Mkuu wa mkoa wa Mwanza amezindua meli kubwa ya kisasa yenye uwezo wa kubeba abiria 500 | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, October 16, 2016

Mkuu wa mkoa wa Mwanza amezindua meli kubwa ya kisasa yenye uwezo wa kubeba abiria 500

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela amezindua rasmi huduma ya usafiri wa meli kati ya Mwanza na mji wa Nansio wilayani Ukerewe katika ziwa Victoria, ambayo itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 500 magari madogo 40 na tani 284 za mizigo, hatua itakayosaidia kutatua changamoto ya huduma za usafiri wa abiria kwa wakazi wa kisiwa cha Ukerewe mkoani Mwanza.

Meli hiyo MV. Nyehunge II, imejengwa na kampuni ya Songoro Marine Transport kwa gharama ya shilingi milioni 800 na kufanyiwa ukaguzi na maofisa wa mamlaka ya udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini (SUMTRA), makao makuu Dar es Slaam.

Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Ukerewe, akiwemo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo George Nyamaha wanaeleza changamoto za usafiri zilizokuwa zinawakabili awali.

Meli zinazotoa huduma ya usafiri ndani ya ziwa Victoria kati ya Mwanza na Ukerewe, ni mv. Butiama inayomilikiwa na kampuni ya huduma za meli Tanzania pamoja na meli ya MV. Nyehunge.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us