GIGY MONEY AELEZA JINSI MWARABU WAKE ALIVYOMSITIRI | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, June 20, 2016

GIGY MONEY AELEZA JINSI MWARABU WAKE ALIVYOMSITIRI

IKIWA imepita wiki moja tangu ‘muuza nyago’ kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ kugundulika kuwa ameangukia katika penzi la mwanaume wa Kiarabu aishiye Dubai, Aziz, staa huyo amefunguka kuwa amemsitiri vitu vingi.
Akizungumza na mwandishi Gigy ambaye pia ni Mtangazaji wa Choice FM katika Kipindi cha Admin alisema kuwa kila binadamu anapangiwa mtu sahihi wa kuishi naye na kwamba kuangukia kwenye penzi na Mwarabu huyo kumemfanya kuachana na mambo mengi aliyokuwa akiyafanya kama kujianika kihasara katika mitandao ya kijamii na kutoa lugha chafu hovyo.
“Kiukweli kabisa, Aziz (Mwarabu) amenisitiri sana, zamani ulikuwa hunikuti hivi, japokuwa yupo mbali (Dubai) lakini kila siku nachati naye, ananipigia simu na anahakikisha sifanyi mambo ya kijinga,” Alisema Gigy.
Gigy anayedaiwa kutoka na msururu wa wasanii wa Bongo Fleva wakiwemo Ommy Dimpoz, Rich Mavoko, Alikiba na Hemed PHD alimnasa Mwarabu huyo miezi sita iliyopita kupitia Instagram ambapo walianza kwa kutumiana picha kisha namba za simu.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us