MAGUFULI KUFUATA NYENDO ZA EDWARD MORINGE SOKOINE | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, April 12, 2016

MAGUFULI KUFUATA NYENDO ZA EDWARD MORINGE SOKOINE


Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya awamu ya 
 Aliyekuwa waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza Hayati ndg.Edward Moringe Sokoine.
Ni wazi kwamba kila siku zinavyozidi kwenda utendaji wa kazi za Rais John pombe Magufuli unazidi
kupata umaarufu,Umaarufu umeanza kuja hivi karibuni ni baada ya kuanzisha operesheni ya kutumbua majipu yaani kuwawajibisha wafanyakazi wasio waadilifu katika nyazifa zao.

Hali hii inakumbusha enzi zile za utawala wa awamu ya kwanza chini ya waziri mkuu wa nyakati hizo Hayati Ndugu Edward Moringe Sokoine akiwa madarakani katika serikali ya awamu ya kwanza ikiongozwa na Hayati baba wa Taifa JK.Nyerere

Leo ni kumbukumbu ya miaka kadhaa ya kifo cha Waziri mkuu ndugu Edward Moringe Sokoine kufuatia ajali ya gari aliyoipata katika eneo la Wami dakawa mkoani morogoro.

Ni Waziri mkuu ambaye mpaka kesho ataendelea kukumbukwa kwa mambo mabalimbali aliyokuwa akiyapigania,Marehemu Sokoine atakumbukwa kwa mambo mengi yakiwemo ya  kupiga vita mambo mbalimbali yakiwemo,wahujumu uchumi,Mafisadi, Wala rushwa,na watumishi wazembe kazini.wakwepa kodi na wengineo.

Leo hii tunamuona Rais john pombe magufuli akiendeleza vita dhidi ya mambo mbalimbali yanayochangia kudidimiza uchumi wa taifa hili la Tanzania,Ni dhahiri anafata nyendo za Hayati Sokoine katika harakati zake za kutumbua majipu serikalini na kwenye sekta mbalimbali za uchumi wa taifa la Tanzania.


Amefanya hayo ni baada ya kuwawajibisha watumishi mbalimbali waliokuwa wakikiuka maadili ya uongozi na kutumia ofisi za umma kwa kujinufaisha wao bila kujali maslahi ya taifa,uchumi na wananchi waliowapa nafasi hizo.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us