Msemaji wa Yanga Jerry Muro Afunguka Baada kufungiwa Kujishughulisha na Soka Tanzania. | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Friday, July 08, 2016

Msemaji wa Yanga Jerry Muro Afunguka Baada kufungiwa Kujishughulisha na Soka Tanzania.


Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Yanga Jerry Muro jioni ya July 7 2016 ameingia kwenye headlines baada ya shirikisho la soka Tanzania TFF kupitia kamati ya maadili, kutangaza kumfungia mwaka mmoja kujihusisha na soka na faini ya Tsh milioni 3.

Jerry Muro amefungiwa na kamati ya maadili kwa makosa mawili, moja alilifanya mwaka 2015 la kukaidi kulipa faini ya Tsh milioni 5 iliyoamuliwa kulipa na kamati ya nidhamu baada ya kufanya makosa, kosa ambalo limemfanya afungiwe mwaka mmoja kujihusisha na soka.

Kosa la pili ni kutuhumiwa kuchochea vurugu kuelekea mchezo wa Yanga wa Kombe la shirikisho dhidi ya TP Mazembe uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam, baada ya hukumu hiyo Jerry Muro ameongea haya:

“Taarifa hizo nimezisikia japo kwa sasa nipo kijijini Machame kwa ajili ya likizo yangu, nimesikia watu wameandika kwenye mitandao kuwa nimefungiwa, lakini mimi nipo Machame na maamuzi yao yametoka nikiwa likizo Machame, yaani wametoa hukumu kwa kusikiliza upande mmoja”

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us