Al-Shabab lakiri kutekeleza shambulio Mandera Kenya | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, June 21, 2016

Al-Shabab lakiri kutekeleza shambulio Mandera Kenya

al-Shabab

Kundi la wapiganaji wa kiislamu nchini Somalia al-Shabab, limekiri kutekeleza shambulio lililotokea Jumatatu asubuhi nchini Kenya, ambapo askari watano waliuawa.

Shambulizi hilo linaloaminika kutekelezwa na roketi na kulenga gari ya polisi aina ya Land Cruiser lilitokea kilomita chache kutoka mji wa Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya.

Mji wa Mandera uko mita chache kutoka mpaka wa Kenya na Somalia.

Radio Andalus iliyoko nchini Somalia, imetangaza kuwa, shambulizi hilo ni kuipa Kenya adabu ya kuwatuma wanajeshi wake nchini Somalia.

Kenya ina vikosi vyake vya kijeshi nchini Somalia chini ya muungano wa Afrika AMISOM.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us