Airlander 10: Ndege ndefu zaidi duniani yapata ajali | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, August 24, 2016

Airlander 10: Ndege ndefu zaidi duniani yapata ajali

 Ndege ndefu zaidi duniani - Airlander 10 - imeharibika baada ya kuanguka ikitua kwenye safari yake ya pili ya kufanyiwa majaribio.

Ndege hiyo ya urefu wa 302ft (92m) - ambayo kwa kiasi fulani ni ndege na pia kwa kiasi fulani puto - iliharibika ikiwa katika uwanja wa Cardington, Bedfordshire nchini Uingereza.

Ndege hiyo ya thamani ya £25m imeharibika eneo wanamoketi marubani baada ya kuangika kwa 'pua' mwendo wa saa tano saa za Uingereza.

Ndege ndefu zaidi hatimaye yapaa Uingereza

Msemaji wa HAV, kampuni iliyounda ndege hiyo, amesema marubani na wahudumu wengine wote wako salama.

Kampuni hiyo imekanusha madai kwamba waya uliokuwa umening'inia kutoka kwenye ndege hiyo ulikwama kwenye kigingi cha nyaya za simu na kusababisha ajali hiyo.
Ndege hiyo ilifanya safari yake ya kwanza 17 Agosti.

 Kampuni ya HAV inapanga kuunda ndege 10 aina ya Airlander kufikia mwaka 2021.

 Airlander 10 kwa takwimu
44,100 lbs (20,000kg): Uzani wa ndege hiyo

20,000ft (6,100m): Umbali ambao inaweza kupaa juu angani

80 knots (148km/h): Kasi yake ya juu zaidi

Siku 5: Muda ambao inaweza kukaa angani

22,050 lbs (10,000kg): Uzani ambao inaweza kubeba



google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us