Mamia kupigwa picha za utupu Uingereza | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, July 10, 2016

Mamia kupigwa picha za utupu Uingereza


TunickImage copyrightAFP
Image captionTunick anasema hiyo ni sanaa halisi
Mamia ya watu watavua nguo zao na kupigwa picha wakiwa tupu kusherehekea utamaduni katika mji wa Hull, Uingereza.
Tukio hilo litakuwa la kusherehekea mji huo kama Mji wa Utamaduni.
Washiriki watapakwa rangi ya samawati Jumamosi na kisha wapigwe picha wakiwa katika maeneo mashuhuri jijini humo kama sehemu ya mradi uliopewa jina Sea of Hull.
Mradi huo unatekelezwa na mpiga picha Spencer Tunick na unadhaminiwa na taasisi ya Sanaa ya Ferens Art Gallery.
Picha zitakazopigwa zitawekwa na kuoneshwa kwa umma wakati wa tamasha ya sanaa ya 2017 itakayoendelea kwa mwaka mmoja.
Tunick, anayetoka New York, amewahi kufanya kazi kama hiyo kwingine.
Amewahi kupiga picha za watu wengi wakiwa uchi Sydney Opera House, Place des Arts mjini Montreal, Mexico City na mjini Munich nchini Ujerumani Germany.
Bw Tunick amesema kazi zake “hugusia historia ndefu ya Sanaa ya utupu”.
"Mavazi ni Sanaa ya mtu mwingine,” anasema.
“Fashoni ni Sanaa. Kwa kuondoa hilo (mavazi), nitakuwa nafanya kazi na usawa na maumbile katika umaridadi wake.”
New YorkImage copyrightAP
Image captionWatu wakipigwa picha wakiwa uchi New York
Watu karibu 2,000 wamejiandikisha kupigwa picha tangu wazo hilo litangazwe mwezi Machi.
Baraza la mji wa Hull limesema baadhi ya barabara zitafungwa wakati wa shughuli hiyo Jumamosi asubuhi.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us