Wanasayansi wasema Mugabe ana Vinasaba vya Kuishi Milele | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, June 13, 2016

Wanasayansi wasema Mugabe ana Vinasaba vya Kuishi Milele

WANASAYANSI maarufu kutoka Taasisi moja kubwa ya Sayansi nchini Uingereza wametoa ripoti ya utafiti walioufanya ikithibitisha kwamba, Rais wa Zimbabwe, Komrade Robert Mugabe amegundulika kuwa na vinasaba (genes) ambavyo vitamfanya aishi milele (asife).


Robert Mugabemiaka ya 1980.

Utafiti huo wa siri unaongozwa na Daktari Irvin Koch umegharimu mabilioni ya fedha na kugundua pia kwamba Bob Robert mwenye miaka 92 sasa haweki dawa kichwani (SUPER BLACK) wala hajawahi kukata nywele zake licha ya kutojihangaisha na kula vyakula vya mimea (veggies) ama kwenda gym kufanya mazoezi.

Katika tafiti hiyo, Wanasayansi hao walichukua sampuli mbalimbali kutoka kwa Bob ikiwemo damu yake, nguo zake, miswaki aliyokuwa akitumia, na hata chanuo kwa miongo kadhaa na kugundua kuwa hakuna hata chembe ya umauti kwa Mugabe.

Baadhi ya watu wameanza kuamini kuamini tafiti hizo baada ya kugundua kutoka kwenye picha za Mugabe akiendelea kupeta katika muonekano huohuo huku akiwa mwenye siha ya haja kwa miaka mingi sasa.

Mpinzani wake mkuu kwenye siasa za Zimbabwe ambaye ni Kongozi wa Chama cha MDC, Morgan Tsvangirai (ama kwa kuguswa kwamba ausahau uraisi) amejibu kwa kejeli kwamba ‘Mugabe ni makusanyo ya nyama na mifupa kama hayawani wengine wote’ na kwamba kila nafsi itaonja mauti (Kulu ‘nafsi dhaaikatul ‘maut).

Inasemekana kwamba utafiti huo unaendelea mpaka mwaka 2018 ndipo utakamilika.

Source: Newssa/Mzansi Satire


google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us