Kauli ya Nay wa Mitego Baada ya “Pale Kati Patamu” Kufungiwa Na BASATA | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, July 19, 2016

Kauli ya Nay wa Mitego Baada ya “Pale Kati Patamu” Kufungiwa Na BASATA

Ni siku chache tu zimepita baada ya hit maker wa nyimbo ya “Shika Adabu Yako” Nay wa Mitego kuachia nyimbo yake mpya inayokwenda kwa jina la “Pale Kati Patamu”

Nyimbo ambayo imezua gumzo kubwa mtaani kwa kile kinachozungumzwa kuwa nyimbo hiyo haina maadili. Gumzo zilianza mapema baada ya picha za kava za nyimbo hiyo kutoka kabla nyimbo hiyo haijaachiwa rasmi ikiwa baadhi ya picha hizo ziliwaonyesha wadada wakiwa watupu (Hawaku vaa nguo).

Jumamosi ya July 16 Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) lilitoa tamko rasmi kuwa wameifungia nyimbo hiyo kwa sababu za ukosekanaji wa maadili katika nyimbo hiyo. Perfect255 imemvutia waya Nay wa Mitego (Imempigia simu) na kumuuliza juu ya swala hilo. Na haya ndio majibu ya Nay Wa Mitego.

“Nimeona hivyo vitu na ndio nataka nivifuatilie kwa sababu mimi sijatoa video ya huu wimbo na kava ya huu wimbo ni kava ambayo mimi nime ipost katika ukurasa wangu wa Instagram ambapo ndipo ninapatumia kwa ajili ya ku promote muziki wangu, vitu vingine tofauti havihusiani na mimi kabisa. Nina imani hawana matatizo tutakaa tutaelewana kwasababu nina imani ni watu waelewa, nitafuata utaratibu unao stahili nadhani nitajua nini cha kufanya baada ya hapo. Nahitaji wimbo wangu urudi na mashabiki zangu waendelee kuusikia.”

Nay Wa Mitego aliweka wazi kuhusiana na mipango aliyokuwa akiipanga kufuatana na wimbo huo kuwa ana mipango ya kushuti video nne kwa wimbo huo na hadi sasa tayari amekwisha kamilisha video mbili ambazo moja ameifanyia South Afrika na nyingine ameifanyia hapa hapa nyumbani.

“Wimbo wa Pale Kati utakuwa na video nne, na tayari nimesha shuti Video moja South Afrika na nyingine nimefanya hapa nyumbani, nimetumia gharama nyingi sana kufanya promotion ya Audio, hizi gharama zinapoteaje!? Mimi ni kijana ambaye nimejiajiri kupitia muziki” Alisema Nay wa Mitego.

BONGOSWAGGSS

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us