KINGAZI BLOG: 04/22/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Friday, April 22, 2016

Maajabu ya dunia!!!!!!!!!! Marehemu Ateuliwa Kusimamia Mechi Huko Nigeria



Mwanamume aliyefariki ameteuliwa kusimamia mechi ya soka nchini Nigeria ambayo itachezwa Jumapili, mwandishi wa BBC anayefuatilia masuala ya soka Oluwashina Okeleji anasema.

Wale Akinsanya aliteuliwa kuwa mwamuzi kwenye mechi baina ya Warri Wolves na Giwa FC katika mji wa Warri kusini mwa Nigeria, gazeti la Punch la Nigeria limeripoti.

Hii ni licha ya kwamba Akinsanya alifariki tarehe 22 Januari 2016 wakati wa kufanywa kwa mtihani wa Fifa Cooper Test, ambao hutumiwa kuamua iwapo marefarii wanatosha kuendelea kusimamia mechi.


Aliteuliwa kusimamia mechi hiyo na mrengo wa Shirikisho la Soka la Nigeria (NFF) unaoongozwa na Chris Giwa.

Video ya ‘Ndi ndi ndi’ ya Jide yazinduliwa rasmi

1....akizungumza jambo kwa mashabiki wake katika hafla hiyo.
2
Lady Jaydee ‘Jide’ akizungumza jambo kwa mashabiki wake katika hafla hiyo.
 4.Msanii Bob Junior (kulia) akizungumza na Global Tv Online kuhusiana na uzinduzi huo wa Video ya 'Ndi ndi ndi' ya Lady Jay Dee.
Msanii Bob Junior (kulia) akizungumza na Global TV Online kuhusiana na uzinduzi huo wa Video ya ‘Ndi ndi ndi’ ya Lady Jaydee.
5.Baadhi ya mashabiki wakifuatilia hafla hiyo.
3.
Baadhi ya mashabiki wakifuatilia hafla hiyo.
6.Lad Jay Dee akifanya mahojiana na baadhi ya wanahabri waliofika kwenye hafala hiyo. 7
Lady Jaydee akifanya mahojiano na baadhi ya wanahabari waliofika kwenye hafla hiyo.
VIDEO ya wimbo wa Lady Jaydee ‘Jide’ ya ‘Ndi ndi ndi’ imezinduliwa jana rasmi jijini Dar es Salaam ambapo uzinduzi huo ulifanyika maeneo ya Samaki Samaki-Masaki.
Katika hafla hiyo wasanii mbalimbali wa muziki akiwemo Bob Junior pamoja na mashabiki wa muziki walihudhuria kumpa sapoti katika uzinduzi huo.
Akizungumza na Global TV Online, Bob Junior alianza kuipongeza video hiyo kwa kusema;
“Nimekuja hapa kumpa sapoti kama dada yangu na kama msanii mwenzangu. Kiukweli video hii itafika mbali Afrika, kwanza ina ubora na pili imefanywa na dairekta mkubwa Afrika (Justin Campos),” alisema Bob Junior.
Video ya wimbo huo inatarajiwa kuanza kuonekana leo kupitia kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa kupitia EATV.


SOURCE GLOBAL PUBLISHERS.

Diamond ni… Busta ya Mastaa Afrika


Nassibu Abdul a k a Diamond Platnumz

 

Miaka kumi tu nyuma, ulipokuwa ukimzungumzia mwanamuziki mwenye jina kubwa kwa sasa, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ hakukuwa na mtu aliyekuwa akimfahamu, labda washkaji zake wa kitaa ambao kwa namna moja au nyingine walikuwa wakimwambia ‘Mwana wewe pigana tu kuna siku utatusua”.

Ndiyo, alipambana, alipopiga ngoma kama Kamwambie, Mbagala na nyingine nyingi zilimfanya kuwa juu na kumpa tuzo kadhaa. Leo hii, unapomzungumzia Diamond, haumzungumzii yule kijana aliyeiba hereni za mama yake akauze ili akarekodi singo yake, bali utakuwa unamzungumzia msela f’lani mwenye taito kubwa hapa Bongo.

Baada ya kukimbiza sana, mwisho wa siku mwana akajikuta akiwa staa mkubwa, si Bongo tu, mpaka nje ya nchi hii. Kwa sasa, amekuwa ni busta kwa mastaa wengine, yaani staa kutoka ndani na nje ya Afrika anamshukuru Diamond kwa kumfanya kujulikana zaidi. Wapo wengi lakini wachache wafuatao wanaweza kukubali kuwa, Diamond amewabusti kimtindo.


Diamond na AY

AY
Ukizungumzia wasanii wa kwanza-kwanza kutusua nje ya mipaka ya Bongo, huyu msela yupo. Alipiga ngoma nyingi na wasanii wa Uganda, Kenya ila pia alipiga ngoma na msanii kutoka Jamaica, Sean Kingstone.

Baada ya kuvuma sana na kuweka video zake Youtube, hakuwa na watazamaji wengi. Kwa mfano ngoma yake ya Touch Me aliyofanya na Sean Kingstone ambaye ana mashabiki wengi duniani ilipata watazamaji 110,703 duniani kote. Ukiachana na hiyo, ngoma yake ya kimataifa ambayo

aliwahi kufanya na Saut Sol ya I Don’t Wanna Be Alone ilipata watazamaji 26,097.
Achana na video hizo, baada ya kukaa kwa kipindi kirefu ndipo akaamua kufanya hit song na Diamond iitwayo Zigo remix. Cha kushangaza zaidi, ndani ya wiki ya kwanza tu ikawa na watazamaji milioni moja, kwa siku 67 ikawa milioni 5.

Mwenyewe ameshangazwa, hakuamini kilichotokea lakini kwa jicho la tatu ni lazima tugundue kwamba ni nguvu ya Diamond Platnumz ndiyo iliyomfanya kufikisha watazamaji wengi namna hiyo.


Diamond na AKA

AKA
Unapomzungumzia msanii mkubwa Afrika, basi huyu Msauzi, AKA jina lake halitakosa. Ana jina kubwa na amefanya ngoma nyingi ila katika video zake zote, video ambayo imetazamwa na watu wengi ni ile ya Make Me Sing ambayo amepiga na Diamond Platnumz ambayo mpaka sasa ina watazamaji milioni 2,924, 412

Amepaishwa, ameweka rekodi ya kuwa Msauzi wa kwanza video yake kutazamwa na watazamaji wengi ndani ya wiki ya kwanza tu ambayo ilifikisha watu milioni moja. Nyuma ya hayo, kuna jina la Diamond ambalo limemfanya kupata watazamaji wengi kwani ngoma yake yenye watazamaji wengi mbali na hiyo ni Baddest aliyowashirikisha Burna, Chana na Yanga ina watazamaji milioni 1,097,812.

Juzikati alifunguka kwamba amefurahi sana kwani ngoma yake imemtambulisha mpaka nchini Rwanda ambapo yeye anaamini hayo ni mafanikio makubwa, ila kupitia mgongo wa Diamond ameweza kufanya vizuri Afrika Mashariki na ngoma zake kupigwa mara kwa mara.


Diamond na Akothee

AKOTHEE
Ni mwanamuziki mkongwe, kutoka katika familia ya kitajiri nchini Kenya. Inawezekana haukuwa ukimfahamu ila baada ya kufanya Ngoma ya My Sweet Love na Diamond, ukamfahamu.

Ni mwanamuziki aliyepaishwa zaidi na Diamond, amepiga ngoma nyingi lakini hata video zake hazikuwa zikiangaliwa na watu wengi mitandaoni. Akaona kwa kusafisha nyota bora apige Ngoma ya Give It To Me na mwanamuziki kutoka Nigeria, Mr Flavour ndipo ngoma hiyo ikatazamwa na watu 267,573 tu.

Unajua alifanya nini baada ya hapo? Akaamua kutoa ngoma na Diamond iitwayo My Sweet Love ambapo kwa kupitia jina la Diamond mpaka sasa imetazamwa mara 1,494,675, mara tano zaidi ya ngoma aliyopiga na Flavour.

Mbali na kuwang’arisha zaidi wakongwe hao, pia Diamond hakuwa mbali katika kuwatangaza wanamuziki chipukizi akiwemo Hermonize ambaye mpaka sasa video yake ya Bado imetazamwa mara 2,897,477 huku ngoma ya wakongwe, Saut Sol waliyomshirikisha Ali Kiba ya Unconditionally Bae ikiwa imetazamwa mara 1,168,202 tu

Waziri Mkuu Majaliwa Kaguswa na kero za Elimu, kutoa maagizo haya ndani ya Bunge



Bunge la 11 limeendelea tena leo April 22 2016, Waziri mkuu Kassim Majaliwa amehutubia bunge kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za Serikali na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2016/2017.

Katika kitengo cha huduma ya Jamii Elimu, Waziri Majaliwa amesema ‘Kwa kutambua umuhimu wa Elimu kama nyenzo imara ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, Serikali imeanza kuboresha na kuimarisha elimu ya awali, msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu.’

Baada ya kuanza utekelezaji wa mpango wa elimu bila malipo, kumejitokeza changamoto kadhaa, ikiwemo miundombinu kama madarasa, mabweni, maabara, nyumba za walimu na vyoo‘ ;-Waziri Mkuu Majaliwa

Napenda kuwahakikishia wananchi kwamba Serikali inaendelea kuzifanyia kazi changamoto hizo na jitihada kubwa zimewekwa‘ ;-Waziri Mkuu Majaliwa

Nitumie nafasi hii kuwashukuru wadau walioanza kuchangia madawati katika maeneo mbalimbali,na niwasihi wengine waendelee kuunga mkono Serikali yao‘ ;-Waziri Mkuu Majaliwa

Kuanzia leo hii, nawaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wote waliokamata mbao ndani ya Halmashauri zao kuzitumia kutengeneza madawati na siyo kuzipiga mnada‘ ;-Waziri Mkuu Majaliwa

Hali ya urejeshaji wa mikopo iliyotolewa hairidhishi, Hivyo naagiza Bodi ya mikopo ya Elimu ya Juu kufuatilia urejeshaji wa mikopo hiyo ili fedha hizo zitumike kuwakopesha wanafunzi wengine‘ ;-Waziri Mkuu Majaliwa


Picha Mzee Mengi na Jacqueline Maisha ni Motomoto... Wakubwa Wanafaidi Sana


Kweli pesa ni kila kitu.Hizi ndio pesa na raha yake,sio wale watani zangu wa Nyanda za Juu Kusini,unakuwa na pesa halafu mke unamuweka kama "msukule" anakaa tu dukani siku nzima.

Msafara wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo Wapotea Dodoma


Msafara wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo leo asubuhi ulipotea njia kutokana na watumishi wa Manispaa ya Dodoma kutojua eneo ambalo waziri huyo alikuwa analitembelea.

Waziri Jafo alikuwa amepanga kufanya ziara kwenye Shule ya Msingi ya Nzuguni B kwa lengo la kuangalia mapungufu, hasa tatizo la uhaba wa madawati, lakini hakufika kama alivyotarajia kutokana na watumishi hao kutojua eneo ambalo shule hiyo iko.

Shule hiyo haijawahi kutembelewa na ofisa elimu tangu mwaka 2007 licha ya kuwa kilomita 6 kutoka katikati ya mji.

Naibu Waziri alikasirishwa na kitendo hicho akawataka watumishi wa idara ya Elimu wajipime kama wanastahili kuendelea kufanya kazi.

“Mstahiki Meya, mimi niliona wazi kuwa watumishi wako wananipoteza," alisema Waziri Jafo.

"Nimechukia sana na hawa watu. Tatizo lao ni kwamba hawajawahi kuja katika shule hii tangu mwaka 2007, lakini wamekaa ofisini tu. Ikiwezekana waondolewe na kupelekwa vijijini,” alisema Jafo.

Msanii wa muziki Prince Rogers (1958-2016) afariki dunia



Prince Rogers Nelson enzi za uhai wake.
Mwanamuziki maarufu wa nchini Marekani, Prince Rogers Nelson amefariki dunia jana.
Prince aliyekuwa na umri wa miaka 57 amekutwa na mauti jana katika makazi yake yaliyopo Minneapolis nchini Marekani.
Alizaliwa Juni 7, 1958 na kutawala chati za muziki kote duniani katika miaka ya 1970 na 1980 kwa vibao vyake maarufu kama vile ‘I Wanna Be Your Lover’ na ‘Little Red Corvette’.

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Katika Magazeti

MASHINE YA KUSIMAMISHA MATITI YAINGIA TANZANIA, ANGALIA MADHARA YAKE HAPA

Hii ndiyo mashine ya kusimamishia matiti na hapa ipo kutumika
Hii sayansi na teknologia sasa inatupeleka pabaya. Hivi karibuni wataalam toka china wameleta mashine maalumu ya kunyanyua matiti (yawe na muonekano wa saa 6)

Rais Magufuli Atema Cheche Kuhusu Wanaolalamika Juu ya MAJIPU Anayoyatumbua Hadharani..Angalia Video Hapa




Rais Magufuli leo amekutana na Viongozi wa CCM ngazi za Mikoa na Wilaya kwa lengo la kuwashukuru kwa kazi nzuri walizofanya wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana. 




Katika hafla hiyo, Rais Magufuli ameeleza kusikitishwa kwake na baadhi ya watu wanaowaonea huruma mafisadi ambao wamekuwa wakitumbuliwa hadharani.



Amesema fisadi hastahili huruma kwa sababu yeye wakati wanawaibia wananchi hakuwa na huruma.



"Wapo Wanaodai Tunakiuka haki za Binadamu Kuwatangaza Wanaotumbuliwa.....Wao walikuwa Wanafanya sawa Kuwaibia Hadharani Watanzania? " Amehoji Rais Magufuli.


==> Zaidi Tazama Video hapa Rais Magufuli Akizungumza

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,ushauri na maoni au chochote wasiliana nasi kupitia 0716528779/0755542721

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo ijumaa ya April 22 2016 kwenye,Habari zaUdaku, Kitaifa,kimataifa na michezo.

 April 22 2016 naanza kwa kukuletea habari zote kubwa zilizobebwa kwenye Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye ,habari za kitaifa,kimataifa Michezo na udaku na stori nyingine kali ili ujue kilichojiri duniani.. usiache kukaa karibu kwenye kurasa zetu za mitandao ya kijamiiyaani facebook/tanzaniampyasasablog na twitter@tanzaniampyasasa.

New AUDIO | Walter Chilambo x Raymond - KWETU (Cover) | Download


Salamu TMK - Mfuko (Official Video)


Rihanna - Needed Me (official video)


Chris Brown – ‘Shut Down’(AUDIO)


 

Gallery

Popular Posts

About Us