Rihanna akasirika kufananishwa na Karrueche | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Monday, March 21, 2016

Rihanna akasirika kufananishwa na Karrueche


best-beauty-rihannaMwanamuziki Rihanna.
NEW YORK, Marekani
MWANAMUZIKI Rihanna, amekasirishwa na kitendo cha ‘ex’ wake, Chris Brown kumfananisha na wanawake wengine aliowahi kutoka nao kimapenzi.
Hivi karibuni Chris alipost kwenye Instagram picha aliyoiunganisha ikimuonyesha akiwa na
wanawake wanne tofautitofauti akifurahi nao sehemu mbalimbali, mmojawao akiwa ni Rihanna, wengine walikuwa Karrueche Tran, Draya Michele na Jasmine Sanders.
Karrueche-TranMwanamitindo  Karrueche Tran.
Rihanna amesema kitendo hicho ni kama Chris amemvunjia heshima kwa kuwa yeye ni mwanamke aliye juu zaidi kati ya wote waliowahi kutoka na Chris, hivyo hastahili kufananishwa na mwanamke yeyote kati ya hao.
“Hajapendezewa na kitendo cha kulinganishwa na wanawake wengine wa Chris, hasa huyu Karrueche,” alisema rafiki wa karibu wa Rihanna na kuendelea: “Hataki kumvunjia heshima mtu yeyote, lakini Riri ni zaidi ya wote hao. Kila sehemu yeye ataendelea kung’ara kama almasi na haitabadilika kuwa ni zaidi ya wanawake wote aliowahi kuwa nao Chris.”

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us