UDOM kuongeza wataalam wa shahada ya mafuta na gesi | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, August 24, 2016

UDOM kuongeza wataalam wa shahada ya mafuta na gesi

Chuo Kikuu cha UDOM kimeandaa mtaala wa elimu kwa ajili ya shahada ya uzalimili katika sekta ya mafuta na gesi ili kutoa watalaam wengi zaidi wa masuala ya athari za kimazingira zinazoweza kusababishwa na uchimbaji wa rasimali hiyo.

Kaimu Makamu mkuu wa chuo hicho Dkt. Peter Msofe amesema hayo mjini Dodoma katika uifunguzi wa mkutano wa wadau wa elimu kutoka nchi za Uganda na Tanzania wanaoandaa mtaala wa unaolenga kuzinufaisha nchi mbalimbali za Afrika.

Dkt. Msofe amesema kuwa mtaala huo umekuja wakati muafaka wakati Tanzania imegundua gesi nyingi hivyo kuna uhitaji wa watalaam ambao wataweza kujua faida na athari za rasimali hiyo kimazingira na kiafya nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo cha Sayansi Asilia na Hisabati Said Ali Vuai, amesema kuwa mtaala huo unatarajiwa kuanza katika mwaka wa masomo 2017/2018.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us