KINGAZI BLOG: 06/12/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, June 12, 2016

Maaaaaajabu!!!!!Mama ajifungua Watoto Mapacha kutoka kwa wanaume wawili tofauti.

Katika hali ya kushangaza, madaktari wamebaini kuwa mwanamke mmoja Jijini Hanoi, Vietnam amejifungua watoto mapacha ambapo alipata ujauzito wa pacha hao kutoka kwa wanaume wawili kwa nyakati tofauti.

Kwa mujibu wa CNN, familia ya mapacha hao ilianza kuwatilia shaka watoto hao kutokana na kutofanana kwao kwa kiwango kikubwa kama watoto wa familia mbili tofauti na ndipo ikawalazimu kuwaona wataalam wa afya ya uzazi kwa ufafanuzi zaidi.

Wataalam hao waliwafanyia vipimo vya vina saba (DNA) na kisha kubaini kuwa watoto hao hawakuwa wa baba mmoja.

Polisi wapiga Marufuku Mkutano wa Chama cha ACT Wazalendo, Millenium Tower DSM leo jumapili

Tunasikitika kuwataarifu Wananchi Na Umma Kwa Ujumla kuwa Polisi katika Mkoa wa Dar es Salaam wametuzuia kufanya Kongamano letu lililolenga kuchambua Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2016/2017. Polisi wamezingira eneo la ukumbi wa Kongamano (LAPF Millenium Towers) tangu saa 12.00 asubuhi.

Viongozi Wakuu wa chama wanakutana na waandishi wa Habari wa Makao Makuu ya Chama Kijitonyama kuanzia saa 7.30 Mchana kwa taarifa zaidi.

Abdallah Khamis
Afisa Habari Mkuu
Chama cha ACT-Wazalendo.

HEALTH TIPS Natural Ways to Help Fight Lung Cancer


lung-cancerLung cancer generally evolved in the cells lining bronchi, or even the bronchial tubes which help deliver oxygen to your lungs and bloodstream.

'ISLAMIC STATE :German citizens who fought with 'IS' under surveillance in Euro 2016


Some 500 Germans who have fought with terrorist group "Islamic State" are under surveillance during the Euro 2016 soccer championship. Germany kicks off its Group C campaign against Ukraine in Lille on Sunday.
Beglien Polizei bei einem anti-Terror-Einsatz in Brüssel
German Interior Minister Thomas de Maiziere told the "Bild am Sonntag" newspaper that security forces have received many tip-offs regarding possible attacks at Euro 2016, but

Maajabu Aishi siku 555 bila moyo wake, akitumia moyo feki

Kwa wapita njia , kijana huyo mwenye umri wa miaka 25 mkazi wa Michigan, alionekana ni mtu mzima akifurahia kuwapeleka watoto wake watatu katika park, akiwa na mdogo wake Dominique.

Kitu ambacho hakikuwa cha kawaida ni begi lake la kijivu alilolibeba mgongoni muda wote, ndilo lililokuwa likimuweka hai. Ndani ya begi hilo kulikuwa na mashine (power source) ya kusaidia kusukuma damu kwenye moyo huo feki kifuani kwake.

Moyo halisi wa Larkin ulitolewa kutoka mwilini mwake November 2014, na kuwekewa kifaa ambacho kilimuzesha kukaa nyumbani badala ya hospitali, wakati akisubiri kuwekewa moyo halisi wa binadamu.

Na hatimaye mwezi Mei mwaka huu, Larkin anaendelea vema baada ya kuwekewa moyo halisi wa binadamu katika kituo cha mishipa na moyo cha Frankel, katika chuo kiku cha Michigan, na kutarajiwa kurudi nyumbani kwake mapema ya wiki ijayo.

“Watu wengi wangeogopa kwenda muda mrefu na moyo feki, lakini nataka kuwaambia unatakiwa kwenda na woga, sikutaka kukubali upasuaji, ilinichukua wiki mbili kukubali, kwa sababu inasaidia, naenda nyumbani haraka baada ya upandikizaji, kwa sababu imenisaidia kuwa mwenye afya hata kabla ya upandikizaji”, alisema Larkin.

Kwa mujibu wa mtandao wa upandikizaji viungo (U.S. Organ Procurement and Transplantation Network), takwimu zinaonyesha kuna takriban wagonjwa 4,000 duniani, wanaosubiri kupandikizwa moyo wa binadamu.

Kijana huyo kutoka nchini Marekani alitoa wito kwa watu kujitolea viungo mbali mbali, ili kuweza kuokoa maisha ya watu wengine.




Watanzania Watakiwa Kushirikiana Kupiga Vita Matukio Ya Mauaji



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania, viongozi wa dini zote kushirikiana kwa pamoja kupiga vita matukio maovu ya mauaji yaliyotokea katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema anatarajia hali ya amani, usalama na utulivu inaendelea kuwepo nchini, hivyo wananchi hawana budi kushirikiana na kushikamana na Serikali katika kuhakikisha matendo maovu hayatokei katika maeneo yao.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Jumamosi, Juni 11, 2016) wakati  alipowasili mkoani Geita kwa ajili ya kuhudhuria ibada ya kuwekwa wakfu Padre Flavian Kassala kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki Geita.

“Mfano tukio la Mwanza watu wanavaa kanzu na wanaingia msikitini na kukuta wenzao wanafanya ibada kisha wakawachinja, hii haiwezekani kwa binadamu wa kawaida hivyo tushirikiane katika kupiga vita matendo haya,” alisisitiza.

Hivi karibuni jumla ya watu 15 waliuawa kwa kukatwakatwa na mapanga katika mikoa ya Mwanza,Tanga, Dar es Salaam  na Mara.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga amesema vitendo vya watu kuuawa kwa kukatwa mapanga vimepungua baada ya kuanzisha kampeni maalumu ya kukemea mauaji hayo.

Alisema katika kampeni hiyo wameamua kuwatumia walimu, viongozi wa dini mbalimbali pamoja na wauguzi ambao wamekuwa wakiwaelimisha wananchi kuachana na imani potofu za kishirikina na badala yake wajikite katika masuala ya maendeleo.

 

Gallery

Popular Posts

About Us