USAFIRI WA MABASI YAENDAYO HARAKA DAR ES SALAAM WAGUBIKWA NA CHANGAMOTO LUKUKI | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, May 16, 2016

USAFIRI WA MABASI YAENDAYO HARAKA DAR ES SALAAM WAGUBIKWA NA CHANGAMOTO LUKUKI

Baadhi ya watu wanaotaka kusafiri na mabasi ya yaendayo haraka wakiwa katika kituo cha Posta ya Zamani (Baharini) wakipewa maelekezo kuwa katika kituo hicho mashine za kutolea tiketi zimeleta hitilafu kwa leo.

 Basi la mwendo wa haraka likitoka katika kituo cha Posta ya zamani bila kupakia abiria kutokana na kutokuwepo kwa tiketi kwa sababu ya mashine za kituo hicho kuleta hitilafu ya mtandao wa kutolea tiketi.
AULI za usafiri wa Mabasi yaendayo haraka zimeanza kutozwa leo katika jiji la Dar es Salaam huku kukiwa na changamoto nyingi katika vituo vya mabasi hayo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Afisa Uhusiano wa UDART, Deus Bugaywa amesema kuwa changamoto waliokutana nayo ni baadhi ya vituo kukosa mashine za kukatishia tiketi, mafuriko ya watu katika vituo pamoja na chenji kwa wasafiri wanaotumia huduma hiyo.

Amesema mfumo wa kadi ukianza utaondoa changamoto hiyo kwa wakazi wa Dar es Salaam na mfumo wa tiketi utatumika kwa wale ambao wanaingia katika jiji na kuondoka.

Aidha amesema mfumo huo unatakiwa fedha itakayotolewa lazima usome benki kuu kwa kuonyesha kodi katika tiketi, suala la chenji ni chagamoto kutokana na fedha ya chenji waliokuwa nayo ni milioni sita za sarafu lakini zimeweza kuisha.

Baadhi ya wananchi wanaotumia usafiri wamesema kuwa kuanza kwa usafiri huo umekuwa ni mapema kwa kushindwa kuona changamoto hizo.

Mmoja wa wananchi, Juma Said amesema kuwa wamekwenda kukata tiketi katika kituo na kuambiwa waende kituo kinachofuata hali hiyo ameona kuwa ni usumbufu.

Hata hivyo amesema kuwa mtu mmoja anapata tiketi ndani ya dakika 10 ambapo  ni vigumu kwenda na idadi ya watu kuweza kwenda kwa wakati.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us