Yanga kutesa nyasi na Al Ahly jijini Dar | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Friday, April 08, 2016

Yanga kutesa nyasi na Al Ahly jijini Dar


Yanga Yanga watakutana na Al Ahly uwanja wa taifa Dar es Salaam
Klabu ya Young Africans itashuka dimbani kesho Jumamosi kucheza dhidi ya miamba wa Misri Al Ahly hatua ya 16 bora katika Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL)
.
Mechi hiyo itachezewa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuanzia saa 10 kamili kwa saa za Afrika Mashariki.
Kocha wa Yanga Hans van der Pluijm, akizungumza awali, alikuwa amesema atahakikisha wanafanya maandalizi mazuri kuweza kuikabili vilivyo timu ya Al Ahly.
Yanga na Azam FC ndio wawakilishi pekee wa Tanzania waliosalia katika michuano.
Azam FC watashuka dimbani Jumapili katika uwanja wa Azam Complex uliopo saa 9 alasiri, kuwakaribisha wenyeji wa Esperance Sportive de Tunis (EST) ya Tunisa.
Kamisaa wa mchezo akiwani Joseph Nkole kutoka nchini Zambia.
Michezo ya marudiano itachezwa Aprili 19-20 mwaka huu.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us