Bungeni: Serikali yaanza Kuzipanga Shule Katika Makundi ili Kuweka Viwango vya Ada Elekezi | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Thursday, April 21, 2016

Bungeni: Serikali yaanza Kuzipanga Shule Katika Makundi ili Kuweka Viwango vya Ada Elekezi


Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, imeanza zoezi la kupanga shule katika makundi ili kuweka viwango vya ada kwa kuzingatia ubora wa huduma na kwamba haitaathiri ubora wa elimu.

Naibu Waziri wa wizara hiyo, Stella Manyanya, aliyasema hayo wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema). 

Mdee alitaka kufahamu iwapo Serikali imebaini kiwango cha gharama kwa kila mwanafunzi kwa shule za bweni na kutwa, iwapo hakitasababisha kuporomoka kwa ubora wa elimu.

Manyanya alisema wizara hiyo imefanya utafiti kuhusu gharama za kila mwanafunzi wa elimu ya msingi na sekondari. 

“Baada ya utafiti, wizara yangu ilifanya mazungumzo na baadhi ya taasisi zinazosimamia elimu kwa shule zisizokuwa za Serikali na kukubaliana jinsi ya kufikia viwango vya ada elekezi,” alisema.

Alisema wizara inatarajia ubora wa ada elekezi hautaathiri elimu kwa shule binafsi, kwa sababu itapangwa kulingana na ubora wa miundombinu ya shule.

Katika swali la nyongeza, Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (Chadema) alitaka kufahamu jinsi Serikali inavyotaka kupanga bei elekezi wakati imeifanya elimu kuwa biashara.

Manyanya alisema siyo mara ya kwanza kwa Serikali kupanga bei elekezi kwa faida ya wananchi na kwamba, imefanyika kwa upande wa huduma ya maji hivyo Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (Ewura) wamefanya.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us