BUNGE LAANZA KUCHAFUKA | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, March 23, 2016

BUNGE LAANZA KUCHAFUKA

Image result for bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania


SIKU moja baada ya baadhi ya Kamati za Kudumu za Bunge kuhusishwa na tuhuma ya kashfa ya rushwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai amefanya mabadiliko ya baadhi ya wajumbe wa kamati hizo ili kuzingatia mahitaji mapya na changamoto zilizojitokeza baada ya kuunda Kamati hizo Januari mwaka huu.

Mabadiliko hayo yamegusa takribani wenyeviti na makamu wenyeviti wote wanaotuhumiwa kuhusika kwa namna moja ama nyingine na vitendo vya rushwa kama ilivyoripotiwa na moja ya gazeti la kila siku (si HabariLeo).
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano cha Bunge, mabadiliko hayo yamefanywa chini ya kifungu cha 116(3) cha Kanuni za Kudumu za Bunge kinachompatia Spika Mamlaka ya kuteua wabunge na kuunda Kamati mbalimbali za Bunge.
Katika taarifa hiyo, imebainisha kuwa mabadiliko hayo yaliyowagusa pia wenyeviti, makamu mwenyekiti au wote wawili, yatalazimisha kamati hizo zilizoathirika na mabadiliko hayo kufanya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wa kanuni ya 116 (10).
Alitaja kamati zilizoathirika na mabadiliko hayo zitakazohitaji ama mwenyekiti na makamu mwnyekiti au wote kuwa ni Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Kamati ya Nishati na Madini, Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.
Ndugai alitaja wabunge waliobadilishiwa kamati kuwa ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Dk Mary Mwanjelwa anayekwenda katika Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Martha Mlata anayekwenda Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala.
Wengine ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji na Mitaji (PIC), Richard Ndassa na aliyekuwa mjumbe wa Kamati ya PIC, Selemani Zedi ambao wote wamehamishiwa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala.
Aidha, Ndugai alitaja wajumbe wengine wa Kamati kuwa ni aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya LAAC, Victor Mwambalaswa, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Dk Raphael Chegeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya LAAC, Kangi Lugola ambao wote wanahamishiwa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Wabunge wengine waliohamishwa ni aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Margaret Sitta anayekwenda Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mjumbe wa Kamati ya Viwanda, Abdulaziz Abood anayekwenda LAAC na Mjumbe wa Kamati ya Viwanda, Suleiman Nchambi anayehamia Kamati ya Katiba.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Ndugai pia aliwahamisha aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Viwanda Ibrahim Raza anayekwenda Utawala, Sylvestry Koka aliyekuwa Kamati ya Mambo ya Nje na kuhamishiwa Viwanda na Peter Lijualikali aliyekuwa Utawala na kuhamia Kamati ya Huduma za Jamii.
Wabunge wengine ni Profesa Anna Tibaijuka aliyekuwa Kamati ya Sheria Ndogo anayehamishiwa Kamati ya Miundombinu, Dunstan Kitandula aliyekuwa Kamati ya Mambo ya Nje, Ezekiel Maige aliyekuwa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Innocent Bashungwa aliyekuwa Bajeti ambao wote wanahamishiwa Nishati na Madini.
Aidha, katika mabadiliko hayo, wabunge wawili ambao ni Azza Hamad na Zaynab Vullu waliokuwa Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa wamehamishiwa Kamati ya Ukimwi. Wengine ni Shally Raymond aliyekuwa Mambo ya Nje sasa anakwenda PAC, Joseph Selasini aliyekuwa Mambo ya Nje sasa amehamishiwa LAAC, Emmanuel Mwakasaka aliyekuwa LAAC, amehamishiwa Miundombinu na Suleiman Sadick aliyekuwa LAAC amehamishiwa Kamati ya Huduma za Jamii.
Katika mabadiliko hayo, pia wabunge wengine ambao ni Sixtus Mapunda aliyekuwa Ardhi amehamishiwa Ukimwi, Hamoud Jumaa aliyekuwa Kamati ya Ardhi naye amehamishiwa Utawala na Serikali za Mitaa, Wilfred Lwakatare aliyekuwa Ardhi sasa yupo Nishati na Boniphace Getere aliyekuwa Ardhi amehamishiwa Huduma za Jamii.
Wakati Spika akifanya mabadiliko hayo, baadhi ya wenyeviti na makamu wenyeviti wa kamati hizo zilizofanyiwa mabadiliko walituhumiwa kuhusika katika kashfa ya kuomba na kupokea rushwa kwa mujibu wa moja ya gazeti linalotoka kila siku (si HabariLeo), ingawa wahusika wote walikanusha tuhuma hizo.
Wenyeviti wanaotuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo ni Mbunge wa Sumve, Ndassa, Mbunge wa Busega, Dk Chegeni, Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola, Mbunge wa Sumbawanga Aeshi na wabunge wa Viti Maalum Mlata na Dk Mwajelwa.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us