Rais wa ZANZIBAR azindua Baraza la Wawakilishi | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, April 05, 2016

Rais wa ZANZIBAR azindua Baraza la Wawakilishi


Rais wa ZANZIBAR na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. ALI MOHAMED SHEIN amehutubia baraza la wawakilishi na kueleza mikakati ya serikali yake
Rais wa ZANZIBAR na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. ALI MOHAMED SHEIN
Rais wa ZANZIBAR  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. ALI MOHAMED SHEIN amehutubia baraza la wawakilishi na kueleza mikakati ya serikali yake katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Miongoni mwa mambo ambayo Dkt.SHEIN ameyataja kuwa ni kipaumbele cha serikali yake ni kuwekeza katika sekta ya viwanda na kutafuta masoko kwa mazao ya bahari huku akiahidi kuwachukulia hatua wafanyakazi wazembe.

Akizungumzia suala la uchumi Rais wa ZANZIBAR amesema serikali yake itahakikisha uchumi unakua kwa kuwekeza katika sekta ya viwanda na kutafuta masoko ya mazao ya bahari.

Amewataka wajumbe wa Baraza la Wawakili kushirikiana na viongozi mbalimbali katika maeneo yao ili kutatua migogoro ya ardhi inayowakabili wananchi.

Dkt SHEIN amesema muswada ya sheria kuhusu rasilimali ya mafuta na gesi  uko tayari na unatarajiwa kuwasilishwa katika baraza hilo kwa ajili ya majadiliano.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us