Mo Dewji akabidhi barua yake Simba, kununua hisa asilimia 51 | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, August 01, 2016

Mo Dewji akabidhi barua yake Simba, kununua hisa asilimia 51

Mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji.

Mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji amesema tayari ameandika barua kwa uongozi wa Simba kueleza kuhusiana na uamuzi wake wa kutaka kununua hisa za Simba kwa asilimia 51.

Mo amesema ameandika barua hiyo leo asubuhi baada ya kusikia baadhi ya viongozi wa Simba wakisema hakuwa amefanya hivyo.

“Kweli hatukuwa tumeandika barua kwa kuwa nilitaka mchakato uchukue hatua. Baada ya hapo lingefuata suala labarua, lakini kwa kuwa wanasema lazima barua, basi acha tufanye hivyo.

“Tayari barua imeandikwa na imepelekwa kwenye klabu, kukawa hakuna mtu na sasa imepelekwa ofisini kwa Aveva,” alisema Mo.

“Nilichoeleza kwenye barua yangu ni kilekile kwamba ninatoa ofa ya Sh bilioni 20 ili kupata hisa asilimia 51. Niko tayari kushirikiana na uongozi wakati wa mchakati kama ambavyo nilieleza awali,” alisema.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us