Kikao cha Baraza la 9 la wawakilishi chaitishwa visiwani ZANZIBAR | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, March 27, 2016

Kikao cha Baraza la 9 la wawakilishi chaitishwa visiwani ZANZIBAR


Kufuatia kukamilika kwa uchaguzi wa marudio visiwani ZANZIBAR , Katibu Mkuu wa Baraza la wawakilishi YAHAYA KHAMIS HAMAD
Katibu Mkuu wa Baraza la wawakilishi YAHAYA KHAMIS HAMAD
 
Kufuatia kukamilika kwa uchaguzi wa marudio visiwani ZANZIBAR , Katibu Mkuu wa Baraza la wawakilishi YAHAYA KHAMIS HAMAD  ametangaza kuitisha kikao cha Tisa cha Baraza la Wawakilishi  siku ya jumatano tarehe 30 mwezi huu ili shughuli za baraza hilo ziweze kuanza kwa mujibu wa sheria.


 Akizungumza na waandishi wa habari Kisiwani UNGUJA HAMAD ametoa ratiba ya kuanza kwa shughuli za baraza ikiwemo uchaguzi wa spika na kuwaapisha wajumbe wateule 76 wa baraza hilo katika siku hiyo ya kwanza,  Siku ya pili ya kikao kutafanyika uchaguzi wa naibu spika na wenyeviti wa baraza.

 Tarehe 5 mwezi april utafanyika uchaguzi wa wajumbe wa baraza na uchaguzi wa wajumbe 5 watakao ingia katika bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Tarehe 6 mwezi April kikao cha baraza kitaahirishwa rasmi.

 Mpaka sasa mwanachama wa chama cha Mapinduzi ZUBERI ALI MAULID ndiye aliyechukua fomu ya kuwania nafasi ya Uspika wa baraza la wawakilishi

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us