Baada ya 
ripoti ya CAG kutangazwa, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji 
Francis Mutungi  amevitaka vyama vya siasa nchini kuwasilisha hesabu za 
Serikali (CAG) ya mwaka 2014/15 ndani ya siku 90 kabla havijachukuliwa 
hatua za kisheria.
Pia 
amevitaka vyama hivyo kuheshimu sheria za mashirika ya umma ambazo ni 
Sheria ya Ukaguzi wa Fedha za Umma, Sheria ya Fedha za Umma na Sheria ya
 Vyama vya Siasa
‘Tulishavikumbusha
 vyama vya siasa kuwasilisha bajeti zao,  baada ya kupata taarifa ya CAG
 hatua inayofuata ni kuangalia taarifa hiyo na kuchukua hatua‘ –Jaji Francis Mutungi 
‘Kama
 kutakuwa na sintofahamu katika mahesabu ya vyama vinavyopata ruzuku 
hatua ni pamoja na kukata kiwango kinachodaiwa,  lakini tumewaambia 
kwenye barua kuwa wana miezi mitatu ya kukamilisha suala hili‘ –Jaji Francis Mutungi
BOFYA HAPA KUONA VIDEO:ALICHOSEMA JAJI MUTUNGI KUHUSU RIPOTI YA CAG













