Picha chafu zavuja na kuvunja ndoa ya wiki moja! | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, July 20, 2016

Picha chafu zavuja na kuvunja ndoa ya wiki moja!


Mwanamke huyo akijiachia ‘kimalovee’ na boyfriend wake wa zamani.

DUNIA ina maajabu! Mwanamke mmoja (jina halijajulikana mara moja) amejikuta akivunja ndoa yake ya wiki moja baada ya picha zake za utupu akijiachia ‘kimalovee’ na boyfriend wake wa zamani kumfikia mume wake wa ndoa wakati wakiwa fungate (honey-moon) baada ya ndoa yake na mumewe iliyofanyika jijini Dar es Saalam.

Tukio hilo la aibu limetokea wiki moja tu baada ya wawili hao kufunga pingu za maisha. Kupitia ujumbe wa sauti mwanamke huyo amedai kuwa picha hizo alijipiga na mpenzi wake zamani miaka saba iliyopita wakiwa chuoni.


Akiongea kwenye Ripoti ya Siku ya kipindi cha Ubaoni cha EFM kilichoruka Ijumaa iliyopita, mwanamke huyo amedai kuwa picha hizo zimedhamlilisha mno kiasi cha kuiharibu ndoa yake, kuwaumiza ndugu zake na kuwakosea heshima wakwe zake na kwamba anajuta kupita kiasi.

“Ni kweli ni mimi ndiye niliyepiga hizo picha lakini ni muda mrefu tangu kipindi nikiwa chuo, yaani hata huyo mtu mwenyewe sijui yuko wapi sina mawasiliano naye tena, sikutegemea kiukweli,” anasema mwanamke huyo.


“Ni kitu ambacho kinaniuma na kimeniharibia mlolongo mzima wa maisha yangu, mpaka sasa hivi sielewi, mume wangu hawezi kunielewa tena na yeye ndio nimemwekea kama nguzo, ndio kila kitu kwasababu hata familia yangu hainielewi ,” ameongeza.

“Mpaka sasa hivi sijui nafanya nini.”

Kwa upande wa mume wake, alidai kuwa picha hizo zimeuvunja moyo wake.

“Tulikuwa tumeshaenda kwenye honey moon tumerudi, sikuamini macho yangu baada ya kuona hizo picha na huyu mwanamke, rafiki zangu walikuwepo wengi sana, best man wangu pia ni vitu ambavyo kuvizungumza mimi nashindwa, naanzia wapi, lakini mapenzi huwa yako hivyo, inawezekana iko hivyo lakini sasa kama mazingira kama yale hata kama ukiwa ni wewe lazima utaumia, familia yangu ntaiambia nini mimi, imenigharamia harusi kubwa,” alisema mwanaume huyo.

Amedai kuwa haoni kama inawezekana tena kukaa chini na mke wake huyo kwa kile kilichotokea.
“Nikae chini ili iweje?” alihoji kwa jazba. “Imeniuma, imeniumiza sana hii kitu haki ya Mungu, hata kama miaka kumi imepita kwanini imekuja kwenye harusi yangu, zawadi zimekuja kwaajili ya harusi yetu kwanini aletewe picha za aina hiyo? Angeniambia before kwamba nilikuwa na moja mbili, ningekuwa najua, lakini amenificha. Imenicost kwa kiasi kikubwa sana, nitaiambiaje familia yangu kwa mfano? Nitasema nini.”

“Sitokuja kupenda tena mwanamke wa aina yoyote ile, mpaka nakuja kuingia kaburini, I swear to God, imetosha kabisa.”

Wawili hao walifunga ndoa tarehe April 23 mwaka huu.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us