EWURA YASHUSHA BEI YA UMEME KUANZIA LEO,SERVICE CHARGE YAZIKWA. | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Saturday, April 02, 2016

EWURA YASHUSHA BEI YA UMEME KUANZIA LEO,SERVICE CHARGE YAZIKWA.





Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji EWURA imetangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.



Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kutaka bei za umeme zipunguzwe sambamba na hilo gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa.


Bei mpya kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292 toka 298 ya zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200 ya hapo awali.

Bei mpya kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152 toka sh. 156 ya hapo awali


Tazama jedwali hili kuona mgawanyo wa bei mpya.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us