Msanii Diamond Platnumz atoa msaada kwa wanafunzi 1800 jijini Dar es salaam | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, June 06, 2016

Msanii Diamond Platnumz atoa msaada kwa wanafunzi 1800 jijini Dar es salaam

e

Msanii Diamond Platnumz akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda

Msanii Diamond Platnumz na uongozi wake siku ya Ijumaa kwenye kipindi cha Friday Night Live alitoa ahadi kuwa Jumatatu watapeleka zawadia kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kwa ajili ya watanzania.

Na leo hii msanii huyo ametimiza ahadi hiyo kwa kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa madawati 600 ya wanafunzi ambayo yatasaidia takribani ya wanafunzi 1800 katika jiji la Dar es Salaam ambao walikuwa wanakaa chini.

"Mapema leo na familia nzima ya WCB wasafi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda tulivyoenda kumkabidhi Madawati 600 kwajili ya Wanafunzi wa shule za Dar es Salaam. Madawati hayo ambayo yataweza kusaidia Wanafunzi elfu moja na mia nane kutoka kwenye kukaa chini na kuweza kukaa kwenye dawati na kupata elimu Vyema" alisema Diamond Platnum



google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us