Mapigano ya wakulima, wafugaji yajeruhi wanne Bagamoyo | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, June 13, 2016

Mapigano ya wakulima, wafugaji yajeruhi wanne Bagamoyo

Mapigano ya wakulima na wafugaji yaliyotokea Alhamisi na kusababisha watu wanne kujeruhiwa katika Kijiji cha Makurunge wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani yamesababisha wilaya hiyo kuja na mkakati wa kuhakiki upya mifugo.

Uamuzi huo umetolewa na Baraza la Madiwani wilayani Bagamoyo baada ya kubaini kuwa bado kuna tatizo la kutoheshimiana kati ya wakulima na jamii ya wafugaji wilayani humo.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Ally Issa alisema kuna haja ya kuangaliwa upya uingiaji wa wafugaji hao kama ni halali au ni wavamizi tu ndiyo maana hawafuati matumizi bora ya ardhi waliyojiwekea.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us