Madereva wa vigogo walia na agizo la Rais Magufuli kurejesha fedha za Mwenge | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, October 16, 2016

Madereva wa vigogo walia na agizo la Rais Magufuli kurejesha fedha za Mwenge

Madereva na Wasaidizi wa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya mbalimbali nchini ambao walikuwa tayari wamefika Mkoani Simiyu kushiriki sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wameeleza kuumizwa na agizo la kurejesha fedha za kujikimu ambazo kiasi walizitumia kwa shughuli husika.

Walisema kuwa agizo hilo la Rais John Magufuli kwao limewatengenezea tatizo lingine la kiuchumi kwani liliwafikia kwa kuchelewa.

Baadhi yao wamesema kuwa wao hawana uwezo wa kurejesha fedha hizo kwani hawakuomba kufanya safari hizo bali ilikuwa sehemu ya kazi zao na kiasi cha fedha hizo walizitumia kama walivyokubaliwa na ofisi kuwawezesha kufika na kuishi katika eneo hilo.

”Sisi hatukuomba kuja Bariadi kwenye sherehe za Mbio za Mwenge wa Uhuru. Tuliambiwa kuja na tukapewa fedha ambazo tumezitumia kwa mujibu wa mahesabu ya matumizi tuliyoandikiwa kwa sababu ilibidi tule na kulala kwenye nyumba za wageni. Hapo sisi kosa letu liko wapi?” Alihoji mmoja kati ya madereva aliozungumza na gazeti la The Citizen.

Alisema kuwa anadhani uamuzi wa wao kurejesha fedha zote ambazo tayari wamezitumia hautawatendea haki kutokana na matumizi husika waliyofanya.

Naye msaidizi wa Mkuu wa Mkoa mmoja ambaye hakutaka kutajwa, alisema kuwa yeye hataweza kurejesha fedha hizo kwa sababu baada ya kufika Bariadi alilazimika kulipia chumba siku 7 alizopaswa kukaa hapo kutokana na upungufu wa vyumba.

”Ilinibidi nimlipe mwenye chumba gharama zote za siku 7 ambazo nilitarajiwa kuishi hapa kama nilivyotumwa kwa sababu ya uhaba wa vyumba hapa. Sasa naanzaje kumwambia mwenye anirudishie pesa yangu yote ili nirejeshe ofisini?” Alihoji.

Hata hivyo, wakati wasaidizi wa vigogo hao wakionesha kuchanganyikiwa na agizo hilo ambalo wanaamini sasa linaweza kuwaingiza hasara ambayo imetokana na kutumwa wafanye wajibu wao, baadhi ya wakuu wa mikoa tayari wameshaanza kurejesha fedha hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ni mmoja kati ya wakuu hao wa mikoa walioweka wazi mbele ya waandishi wa habari kusitisha safari hiyo na kurejesha kiasi cha fedha walizopangiwa kwa shughuli hiyo.

Rais John Magufuli aliagiza viongozi wote pamoja na wasaidizi wao waliokuwa wamepanga kuhudhuria sherehe za kuzimwa kwa mbio za Mwenge mkoani Simiyu wasitishe safari zao na waliokwishachukua posho wazirejeshe.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us