AJABU: Mwanafunzi wa kiume apata ‘Hedhi’ | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Saturday, April 09, 2016

AJABU: Mwanafunzi wa kiume apata ‘Hedhi’


Dunia ina mambo waswahili hawakukosea kusema hili, kila kukicha linaibuka jipya ambalo kwa namna moja ama nyingine linaweza kukuacha mdomo wazi.
Umeshawahi kukutana na mwanaume ambaye hupata siku za mwezi kama kawaida kama wapatavyo wanawake?

Nakukutanisha na George Fellowes ni mwanafunzi wa chuo kikuu mwenye umri wa miaka 22 na anaamini kwamba hata yeye hupatwa na ‘hedhi ya kiume’.

Anasema kuwa ni rafiki wa karibu wa Amber May Ellis jirani yake na hivyobasi hupata uchungu wa hedhi kila mwezi rafikiye anapopata hedhi.

Uchungu huo anasema huwa mkali hadi kulazimika kuchukua likizo ya kuwa mgonjwa.

Akizungumza na Newsbeat George alisema:Nadhani ni swala la kifikra kwa sababu sisi ni marafiki wa karibu sana na tuna hisia sawa.

Katika kipindi cha miaka mitatu iliopita anasema kuwa amekuwa akipata uchungu wa hedhi na ishara hizo ni sawa na zile za wanawake.

“Ninapata uchungu chini ya tumbo langu pamoja na katika kinena.Huwa nahisi vibaya na kuwa na hasira na marafiki wangu wengi. Pia huwa na hisia zenye mhemuko,” alisema.

George anaelezea kwamba wakati alipoanza kupata uchungu miaka mitatu iliopita alitaka ushauri wa daktari wake. Lakini hakukuwa na maelezo hivyo basi alipewa dawa za kumaliza maumivu ya kinena.

-BBC
 
 BOFYA HAPA KUDOWNLOAD APPLICATION YA TANZANIAMPYA NEWS BLOG>>>HAPA<<

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us