Mwigulu Nchemba Awaonya Polisi Wanaowabambikiza Kesi Raia | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, August 10, 2016

Mwigulu Nchemba Awaonya Polisi Wanaowabambikiza Kesi Raia

Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba amewaambia askari wa jeshi la Polisi mkoani Katavi kufanya kazi kwa taratibu na sheria bila kumuonea mtu yeyote hasa wanyonge.

Waziri Mwigulu ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kutembelea makazi ya watanzania wapya pamoja na kuzungumza na askari wa jeshi la polisi, Magereza pamoja na Uhamiaji.

Mhe. Mwigulu amesema kuwa Askari hao waondokane na tabia ya matukio ya kuwabambikizia kesi raia kwa maslahi binafsi na kuwaonea na kusema kuwa serikali kali ya awamu ya tano haitamfumbia macho askari atakayebainika kufanya hivyo.

Aidha Waziri Mwigulu amechukua fursa hiyo kuwapa hamasa Askari hao kwa kusema kuwa serikali itawaboreshea maslahi yao kadri bajeti itakavyoruhusu ili waweze kufanya kazi kwa weledi zaidi.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us