaangamiza dunia kwa kutojua elimu hizi.

2. PARABENS

Hii ni aina ya kemikali ambayo ukichunguza kila vipodozi vina hiki kiini. Ili uweze kuhakikisha ni kuwa chunguza kwa makini vipodozi vyako itaikuta ipo katika mifumo aina kuu nne kama ifuatavyo
a) Methyl parabens: EWG 4
b) Ethyl parabens: EWG 4
c) Propyl parabens :EWG 7
d) Isobutyle parabens: EWG 7

MADHARA YAKE

Kemikali ya PARABEN ina uwezo mkubwa wa kuharibu mfumo wa vichocheo vya mwili yani HORMON. Kwani ndiyo kisababishi kikubwa cha kuvurugika na kuongezeka kwa vichocheo vya kike vya estrogen na kupelekea kuwa na maumivu wakati wa hedhi na matatizo mengine yote wakati wa hedhi. Pia husababisha kutokea kwa vimbe kama uvimbe wa titi na uvimbe kwenye kizazi

INAPATIKANA WAPI?
1. DEODORANT SPRAY
2. MAKE UPS
3. SHAMPOO
4. LOTIONS 
5. VIONJO KWENYE VYAKULA VYA VIWANDANI
6. DAWA ZA KEMIKALI
NOTE: Soma kwa makini mafuta yako ujue kuwa kemikali hii haipo kwani ndio suluhisho pekee la kuishi bila magonjwa sugu tafadhari kuhudhuria hospitali sio tiba bali kuepuka vitu kama hivi ndio tiba pekee

3. PHTHALATES
Kuna aina kuu nne kama ifuatavyo
a) Diethylhexyl phthalates EWG10
b) Dibutyl phthalates EWG 10
c) Dimethyl phthalates EWG 4
d) DiEHTYL PHTHALATES EWG 3
MADHARA
Inamaliza nguvu zakiume kwa kupunguza kiwango cha testosterone hormone pia ina punguza kiwango cha mbegu zakiume.
INAPATIKANA KATIKA MAJI YA KEMIKLI YA KUSAFISHIA NGUO,CHOO AU GARI, VIFAA VYA PLASTIC VINGI HUTENGENEZWA KWA HII CHEMIKALI
4. TOLUENE EWG 10
Hii aina ya kemikali hupatikana kwenye rangi mbalimbali za kupakalia majumba na vyombo mbali mbali
MADHARA
Matumizi ya mara kwa mara au kutumia kwa muda mrefu yanaweza kusababisha figo yako kuharibika,ini kuugua na kinga ya mwili kushuka

5. TICLOSAN
Hii kemikali hupatikana kwa wingi sana katika sabuni tunazo ogea kila siku. Hasa sabuni zilizo andikwa ANT BACTERIAL SOAP. Angalia kwa makini. 
MADHARA
Huvuruga hormone za kike,figo kufa na magonjwa ya moyo.
ANGALIA KOPO LAKO KWA MAKINI KWANI NINA IMANI KUEPUKANA NA HIVI VITU KUTAPUNGUZA GHARAMA ZAKUONANA NA DAKTARI KILA SIKU,KUPOTEZA MUDA WAKAZI UKIHANGAIKA KUTIBU UGONJWA NA KUPOTEZA NGUVU KAZI YA FAMILIA YAKO.

SOMA KWA MAKINI INGREDIENT ZA MAKOPO YAKO UNAPOSOMA ZINGATIA UJUMBE HUU

“Ushauri wangu ni kwamba tuache kupeperusha bendera ya umagharibi (kuiga tamaduni za kigeni), tudumishe mila zetu ikiwemo kula vyakula vya asili, matatizo haya yatapungua kwa kiasi kikubwa,” DR MERCOLA

Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudensia Simwanza alinukuliwa wakati mmoja akisema mamlaka hiyo imepiga marufuku vipodozi vyote vyenye viambata sumu, lakini watu wanaendelea kuvitumia.

“Madhara yake ni makubwa, mwanamke mjamzito ni rahisi kuzaa mtoto taahira, au mimba ikatoka,” alisema huku Daktari wa Magonjwa ya Ngozi wa Kituo cha Afya Centre, Isaack Maro akisema wanawake wanaotumia vipodozi vyenye viambata sumu huathirika kwa kiasi kikubwa bila kujijua.
Alisema madini ya zebaki yanayotumika katika vipodozi vingi hayatoki kwa urahisi mwilini kwani hujazana mwilini kwa muda mrefu na kusababisha maradhi.
VIPODOZI HATARI ZAIDI KWA MTUMIAJI : MISS AFRICA, CITROLIGHT, COCODERM, CAROLIGHT, MAXLIGHT, EXTRA CLAIR, TOP LEMON PLUS, BETA SOL LOTION, LEMONVATE CREAM, JARIBU KWANZA, DIPLOSON, SUPER CLAIR, CLAIR MEN, FAIR AND HANDSOME, BIOCLARE, CAROTONE, MEDICATED FADE CREME, PRINCESS CLAIR, EPIDERM, BETASOL, IVAN HABART na SICAIRE.

 

Gallery

Popular Posts

About Us