Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki afariki dunia. | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, April 26, 2016

Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki afariki dunia.


Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki. Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. 
 
Alisafirishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.
 
Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki.
 
Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja .
 
Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.
 
Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.
Via>>BBC

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us