Man Fongo awachimba mkwara wa Bongo fleva | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, August 21, 2016

Man Fongo awachimba mkwara wa Bongo fleva

Kwa kasi iliyopo kwenye muziki wa Singeli, ni wazi kwamba unaelekea kuupoteza muziki wa Bongo Fleva kutokana na kasi ya kuenea kwake hapa nchini, jambo linalosisitizwa na mkali anayetesa katika muziki huo, Amani Hamisi ‘Man Fongo’.

Man Fongo ambaye amepachikwa jina la Mfalme wa Singeli, anayesumbua na kibao chake cha Hainaga Ushemeji amesema wasanii wa Bongo Fleva wana kazi kubwa kuhakikisha wanabaki kileleni kutokana na namna muziki wao ulivyopokelewa vizuri na mashabiki.

“Muziki tunaouimba ni wa mtaani ambapo ndiko chimbuko na watu wa uswahilini, kwa sasa huwaambii kitu kuhusu muziki wetu. Nawaambia ukweli kabisa wasanii wa Bongo Fleva, wakaze buti twende sawa au watafute kitu kingine cha kufanya.

“Ujue wao wanaimba vitu vya kubuni wakati sisi tunaimba maisha halisi hasa ya uswahilini kwa masikini wenzetu,” anasema Man Fongo.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us