KIONGOZI WA ISIS AKIRI KWAMBA WANAFADHILIWA NA UTAWALA WA OBAMA | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, July 11, 2016

KIONGOZI WA ISIS AKIRI KWAMBA WANAFADHILIWA NA UTAWALA WA OBAMA

Kiongozi wa ISIS kwa jina Yousef al-Salafi kutoka Pakistan amekubali kwamba kundi lao la ISIS linafadhiliwa na Marekani, kutoka utawala wa Obama. Habari hii ilikuja kutoka serikali ya Pakistani mara baada ya kuhojiana na Yousef na kupokea taarifa hii.
Chanzo kilichofanya uchunguzi wa siri kilisema:
Wakati wa uchunguzi,Yousaf al Salafi alibainika kuwa alikuwa akipata fedha kutoka Marekani- kuendesha hiki kikundi nchini Pakistan na kuwaajiri vijana wengi kwenda kupigana nchini Syria.
Chanzo kimoja kinasema kuwa Yousaf al Salafi amekiri mwenyewe kuwa mshirika-akisema yeye ni imam-alikuwa akilipwa na Marekani kuwaajiri vijana wengi hili kujiunga na ISIS kwa kuwapa $600.
Chanzo hiki pia kimesema:
Marekani imekuwa ikilaani shughuli za IS lakini kwa bahati mbaya imeshindwa kujizuia kuwafadhili.Marekani inawatumia IS kwa maslahi yake binafsi na imejaribu kukishambulia kikundi hiki kilichopo Iraq ila imeshindwa kabisa kuzuia maasi yanayofanywa na kikundi hiki nchini Syria.
Utawala wa Obama kuwafadhili ISIS, sio kitu cha kushangaza, Hebu tujikumbushe kwamba utawala wa Obama umekataa kuiunga mkono Misri katika uharibifu uliofanywa na ISIS, hata hivyo inafanya kazi na Uturuki ambao ni moja ya waunga mkono wakubwa wa ISIS.Pia tusisahau ya kuwa Marekani inawasaidia FSA na inaendelea kuvifadhili vikundi vya jihad ili kupigana na serikali ya Assad, mapigano yanayowahusisha waislamu tu, na hatimaye hili Uturuki iweze kutawala Mashariki ya Kati.
Kweli duniani kwa sasa inatawaliwa na shetani, na wengi kati ya watu wenye nguvu duniani wanaingiliwa na mapepo,wanavyofanya vitu kwa upande wao wanajiona wapo sahihi, na kwa kiasi kikubwa wanakubaliana na maovu yote yanayoiandma dunia.
Kuanzia madawa ya kulevya, magaidi, mauaji ya watoto wasio na hatia, hadi agenda ya mashoga, uovu tunaouona kwa sasa machoni petu unawezeshwa zaidi na watu waovu waliopewa nguvu na umma, wakijifanya wema wamevaa suti na wana tabasamu zuri.
Watu wengi wanafikiria ugaidi ni uovu pekee mbaya, ila ukweli ni kwamba watu wengi wenye ushetani ndani yao wanafanya matukio mabaya sana nyuma ya pazia, wakielekeza kwa siri, na wana nguvu maana wapo madarakani.
Hebu tukumbuke kwamba George Bush ambaye alimtoa Saddam madarakani, aliyekuwa anawakandamiza jihad na kuwalinda wakristo, kitu ambacho Bush alifanya ni kutengeneza mazingira kwa ISIS kuvamia mashariki ya kati na kusababisha matatizo makubwa na machafuko yaliyogharimu maisha mengi ya wasio na hatia.
Ukweli unabaki kwamba Marekani inasaidia mateso yote wanayopata Wakristo katika Mashariki ya Kati, na lengo lake kubwa ni kuwatumia wanajihadi: kuharibu ukristo wote mashariki ya kati.
Huyu kamanda wa ISIS ambaye yupo nchini Pakistan, ambapo anafanya kazi kuunda sharia state katika nchi ya Pakistan,ambayo utaleta uharibifu mkubwa wa ukristo nchini humo.
Inatupasa wote wenye mapenzi ya dhati na utu wa binadamu kutoa sauti zetu juu ya vitendo viovu wanavyofanyiwa watu wasio na hatia yeyote duniani. Kuna idadi kubwa ya watu wanauliwa na wanateswa kijinsia na wengine wanauzwa kwa ajili ya maslahi ya wale waovu.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us