Oparesheni dhidi ya ugaidi yawageukia polisi Ubelgiji | KINGAZI BLOG

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Tuesday, March 15, 2016

Oparesheni dhidi ya ugaidi yawageukia polisi Ubelgiji

Oparesheni dhidi ya Ugaidi nchini Ubelgiji
Vikosi vya maafisa wa usalama nchini Ubelgiji vinawasaka watu wawili baada ya maafisa wa polisi kufyatuliwa risasi katika oparesheni dhidi ya ugaidi katika mji mkuu wa Brussels.

Kisa hicho kilitokea katika makaazi ya kusini ya Forest.Maafisa watatu walijeruhiwa huku mmoja wao akijeruhiwa vibaya.
Mwendesha mashtaka amesema kuwa uvamizi huo unahusishwa na shambulio la Paris ambalo liliwaua watu 130 mwezi Novemba.
Maafisa wa polisi wa Ubelgiji wamekuwa wakijaribu kuwasaka wapiganaji kutoka kwa kundi la Islamic State.
Baada ya kisa cha Jumaane ,maafisa wa polisi wamesema kuwa wanawasaka washukiwa wawili waliotorokea kwenye paa la nyumba.
Eric Van Der Sypt,msemaji wa waendesha mashataka hao waliambia AFP kwamba maafisa wa polisi walifyatuliwa risasi wakati wa shambulio hilo la jumanne mchana.
Ameongezea kuwa msako huo unahusishwa na uchunguzi wa shambulio la Paris.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us