Mtoto wa OBAMA arekodiwa Akivuta Bangi | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Thursday, August 11, 2016

Mtoto wa OBAMA arekodiwa Akivuta Bangi

Mtoto mkubwa wa Rais Barack Obama – Malia Obama – anahisiwa siku kadhaa nyuma alikuwa amepewa kipisi cha bangi kuvuta na akavuta na kujikuta akirekodiwa na video za mapaparazi wa Marekani. Tukio hilo limekuja siku chache tu baada ya video nyingine kumuonesha binti huyo akikata viuno kwenye moja ya matamasha ya muziki huko Marekani.

Inasadikiwa Malia alivuta sigara hiyo ‘haramu’ kwenye tamasha la lollapalooza kwenye Jiji la Chicago, jimbo la Illinois ambalo ni jimbo la nyumbani kwa Rais Obama. Mmoja wa wahudhuriaji wa tamasha hilo Jerrdin Selwyn mwenye umri wa miaka 18 alidai kuwa alimkuta Malia akiwa anavuta ganja na marafiki zake na hakukuwa na shaka ya hilo kwani harufu ya bangi ilikuwa wazi
“Kulikuwa na kijana mmoja pale ambaye alikuwa anavuta na akampasia Malia ambaye alishikilia kama kwa dakika moja kisha akampatia mtu mwingine” alidai binti huyo. Na alidai pia kuwa alikuwa na picha zinazoonesha mtoto huyo wa Rais wa Marekani akivuta bangi hiyo

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us