Shein atangaza kutumbua majipu Zanzibar. | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, April 06, 2016

Shein atangaza kutumbua majipu Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ametangaza hatua za kubana matumizi ya serikali yake, lakini pia akifuata nyayo za Rais John Magufuli kwa kuahidi kukabiliana na vitendo vya rushwa kwa kutumbua majipu ili kuhakikisha haki inatendeka kwa wanyonge kuona wanafaidika na huduma muhimu zinazotolewa na serikali.
Aidha, amesema Baraza lenye mawaziri makini na miongoni mwa majukumu yake makubwa kuhakikisha Zanzibar inajitegemea na kupunguza utegemezi kutoka kwa nchi washiriki wa maendeleo.
Dk Shein alisema hayo wakati akilizindua Baraza la Wawakilishi la Tisa, ikiwa ishara ya kuanza kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba, ikiwemo kuisimamia Serikali na kupitisha matumizi ya fedha za serikali kwa wizara kwa ajili ya mwaka waAliwataka watendaji wa taasisi hizo, ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Bodi ya Mapato (ZRB) kuwa wabunifu zaidi kwa kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato na kupambana na watu wanaokwepa kodi ikiwemo wafanyabiashara.
“Serikali zetu mbili zimeamua kubana matumizi yasiyokuwa ya lazima ambapo sasa tutakuwa tukifuatilia zaidi katika taasisi zinazokusanya kodi kuona kwamba watendaji wake wanakuwa makini zaidi na kuwa wabunifu,” alisema Dk Shein aliyeshinda Uchaguzi Mkuu wa marudio wa Machi 20, mwaka huu.
Kuhusu maadili na utawala bora, alisema atahakikisha kuanza kutumika kwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 8 ya mwaka 2015 ambayo itafuatilia utendaji wa viongozi waliopewa dhamana zao kuona kwamba wanawajibika kikamilifu kwa ajili ya kuleta maendeleo.
Alisema moja ya kazi kubwa atakayoifanya katika kipindi cha miaka mitano ni kuhakikisha Serikali inapambana na rushwa ambayo ni adui wa haki kwa watendaji wa serikali ikiwemo viongozi waliopewa majukumu.
Alisema yapo manung’uniko makubwa kutoka kwa wananchi kwamba wapo viongozi wanaendekeza rushwa na huduma muhimu hazipatikani bila ya kutoa fedha na matokeo yake wananchi kuichukia Serikali yao.
‘Rushwa na vitendo vya aina hiyo ndiyo yanayoitwa majipu.....nitahakikisha tunatumbuwa majipu na kutoa moyo wake hadi kuhakikisha haki inatendeka kwa wanyonge kuona wanafaidika na huduma muhimu zinazotolewa na serikali,” alisema Dk Shein na kuongeza kuwa, “sasa imetosha.”
Alieleza kuwa malengo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ifikapo mwaka 2020 kuyafikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati, utakaoongeza ajira kwa vijana na kuweza kupiga hatua kubwa ya maendeleo.
Alisema hali ya uchumi wa Zanzibar imekuwa ikitoa matumaini makubwa kutoka ukuaji wa uchumi kutoka asilimia 6.6 katika mwaka 2015, na kuwa matarajio makubwa ni kufikia asilimia 8.10 ifikapo mwaka 2020.
K u h u s u maslahi kwa watumishi wa Serikali, alisema ahadi yake aliyoitoa wakati wa mikutano ya kampeni ya kuongeza kima cha chini cha mishahara ya wafanyakazi wa SMZ kufikia Sh 300,000 ipo pale pale na ataitekeleza.
Aidha, alisema alitoa ahadi kwa wapiganaji wa vikosi ya Idara maalumu za Serikali kuongeza viwango vya mishahara kulingana na wenzao wa Serikali ya Muungano kwamba atazitekeleza katika mwaka wa fedha kulingana na hali ya makusanyo ya kodi.
Hata hivyo, alisikitishwa na tatizo la wafanyakazi wengi wa SMZ kushindwa kuwajibika ipasavyo huku wale wenye majukumu ya kutoa huduma kwa wananchi wakiyakwepa na kupelekea wananchi kuichukia Serikali.
Alisema katika Serikali atakayounda haitovumilia wafanyakazi watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria za utumishi na kusema wafanyakazi wa aina hiyo watawajibishwa kwa kufukuzwa kazi.
“Hatutawavumilia wafanyakazi wa serikali waliopewa jukumu la kutoa huduma na kushindwa kutekeleza majukumu hayo......mshahara unatokana na jasho la kazi unayoifanya kwa hivyo wafanyakazi wazembe tutawafukuza,” alisema Dk Shein.
Aidha, alitangaza neema kwa wakulima wa zao la karafuu zaidi katika kisiwa cha Pemba na kusisitiza kwamba faida ya asilimia 80 wanayoipata, itaendelea kuwepo huku wakulima hao wakipewa motisha ya kuimarisha mashamba ya karafuu na vitalu vya miche hiyo.
Aliwakumbusha Wazanzibari kuwa uchaguzi umekwisha na kazi kubwa iliyopo sasa ni wananchi kujenga nchi na kuimarisha umoja na mshikamano ambao ndiyo malengo ya serikali yanayotokana na utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Alisema Chama Cha Mapinduzi CCM ndiyo kilichopewa ridhaa ya kuongoza nchi kutokana na kukubalika kwa Ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka 2015-2020 kwa hiyo viongozi wanatakiwa kubeba jukumu hilo kwa kufanya kazi na kuweka pembeni itikadi za kisiasa.
Alisema ataendelea kuwa muumini wa umoja na utulivu wa Wazanzibari wote huku akisisitiza kuwaunganisha wananchi wote wa Zanzibar kwa kuongoza nchi bila ya chuki, jazba au uonevu kwa itikadi za kisiasa, lakini hatamvumilia yeyote atakayeibeza Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 akiapa kupambana naye kwa nguvu zote.
Alisema hana mbadala wa Muungano na kuahidi kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais John Magufuli kuleta maendeleo na kupambana na umasikini wa wananchi kwa kufuata Ilani ya CCM. fedha wa bajeti.
Alisema Serikali itachukua hatua za kubana matumizi yasiyokuwa na lazima na kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato kutoka katika vyanzo vyake na kusimamia taasisi zilizokabidhiwa jukumu hilo kuona ufanisi unapatikana.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us